• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mh.Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Kanali Patrick Songea Awaagiza Viongozi Wote Kuongeza Kasi ya Kuwahudumia Wananchi Katika Maeneo Waliyopo Leo Tarehe 11.08.2020

Imetumwa : August 11th, 2020

Mh.Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Kanali Patrick Songea Mwenye Suti Akizungumza na Viongozi Hao Katika Ukumbi wa Maktaba ya Wilaya ya Kiteto, Kulia Kwake ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Emmanuel Mwagala na Kushoto kwake ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto Bi. Neema Nyalege.


 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Tamim Kambona  Aliyesimama Akizungumza Katika Kikao hicho, Kushoto Kwake ni Mh.Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Kanali Patrick Songea na Mwisho ni Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto Bi. Neema Nyalege.

 Katibu Tawala wa Wilaya ya Kiteto Bi. Neema Nyalege Aliyesimama Akizungumza Katika Kikao hicho


Viongozi mbalimbali Wakiwa Katika Kikao Hicho Kama Wanavyoonekana Kwenye Picha za Hapo Juu.






---------------------------------------- HABARI KAMILI ----------------------------------------



Haya yamejiri katika kikao cha viongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto yakiwahusisha Wakuu wa Idara na Vitengo, Maafisa Tarafa, Maafisa Watendaji wa Kata na Vijiji yaliyofanyika katika ukumbi wa Maktaba ya Wilaya Kiteto. Mkuu wa Wilaya huyo amesema "Kila mmoja anapaswa awe ana taarifa zote za ofisi yake ikiwa ni pamoja na kuwajua watumishi alionao kwa utendaji wao wa kazi kwa ujumla".

Baada ya majadiliano na viongozi hawa kuhusiana na baadhi ya migogoro ya ardhi, ilifahamika kwamba Sheria ya aridhi iko wazi juu ya mipango ya matumizi bora ya ardhi na iko vizuri chamsingi kwa viongozi ni kufuata taratibu za maamuzi ya maeneo yoyote katika kijiji kuamuliwa na mkutano mkuu wa kijiji kama sheria ya adhi ya namba 5 ya mwaka 1999 inavyoeleza, kisha mihutasari ya mikutano hiyo ndiyo msingi na dira ya mustakabali wa nini cha kufanya katika kijiji husika. Hata hivyo inajulikana kuwa daftari la wakazi au rejista ya wakazi ni muhimu kuwepo, kutekelezwa na kusimamiwa kisheria hili litasaidia kujua kila mtu katoka wapi, anakaa wapi na anafanya nini kwa madhumuni gani.

Kwa sasa kasi ya  utendaji wetu wa kazi haujaridhisha hivyo inatupasa kuongeza kasi zaidi, ugawaji wa vitambulisho vya wajasiriamali wadogowadodgo ni muhimu wapewe wote wanaostahili kama agizo la Mh. Rais Dkt. J. P. Magufuli alivyoagiza kwani hadi sasa wapo wajasiriamali ambao hawana hadi leo vitambulisho hivi, kwa hiyo mjitahidi wale wote wenye sifa za kupata vitambulisho wapewe haraka.

Maafisa Watendaji katika ngazi zote mkae katika maeneo yenu ya kazi siku zote, zingatieni kufungua ofisi za serikali na kufunga kwa muda mwafaka, tuwahudumie wananchi hawa kwani ndiyo wajibu wetu kwao na kwa serikali pia, cha msingi ukiwa kama kiongozi weka ratiba ya siku zipi katika wiki utakuwepo ofisini na zipi utakuwa kwenye miradi na kutembelea kazi mbalimbali za maendeleo ya vijijini.

Mh.Mkuu wa Wilaya huyo aliendelea kusisitiza kwamba "fanya kazi lakini hukatazwi kufanya kazi baada ya masaa ya kazi hili ni la kawaida ili kujiongezea kipato kama vile ufugaji na kilimo lakini kumbuka kujiongezea kipato ambacho ni halali, usitoroke kazini kwenda kufanya kazi zako mwenyewe. Suala la Kutilia mkazo ni kuwashawishi wananchi kujiunga katika bima ya afya ya jamii, ni muhimu sana kwani mtaji wa maskini ni nguvu zake mwenyewe lakini ni lazima mtu huyu awe na afya bora ndipo atazalisha kwa ufanisi.

Zamani watu wote waliokuwa wakimaliza masomo ya kidato cha 4 walikuwa wanaajiriwa wote bila shida lakini leo hii kuna changamoto nyingi za kupata ajira na vyuo ni vingi sana na wahitimu ni wengi mno ni maendeleo kwa kweli, kwa sasa tunapaswa kama wazazi, kama viongozi kuwaandaa watoto wetu hawa kuwa wajasiria mali na sio kutegemea kazi za maofisini "white collar job" kwani ukimuandaa mtoto kujiajiri baadaye hatapenda tena kazi za kuajiriwa atajitafutia yeye mwenyewe kazi na wazazi hatutahangaika tena na uzuri nchi yetu ni pana na yenye amani, mzunguko wa fedha upo vizuri, miundombinu wezeshi ipo barabara, usafirishaji, mawasiliano na vingine vingi hivyo fursa hizi zitumike kwa wao kujiajiri ipasavyo.

Tukumbuke kudumisha utawala bora kwa kuzingatia kusoma mapato na matumizi katika ngazi zote za mikutano mikuu ya kitongoji na kijiji pia ili kuongeza imani ya wananchi kwa serikali yao hii itarahisisha utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo yao kupitia muitikio chanya wa utoaji wa michango na usimamizi wa miraji mbalimbali ya kijiji husika kupitia kamati zao.











Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa