• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“ Mgogoro wa Irikiushibor na Mkungunero Utamalizwa Mezani” Mhe. Papian

Imetumwa : July 12th, 2018

Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian akizungumza na wakazi wa kijiji cha Irikiushibor katika mkutano wa hadhara uliofanyika  kijijini Irikiushibor mwishoni mwa wiki.

Mwenyekiti wa kitongoji cha Madukani  akifungua Mkutano wa hadhara kwa niaba ya mwenyekiti wa kijiji cha Irikiushor. Mkutano huo umefanyika  kijijini Irikiushibor  mwishoni mwa wiki.

Wakazi wa kijiji cha Irikiushibor wakiwa wamekusanyika kumsikiliza mbunge wao Mhe . Emmanuel Papian kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho mwishoni mwa wiki.

Wakazi wa kijiji cha Irikiushibor wakiwasilisha kero  kwa Mbunge wao Mhe. Papian kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji hicho mwishoni mwa wiki.



............HABARI KAMILI..................


Mbunge wa jimbo la Kiteto Mheshimiwa Emmanuel Papian amewataka wakazi wa kijiji cha Irikiushbor kuamini zaidi katika mazungumzo kama njia sahihi ya kumaliza mgogoro kati yao na hifadhi ya Mkungunero, badala ya kutumia nguvu. Mhe. Papian ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini Irikiushibor  mwishoni mwa wiki.


Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Papian amewasihi wanakijiji hao kuendelea kuwa watulivu wakati suala hilo linashughulikiwa.Hapa Mhe. Papian anasema “Poleni sana na matatizo yaliyowapata kutokana na hifadhi ya Mkungunero. Najua kabisa kwamba mmeumia sana na mmeghadhibika sana, lakini hili tunakwenda nalo polepole. Ninachoomba, sisi tutulie ,tuwe na imani kuwa suala hili linashughulikiwa .Nina uhakika kwamba tukienda nalo polepole tutafika mahali jambo hili litakwisha huku wote tukiwa salama”.


Aidha Mhe Papian  amewahakikishia wanakijiji hao kwamba mgogoro kati yao na Mkungunero utamalizwa na watakaa kwa usalama na amani. Akieleza jitihada zinazoendelea katika kutatua mgogoro huo.Mhe. Papian amesema “ Katika mkutano wetu wa Halmashauri kuu mwezi wa tatu tulijadili kuhusu suala hili, na tunaendelea nalo.Tumeshaonana na Mhe. Kigwangala mara kadhaa, tumezungumza, sasa tunakwenda kwenye ramani. Ninaamini kwamba kwa kukaa mezani tutapata mwafaka mzuri.Tunaendelea kushirikiana na mkuu wa mkoa , nawahakikishia kwamba jambo hili tutalimaliza”.


Kadhalika Mhe Papiani amebainisha mikakati waliyonayo sasa  katika kushughulikia mgogoro huo. Mhe Papian amesema “ Tuna mikakati mizuri ,kuweka mazingira mazuri kuwaokoa watu wetu ili muweze kukaa kwa amani.Tutakutana tena na Mhe. Kigwangala, tutazungumza nae ili tuone ni kwa namna gani suala hili linafika mahali linakaa sawasawa, tutakaa mezani ,tukishindwana na waziri tutakwenda kwa waziri Mkuu, kuhakikikisha kwamba jambo hili linafika mwisho”.


Nao wakazi wa kijiji cha Irikiushibor wamesema kwamba ,kwa jinsi ambavyo mbunge wao amezungumza nao kuhusiana na mgogoro huo ,wana imani nae, hivyo wanamuomba kama alivyosema yeye mwenyewe, basi aende akawatetee. Kwa sababu mgogoro huo wa mpaka ni tatizo kubwa  sana kwao, kwani eneo ambalo wao wanalitambua kama mpaka kati ya kijiji hicho na hifadhi, ni tofauti na ilivyo kwa upande wa uongozi wa hifadhi hiyo , jambo ambalo limekuwa likisababisha vurugu na hata kupigwa risasi, wakati wakichunga katika eneo ambalo wao wanasadiki kama ni eneo la kijiji chao,huku upande wahifadhi wakidai kwamba ni eneo la hifadhi.Wanakiji hao wamedai kwamba  wamekuwa wakifanyiwa vitendo vya ukatili vya kila namna pamoja na kuchukuliwa mifugo yao, ambapo hadi sasa ng’ombe 264 za  mwanakijiji mwenzao  zimechukuliwa, na zimezuiwa katika eneo la ofisi za hifadhi hiyo.


Katika hatua nyingine Mhe. Papia amezungumzia suala la elimu. Mhe. Papian amesema “Hapa kuna upungufu wa vyumba vya madarasa , pana upunguvu wa walimu. Afisa mipango ichukue hiyo changamoto ya upungufu wa vyumba vya madarasa ,tuingize kwenye mpango wetu wa maendeleo ,pesa yetu ya mfuko wa jimbo ikiingia tuchomoe tuchomeke hapo, tumalize hili tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa. Kuhusu Suala la walimu  nitazungumza na Mkurugenzi ili kuhakikisha kwamba katika walimu watakao ajiriwa msimu ujao,wanapatikana walimu watakaopangwa kuja kufundisha katika shule yetu ya Irikiushibor”.


 Wakati huo huo Mhe Papian amemtaka Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Irikiushibor Mwalimu Charles Mnyutwa kueleza sababu za shule hiyo kuwa ya mwisho katika matokeo ya mitihani.Ambapo mwalimu huyo amebainisha changamoto zinazowakabili katika shule hiyo, ikiwemo upungufu wa walimu, uhaba wa vyumba vya madarasa, umbali wa maeneo watoto wanakotoka hadi kufika shule ,pamoja na utoro.


Mnyutwa amesema kwamba, kutokana na umbali wanafunzi wamekuwa wakifika shule saa tatu asubuhi, na hao wanaofika saa tatu ni wachache, na kwamba wanafunzi wanakuwa wengi kuanzia saa sita mchana, hali ya kuwa vipindi vinaanza saa mbili kamili asubuhi. Na kwamba walimu wanakuwa wako tayari kuanza vipindi saa mbili, lakini katika muda huo wanafunzi wengi wanakuwa hawajafika shule, na hivyo kukosa vipindi vya asubuhi . Vilevile wanafunzi wengi ni watoro. Mnyutwa amesisitiza kwamba changamoto hizo mbili (utoro na umbali) ndizo hasa  zinazosababisha shule hiyo kufanya vibaya katika matokeo ya mitihani.


Akijibu kuhusu changamoto hizo , Mhe.Papian amewata wakazi wa kijiji hicho kuhakikisha kwamba watoto wao wanakwenda shule, na sio kwenda tu,bali wawahi kufika shule  ,wahudhurie vipindi vyote ili wawe  na maendeleo mazuri kitaaluma.Na kwamba atafika kijijini hapo wakati mwingine kwa ajili ya kukutana na wazazi pamoja na walimu wa shule hiyo, ili wajadiliane na  wapate ufumbuzi  wa changamoto hizo.


Mhe Papian ametembelea kijiji cha Irikiushibor , ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku saba  katika jimbo lake kukagua shughuli za maendeleo ,sambamba na kuzungumza na wapiga kura wake ili kusikia kero na changamoto zinazowakabili na kuzitafutia ufumbuzi.



............MWISHO.................

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa