• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Migogoro Inatuchelewesha Kupata Maendeleo” DC Kiteto

Imetumwa : October 5th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe Tumaini Magessa akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Chekanao,kata ya kiperesa, wilayani Kiteto.

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe Tumaini Magessa akisaini Kitabu cha wageni kabla ya kuanza kuhutubia  mkutano.

Mwenyekiti wa kijiji cha Chekanao akifungua mkutano.

Diwani wa kata ya Kiperesa  Mhe Habib Kiberenge akisalimia mkutano.

Kaimu Katibu Tawala (W) akimkaribisha Mh. Mkuu wa wilaya kuzungumza  katika mkutano huo.

Afisa Ardhi (W) Ndg. Damas Gulisha akizungumza katika mkutano huo

Kaimu Afisa kilimo na ushirika (W) Ndg. Antony Kwilasa  akizungumza katika mkutano huo


Wakazi wa kijiji cha Chekanao wakiwa wamekusanyika kumsikiliza Mhe. Mkuu wa wilaya  .

Baadhi ya wakazi wa kijiji cha Chekanao wakiwasilisha kero zao kwa Mhe. Mkuu wa wilaya.



.......HABARI KAMILI......





Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa amewataka wakazi wa kijiji cha Chekanao  kuacha migogoro, na badala yake wajikite zaidi katika shughuli za uzalishaji mali ili waweze kupata maendeleo. Mhe. Magessa ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika  kijijini  Chekanao ,kata ya Kiperesa , wilaya ya Kiteto jana mchana.

Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Magessa amesema” Haya mambo ya migogoro isiyokwisha yanatuchelewesha  kupata  maendeleo. Kama  mkuu wa wilaya sasa, mpango wangu ni kujikita katika kutafuta masoko, kwa sababu watu wanalima sana, na bei ya mazao ndani ya wilaya yetu iko chini sana. Nahitaji kushughulika kuhakikisha masoko yanapatikana  katika mikoa mingine, na hata nje ya nchi, ili mazao  yetu yauzwe kwa bei nzuri itakayo wanufaisha wakulima na kuwawezesha kujiendeleza kiuchumi. Lakini hilo halitawezekana kama migogoro ikiendelea. Kwa sababu tutabaki kila siku kukimbizana na matatizo ambayo ni matokeo ya migogoro, tunatumia muda mwingi kushughulikia migogoro, badala ya kufikiria jinsi ambavyo tutainua uchumi wetu ”.

Aidha Mhe. Magessa ameitaka serikali ya kijiji kuitisha mkutano mkuu wa kijiji ili kupanga matumizi bora ya ardhi ya kijiji , kama  njia ya kuondoa migogoro ya wakulima na wafugaji , ambapo watakaa na kupanga  na kukubaliana kutenga  maeneo ya mifugo, maeneo ya kilimo, maeneo ya makazi na maeneo ya hifadhi .

Akisisitiza kuhusu kuweka mpango wa matumizi bora ya ardhi kwa ajili ya kijiji hicho,  Mhe Magessa amesema “Hatuwezi kutenganisha kilimo na ufugaji, ni lazima mfanye maamuzi, mkubaliane kwamba ni maeneo gani mnalima,maeneo gani mnafuga.Na mkishakubaliana, kama wewe ulikuwa unalima eneo ambalo ni la mifugo ukubali kuondoka uende eneo la kilimo,kama ulikuwa unafuga eneo ambalo ni la kilimo, ukubali kuondoka uende eneo la mifugo. Baada ya kuweka mpango huo na kukubaliana ,wataalamu hawa watakuja kurasimisha. Hiyo ndiyo itakuwa salama ya kijiji, vinginevyo itakuwa ni ngumi mkononi, migogoro haiwezi kwisha”.

Kadhalika  Mhe Magessa amewashauri wakazi wa kijiji hicho kubadilika, na kuachana na kilimo na ufugaji wa mazoea,ambao hauna tija,badala yake walime kilimo chenye tija na kufuga kwa tija, ambapo watakuwa wakiwatumia  wataalamu wa kilimo na mifugo kulima na kufuga kwa kufuata kanuni za kilimo na ufugaji bora. Kwa kufanya hivyo wataweza kulima mashamba madogo na kuvuna mavuno mengi, sambamba na kufuga mifugo michache ambayo itakuwa na ubora unaotakiwa, itatoa maziwa mengi , na vilevile itauzwa kwa bei nzuri. Hivyo kupata muda wa kufanya shughuli nyingine za kiuchumi na za kijamii, vilevile kutapunguza tatizo la ukosefu wa ardhi, kwani hata wale ambao hawana maeneo ya kulima,  watapata , kwa sababu  watu hawatahitaji  maeneo makubwa sana kwa ajili ya shughuli za kilimo ,na mifugo itakuwa michache , itafugwa kwa utaratibu ,haitahitaji  maeneo makubwa sana ya malisho kama ilivyo sasa,ambapo wingi wa mifugo ni moja wapo ya sababu migogoro kati ya wakulima na wafugaji, ambapo kutokana na uhitaji wa eneo kubwa la malisho, baadhi ya wafugaji huingiza mifugo katika mashamba ya wakulima ili kulisha mifugo yao.

Katika hatua nyingine Mhe. Magessa amezungumzia suala la elimu, ambapo amewataka wazazi na walezi kuhakikisha kwamba watoto wote ambao wamefikia umri wa kwenda shule, wanakwenda shule,na wale ambao umri wao umesogea na hawajapelekwa shule waandikishwe katika Mpango wa Elimu kwa Walioikosa(MEMKWA) ili asiwepo mtu ambaye atakosa elimu.Mhe. Magessa amesisitiza kwamba suala la kuwapeleka watoto shule ni suala la lazima, na wala sio suala la hiyari.

Katika mkutano huo wanakijiji wa Chekanao wamewasilisha kero zao kwa Mhe. Mkuu wa wilaya ambapo kero kubwa ni kutokukamilika kwa mradi wa maji kwa muda mrefu jambo ambalo linasababisha wanakijiji  hao kuendelea kukosa kukosa  maji, ilhali wano mradi wa maji katika kijiji chao. Kero nyingine ni wafugaji kuchungia kwenye mashamba ya wakulima, na  mgogoro wa bwawa kwa wakazi wa kitongoji cha Kichwa cha tembo ,ambapo wanadai kwamba wafugaji wanaingiza mifugo na kuchafua maji katika bwawa  ambalo ndilo linalotumiwa na wakazi kitongoji hicho  kwa matumizi ya binadamu.

Mhe. Magessa ametoa majibu kwa baadhi ya kero , vilevile  ameahidi kufanyia kazi  kero zote zilizowasilishwa katika mkutano hou.Sambamba na  kufanya mkutano mwingine katika kijiji hicho ndani ya mwezi huu wa kumi kwa ajili ya kutoa majibu ya kero hizo ambazo hazijatolewa majibu,kufuatilia utekelezaji wa maelekezo aliyoyatoa , pamoja na kuzungumza na wanakijiji hao.






.......... MWISHO...........

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa