• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Aagiza Kuvunjwa kwa Makazi Holela Wilayani Kiteto

Imetumwa : January 16th, 2018



                           Mbunge wa jimbo la Kiteto Mhe. Emmanuel Papian,Mwenyekiti wa Halmashauri  Mhe. Lairumbe Mollel , Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri  ndugu Tamim Kambona , Kamati ya Ulinzi na usalama, viongozi wa kijiji ( Waliokaa kwenye viti)  pamoja na wakazi wa kijiji cha Kimana kata ya Partimbo wilayani Kiteto wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti alipokuwa akizungumza na  wakazi hao  katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.


                          Wakazi wa kijiji cha Kimana kata ya Partimbo wilayani Kiteto wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti alipokuwa akizungumza nao katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.


.......HABARI KAMILI......


Mkuu wa Mkoa wa Manyara Aagiza Kuvunjwa kwa  Makazi holela  Wilayani Kiteto

Mkuu wa mkoa wa Manyara Mheshimiwa Alexander Mnyeti ameagiza kuvunywa kwa makazi holela yaliyojengwa katika kata ya Partimbo.Na wamiliki wa makazi hayo kuhamia katika kijiji cha Kimana,ambacho ni kijiji halali . Mhe. Mnyeti ametoa agizo hilo  katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Kimana kilichopo kata ya Partimbo wilayani Kiteto.


Akizungumza wakati anatoa agizo hilo Mhe. Mnyeti anasema “Mkuu wa wilaya nakuagiza, hakikisha unasafisha barabara yote, kote kwenye makazi holela.warudishe hapa,wakae hapa,na mji huu utakuwa mkubwa sana.Maana taarifa niliyonayo nimeambiwa wako watu hapa wanasubiri msimu wa kilimo wanakuja kulima na kuondoka.Kama huwezi kuishi nenda kwenu kaishi. Manyara sio sehemu ya kuchezea,Mnakuja kulima,baada ya mavuno mnawaachia watu takataka mnaondoka.Nataka nijue kama hiki ni kijiji,kitongoji au ni kitu gani.Nataka nikirudi  hapa nikute watu wote wamehamia kwenye kijiji hiki, na ulinzi na usalama uimarishwe na watu waishi kwa amani”.


Mheshimiwa Mnyeti pia amemtaka  Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini Magessa kusimamia kazi hiyo ya uvunjaji wa makazi  holela ,na ametoa mwezi mmoja kukamilika kwa kazi hiyo, ambapo amemtaka Mhe. Magessa kumpa taarifa ya namna alivyotekeleza maagizo hayo,mara  baada ya muda huo .


Katika hatua nyingine Mhe. Mnyeti  amewapongeza wakazi wa kijiji cha Kimana kwa kuheshimu mpango wa matumizi bora ya ardhi  .Wakati huo huo ametoa onyo kali kwa  wakazi wa kijiji hicho ambao hawaheshimu mpango wa matumizi bora ya ardhi na wavamizi wa mashamba ya watu kwamba  waache  mara moja kulima kwenye maeneo ambayo sio mashamba, kwani kufanya hivyo  ni kuchochea  migogoro . Mhe. Mnyeti anasema “Ukianzisha shamba jipya ambalo haliko kwenye utaratibu unatafuta ugomvi.Hatutaki kugombana.Mnapaswa mkalime kwenye maeneo ambayo mmekubaliana. Na waliovamia mashamba yasiyo ya kwao waondoke mara moja”.Mheshimiwa Mnyeti amewaambia wananchi hao kwamba wasiende kulima mashamba ambayo hawajui wamiliki wake.na ambayo hawajui wameyapataje kwani kufanya hivyo ndiko kunakosababisha migogoro.Hapa Mhe. Mnyeti anasema ‘‘Unakwenda kwenye shamba ambalo mwenyewe humjui, unaingiza trekta unalima.mwenyewe akija kesho mnapigana mikuki. Sasa hao wanaosababisha chokochoko  sitaki kusikia habari hii tena”.


Kata ya Partimbo ndio kata ambayo eneo lake kubwa limevamiwa na watu na kujengwa makazi holela.Makazi hayo ambayo yako nje ya utaratibu  yanasababisha wakazi wa maeneo hayo kukosa huduma muhimu kama shule, zahanati ,maji na umeme.



                                                                                                         ................. MWISHO................

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa