• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa wilaya ya Kiteto awataka madiwani kusimamia elimu katika kata zao

Imetumwa : October 29th, 2017

                                                                                                                                               

                                                      Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Mh. Lairumbe Mollel akifungua  kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto

                                                         Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya wilaya ya Kiteto Mh. Hassan Benzi akichangia hoja katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya  Kiteto                   Kaimu mkurugenzi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  ndugu Emmanuel Mwagala akijibu hoja za waheshimiwa madiwani katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto                                              

                                                                                                                                                                                                                      Kikao cha baraza la madiwani  kikiendelea  katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto


                                                                                                                                            

                                                                                                                                         

                                                                                                                                               

                                           Waheshimiwa mdiwani wakifuatilia kwa makini mijadala katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto

                                                                                                                                               

                                                                                                                                             



                                             Wataalamu wa fani mbalimbali wa halmashauri ya wilaya ya kiteto wakijibu hoja za waheshimiwa madiwani katika baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto


HABARI KAMILI...


Mkuu wa wilaya ya Kiteto awataka madiwani  kusimamia  elimu katika kata zao

Mkuu wa wilaya ya Kiteto mheshimiwa Tumaini Magessa amewataka madiwani kusimamia  elimu katika kata zao.Mkuu wa wilaya ameyasema hayo alipokuwa akitoa maelekezo ya serikali katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto.Akizungumza katika ukumbi wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto, mkuu wa wilaya amesema kwamba suala la elimu limekuwa tata katika wilaya ya Kiteto ,na mpango mkakati uliopo ni kuongeza kiwango cha elimu na ufaulu , na kwamba kila diwani kwenye eneo lake la kazi apite kila mahali kujua kama walimu wake wanakwenda shule, na kama wanakwenda shule,wafuatilie kama wanafundisha  inavyotakiwa. Mkuu wa wilaya amesema “Madiwani tufuatilie suala la elimu ili kujua tatizo liko wapi linalosababisha matokeo mabaya katika shule zetu.Tusipowasimamia walimu hatuwezi kuondoa tatizo la kushuka kwa elimu katika kata zetu.Tutafute njia ambazo tutatumia kuwabana  walimu katika  kata zetu ili wafanye kazi’’ .
 Mkuu wa wilaya amesema kwamba katika wilaya ya Kiteto bado kuna vijiji ambavyo havina shule,vijiji hivyo ni Ngapapa na Leluku ,na kumuagiza diwani wa kata ya Kijungu  mheshimiwa Mandalo Mussa kuhakikisha kwamba ifikapo tarehe 01 mwezi Novemba ujenzi wa madarasa katika vijiji hivyo unaanza kwa kutumia matofali yaliyopo ambayo yametolewa na wananchi wa vijiji hivyo,huku jitihada za haraka za kupata simenti na vifaa vingine zikiendelea kufanyika ili ujenzi huo uweze kuendelea na hatimaye madarasa hayo yaweze kukamilika ndani ya muda mfupi ili watoto wanaoishi katika vijiji hivyo waweze kwenda shule kwa urahisi, kwani kwa sasa shule ipo umbali wa kilometa kumi na saba (17) kutoka katika vijiji hivyo jambo ambalo linaweza kuwa sababu mojawapo ya matokeo mabaya na kushuka kwa kiwango cha elimu  katika wilaya ya Kiteto  kwani katika hali ya kawaida sio rahisi mtoto kutembea KM 34 kila siku kwenda  na kurudi shule ,watoto watakuwa wanaaga kwenda shule lakini hawafiki shule, wanafika shule  wakati wa mitihani ,matokeo yake wanafanya vibaya na kusababisha kushuka kwa ufaulu  katika wilaya.

Katika hatua nyingine mkuu wa wilaya ameelezea suala la pori la akiba la Mkungunero ambapo amesema kwamba suala la Mkungunero linahitaji historia  na uelewa,mkuu wa wilaya  alieleza historia ya mgawanyo wa maeneo uliosababisha mgogoro huo wa Mkungunero,na jitihada mbalimbali zilizofanyika katika kutatua mgogoro huo, na kwamba yeye kama mkuu wa wilaya amefanya jitihada binafsi ikiwemo kukutana na viongozi wa wilaya jirani ambazo ziko katika mgogoro kuhusiana na suala hio katika mikutano ya ujirani mwema,pia kukutana na waziri wa mali asili na utalii pamoja na uongozi mzima wa wizara hiyo, ambapo waziri wa mali asili amesema kwamba suala hilo lisifanyiwe maamuzi ya haraka ,hivyo baada ya kikao kati yake na uongozi wa wizara ya mali asili, iliamuliwa kwamba wizara zote tatu zinazohusiana na suala hilo (OR - TAMISEMI,wizara ya mali asili na utalii na wizara ya ardhi) zitakaa kujadili na kufikia maamuzi juu ya nini kifanyike kuhusiana na suala hilo.Baada ya maelezo hayo Mkuu wa wilaya amewataka madiwani kusubiri maelekezo ambayo yatatolewa mara baada ya wizara hizo kukaa .

Kadhalika mkuu wa wilaya amezungumza kuhusu zoezi la kupiga chapa ngo’mbe ambapo amesema kwamba kuna watu wanaeneza maneno ya upotoshaji kwamba ng'ombe zikipigwa chapa zitakaa miaka minne bila kuzaa ,hivyo amewataka madiwani wawaeleweshe wananchi wao umuhimu wa kupiga chapa ng’ombe.Mkuu wa wilaya amesema “Tunapotoka katika kikao hiki tuwe mabalozi wazuri kuhusu jambo hili.Tuwaeleweshe wananchi vizuri na kwa upole waelewe umuhimu wa zoezi hilo, ili lisikwame.

Mkuu wa wilaya pia amezungumza kuhusu ujenzi wa bomba la mafuta, ambapo litapita katika wilaya ya Kiteto, amesema kwamba ujenzi wa bomba la mafuta upo katika mchakato ,makampuni mbalimbali yanafika wilayani kiteto kwa ajili ya kufuatilia mambo mbalimbali kuhusiana na ujenzi wa bomba hilo .Makampuni hayo yapewe ushirikiano unaostahili ili kuunga mkono agizo la mheshimiwa Rais.

 Aidha shughuli za kawaida za baraza ziliendelea  kulingana na ajenda zilizokuwepo ambapo  taaarifa za miradi ya maendeleo kwa kwa kila kata ziliwasilishwa na kupokelewa ambapo  madiwani walieleza hatua ilipofika, miradi  hiyo ni ujenzi wa vyumba vya madarasa, nyumba za walimu, mabweni , zahanati na uhifadhi na usimamizi wa mazingira ya mlima simu.Katika kuwasilisha  taarifa hizo za miradi ya maendeleo, madiwani walielezea masikitiko yao ambapo wamesema kwamba kumekuwepo na tatizo ambalo ni serikali kutokuleta fedha za miradi,tatizo ambalo linasababisha miradi mingi kukaa muda mrefu bila kukamilika pamoja na jitihada za wananchi kuanzisha miradi hiyo na kuchangia gharama .

Pia madiwani waliwasilisha majina ya wajumbe wa mabaraza ya kata ,ambapo majina hayo yalipokelewa .Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto mheshimiwa Lairumbe Mollel aliwataka madiwani  ambao hawajawasilisha majina hayo kuhakikisha kwamba wanawasilisha kabla ya kikao cha kamati ya fedha na mipango,ili yaweze kujadiliwa na kupitishwa katika kikao hicho ili wajumbe hao waweze kupatiwa mafunzo na hatimae mabaraza hayo yaweze kuanza kutekeleza majukumu yake mapema iwezekanavyo.

Katika kikao hicho pia baadhi ya madiwani walizungumzia tatizo la kuwepo kwa popo katika majengo ya serikali ,ambapo popo hao wamekuwa wakiharibu  paa za majengo ,ilhali baadhi ya majengo hayo yakiwa bado ni mapya ,lakini huharibiwa na popo hao.Kutokana na kuwasilishwa kwa  tatizo hilo la popo, madiwani hao walishauriwa kutumia bati nyeupe za plastiki kupaua majengo katika maneo ambayo yameonekana kuwa na tatizo hilo la popo,kwani bati hizo huingiza mwanga,ambapo hali ya kuwepo kwa mwanga katika majengo hayo hufanya popo hao kuondoka.



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa