• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi Tumaini Magessa Asisitiza Ufanyaji Mazoezi kwa Watumishi Ili Kuimarisha Afya Zao.

Imetumwa : October 26th, 2019




Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi Tumaini Magessa Akikagua Mazoezi Hayo Katika Viwanja vya Michezo Kiteto Sekondari







Watumishi Mbalimbali  na Wanafunzi Wakijiachia Vilivyo na Mazoezi ya Viungo Kama Inavyoonekana Hapo Juu.Askari Mmojawapo Akitembea Juu ya Tumbo la Mkuu wa Kituo cha Polisi Kibaya Afande Partrick Kimaro Maarufu "Sabasita" Kwa Kuonyesha Ukakamavu wa Hali ya Juu Alionao.



Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi Tumaini Magessa Akitembea Juu ya Tumbo la Mkuu wa Kituo cha Polisi Kibaya Afande Partrick Kimaro Maarufu "Sabasita" Kwa Kuonyesha Ukakamavu wa Hali ya Juu.

Watumishi  Wakirudi Toka Mazoezini 


-----------------------------------------------     HABARI KAMILI     -----------------------------------------------



Wakati zoezi la usafi wa Kitaifa likiendelea kwa wananchi, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi Tumaini Magessa amesisitiza  watumishi wote wa Serikali kufanya mazoezi ya viungo mara kwa mara  ili kuimarisha afya zao. Maneno haya ameyasema leo asubuhi katika viwanja vya michezo shule ya Kiteto sekondari Mjini Kibaya Wilayani Kiteto. Awali mazoezi haya yalihusisha watumishi wa serikali zikikiwemo Taasisi mbalimbali za serikali kama vile Polisi, Magereza, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto na wanafunzi toka shule za bwneni za jirani kama vile Kibaya Sekondari, Bwakalo Sekondari na Kiteto Sekondari.

Mazoezi haya yalianza saa 12:00 asubuhi katika Kituo cha Polisi Kibaya Mjini kwa kukimbia mbio za kawaida hadi viwanja vya michezo vya Kiteto sekondari ambako kule mambo yalikuwa mazuri sana na kila mshiriki amefuraha sana ufanisi wa mazoezi haya yaliyodumu kwa muda wa masaa mawili na nusu.

Hata hivyo Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi Tumaini Magessa amesema ni muhimu kama mtu kajafanya mazoezi mazito kama haya basi ahakikishe anarudia tena kwa siku mbili tatu mfululizo ili kuuweka mwili sawa kwani bila kufanya hivyo mwili utakuwa na uchovu mwingi zaidi na hata kuugua viungo. 

Watumishi wote wanaofika katika mazoezi  haya wanashauriwa kuwa na mavazi ya staha na ya kimazoezi pia mfano kwa wanawake na wasichana ni muhimu kuvaa "track suit" na kiatu kinachoendana na raba lakini sketi ni nzuri kuvaa ila ni lazima mhuhusika aongeze na uvaaji wa suluari ndani au "track sout" na sio nguo nyepesi kama "skin tight" 

Wakiongozwa na wabobezi wa mazoezi haya yaani askari Polisi toka Kituo cha Polisi Kibaya na Kiongozi wao Mkuu wa Kituo Afande Patrick Kimaro maarufu kama "Sabasita"

Baada ya kufunga mazoezi haya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi Tumaini Magessa amesema tutaendelea na mazoezi haya Jumamosi ya wiki ijayo tarehe 02.10.2019 kwa kufuata muda ule ule wa saa 12:0 asubuhi  na mahali pa kukutana ni pale pale Polisi Kituoni Kibaya.




Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa