• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh.Mhandisi Tumaini Magessa Ashuhudia Red Star FC (Watumishi FC) Ilivyopambana Kufa na Kupona na Mahasimu Wao Royal FC ya Arusha Leo Tarehe 09.11.2019

Imetumwa : November 9th, 2019

Meza Kuu Katikati ni Mgeni Rasmi Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi  Tumaini Magessa Akiwa na (kulia kwake) Afisa Michezo (W) Bi. Juliana Mtei, Afisa Utamaduni (W) Bi. Hawa Masawika  na Kushoto ni Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kiteto Bw. Peter Nyigu Wote Wakiangalia Mechi za Shirikisho la Kombe la Azam Tanzania kwa Mwaka  2019/2020 Zilizofanyika Katika Uwanja wa Mpira wa Miguu wa Wilaya ya Kiteto.


Kushoto ni Mgeni Rasmi,  Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Mhandisi  Tumaini Magessa Akipokelewa na Mwenyeji wake Bw. Hamadi Muya Katibu Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kiteto.


Wadau Wakubwa wa Shirikisho la Kombe la Azam kwa Wilaya ya Kiteto  Benki ya CRDB Tawi la Kibaya "Ulipo Tupo" Nao Walijumuika na Mashabiki wa Timu Zote Mbili Uwanjani Hapa Kutoka Kushoto ni Joseph Kisipa, Edwin Swai, Lucy John na Diclan Assey. 


Wafanyakazi wa Benki ya CRDB Tawi la Kibaya "Ulipo Tupo" Kutoka Kushoto ni Edwin Swai, Joseph Kisipa,  Peter Nyigu ( Mwenyekiti wa Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Kiteto), Lucy John (Meneja Benki ya CRDB Kibaya) na Diclan Assey. 


Kamisa Bw. Haruna Kombo


Wachezaji wa Timu ya Red Star FC (Watumishi FC) ya Kiteto Wakifanya Mazoezi ya Viungo Muda Mfupi Kabla ya Kuanza Mpira.


Wachezaji wa Timu ya Royal FC ya Arusha Wakifanya Mazoezi ya Viungo Muda Mfupi Kabla ya Kuanza Mpira.




Wachezaji wa Timu Zote Mbili Wakipeana Salama za Kheri Tayari kwa Kuanza Mechi hiyo 

 Kutoka Kushoto Mwenye Jezi Nyekundu  ni Nahodha wa Timu ya Red Star FC Bw. Abdullaziz Kibwana  Wakipeana Mkono na Nahodha wa Timu ya Red Star FC (Watumishi FC) ya Kiteto Mwenye Jezi Nyeupe Kulia. 


Watatu Kutoka Kushoto ni Mwamuzi (Refa) Mwenye Jezi Nyeusi na Mistali na Anayefuata Ni Haruna Kombo Kamisaa wakiwa na Manahodha wa Timu Zote Mbili na "Lines Men" 

Timu ya Red Star FC ya Kiteto Muda Mfupi Kabla ya Kuanza Mechi Hiyo.


Hapo juu Mechi Inaendelea.

Timu Zote Mbili Zikienda Kwenye Mapumziko Baada ya Kipindi cha Kwanza Kuisha.

Hawa Ni Baadhi ya Watazamaji Waliofika Uwanjani Hapo.

Watoa Huduma Mbalimbali Walitumia Fursa Vizuri Katika Kujiongezea Kipato Kama Unavyoona Mpenzi Msomaji.



Huu ni Usafiri Uliotumiwa na Timu ya Royal FC Kutoka Arusha Kuja Kiteto.


-------------------------------------------------------------   HABARI KAMILI -------------------------------------------------------------


Mashindano haya ni ya Mechi za Shirikisho la Kombe la Azam Tanzania kwa Mwaka  2019/2020 ambapo kwa sasa ni hatua za awali za mtoano.

Kabla ya mechi kuanza kulikuwa na mvua kubwa iliyoanza kunyesha muda wa saa nane alasili na kufanya uwanja mzima kuwa na utelezi mwingi lakini baada ya kipenga kulia na Mwamuzi Christopher Kamula saa 10:13 jioni mpambano ulianza kwa mahasimu hao kila mmoja kuusoma mchezo wa mwenzake.

Katika mechi ya leo kila timu ilihitaji kuendelea na mashindano haya kwa kumfunga mpinzani wake, hata hivyo katika kipindi cha kwanza mchezazi machachari wa Royal FC Joseph Mpeka aliipatia bao la kwanza timu yake ambalo lilidumu hadi kipindi cha mapumziko, timu ya Red Star FC (Watumishi FC) ya Kiteto iliongeza nguvu kwa kubadilisha wachezaji wake, kujituma zaidi na kuongeza kasi ya uchezaji uwanjani ili kurudisha majibu kwa mashambulizi makali ya goli la Royal FC lakini wapi hali ilikuwa ngumu hadi kipindi cha kwanza kilipoisha.

Kwa ujumla mashabiki wengi mno waliojitokeza kuishangilia timu ya Kiteto yaani Red Star FC (Watumishi FC) walikuwa na shauku kubwa kuona timu yao inashinda haikuwa hivyo, kwani baada ya mapumziko kipindi cha pili timu ya Red Star FC (Watumishi FC) ya Kiteto ilipachikwa bao lingine la pili na mchezaji yule yule Joseph Mpeka, lililodumu hadi kufikia mwisho wa mchezo Royal FC 2 na Red Star FC (Watumishi FC) 0. Kwa matokeo haya Red Star imeaga rasmi mashindano haya na Royal FC ya Arusha inaendelea na mechi zijazo. 


Benki ya CRDB Tawi la Kibaya, "Ulipo tupo" hawakuwa nyuma kwani walishiriki ipasavyo katika kuhakikisha mechi hizi za Shirikisho la Kombe la Azam Tanzania kwa Mwaka 2019/2020 Wilayani Kiteto Mkoani Manyara wanapata huduma mbalimbali ili kufanikisha mechi hii.

Kwa upande mwingine kuwepo mara kwa mara kwa mechi kama hizi hususani za kutoka nje ya Wilaya huvutia watu wengi sana kushiriki kunakopelekea kuibuka kwa fursa mbalimbali za muda mfupi kwa wafanyabiarana na wajasilia mali kama vile nyumba za kulala wageni (Lodges & Guests), Usafirishaji "bodaboda, Taxis na daladala" Huduma za chakula na zingine pia hali hii huongeza mzunguko wa kifedha kwa eneo husika kupitia uwepo wa michezo hii.

Wakiongea kwa muda tofauti, wamesema tunawashukuru wote walioshiriki kwa namna moja au nyingine ili kufanikisha michezo hii na wawe tayari kwa mashindano mbalimbali yanayofuata huko mbele.










Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa