• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

MPANGO WA KUJIANDAA NA KUKABILIANA NA MAAFA KITETO

Imetumwa : November 3rd, 2024

Katika juhudi za kuboresha ufanisi wa kukabiliana na maafa Katika Halmashauri ya Wilaya Kiteto, Serikali kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, ilifanya kikao kazi cha Wakuu wa Idara na Vitengo kuanzia Oktoba 28-30,2024 wilayani hapo ili kuandaa mpango wa kujiandaa na kukabiliana na maafa. Kikao hiki kiliongozwa na wataalamu kutoka ofisi ya Waziri Mkuu, pamoja na wataalamu wa Shirika la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) na Mratibu wa Maafa wa Mkoa wa Manyara. Mbali na wataalumu hao kutoka Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, kikao kazi hicho kilihudhuriwa na wakuu wa taasisi zote wilayani hapa pamoja na wadau mbalimbali.


Katika kikao hicho, washiriki wa kikao hicho walijadili kwa kina mfumo na miongozo ya usimamizi wa maafa, wakilenga kuboresha mikakati ya kukabiliana na changamoto zinazoweza kutokea katika wilaya. Mada nyingine zilizozungumziwa ni pamoja na tathmini ya maafa katika halmashauri, ambayo itasaidia kutambua hatari na athari zinazoweza kuikabili jamii.


Aidha washiriki hao walijadili mgawanyo wa majukumu katika mpango wa kukabiliana na maafa, ili kuhakikisha kuwa kila taasisi inajua jukumu lake na inashirikiana kwa ufanisi katika kukabiliana na maafa. Aidha, kikao kilijikita pia katika kutathmini uwezo wa wilaya wa kukabiliana na maafa, ikiwa ni pamoja na rasilimali zilizopo na mahitaji ya kuongeza nguvu katika eneo hili.


Kikao hiki ni sehemu ya juhudi za muda mrefu za serikali katika kuimarisha usimamizi wa maafa na kuhakikisha kwamba jamii inakuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto za maafa. Wataalamu walisisitiza umuhimu wa ushirikiano kati ya serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali na jamii katika kuhakikisha kuwa mipango inayoundwa inatekelezwa kwa ufanisi.


Kikao kilihitimishwa kwa makubaliano ya kuandaa mpango mkakati ambao utawasaidia wakazi wa Kiteto kuwa na maandalizi mazuri ya kukabiliana na maafa, huku wakisisitiza umuhimu wa kuendelea na mafunzo na elimu kuhusu usalama wa jamii.


Kwa ujumla, kikao hiki kinaashiria hatua muhimu katika kujenga uwezo wa halmashauri ya Kiteto katika usimamizi wa maafa, na kuonyesha dhamira ya serikali katika kulinda maisha na mali ya wananchi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa