• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

‘‘Nimeboresha Makazi yangu kwa Fedha za PSSN’’ Mlengwa wa TASAF Wilayani Kiteto.

Imetumwa : February 15th, 2018

              

Mlengwa wa TASAF bibi Mariamu Kombo Mbaruku akiwa  na watoto wake nje ya nyumba yao. Nyumba hii ilikuwa ni chumba kimoja tu ,lakini Mama huyu aliweza kuongeza chumba kingine  kimoja kwa kutumia fedha za ruzuku za PSSN na kufanya nyumba hii kuwa ya vyumba viwili kama inavyoonekana sasa.

                                                                                                  

    .........HABARI KAMILI.......


‘‘Nimeboresha  Makazi yangu kwa  Fedha za  PSSN’’ Mlengwa wa TASAF Wilayani Kiteto


Mlengwa wa TASAF bibi Mariamu Kombo Mbaruku amesema  kwamba TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN) imemuwezesha kuboresha makazi yake. Bibi Mariamu ameyasema hayo nyumbani kwake ,katika kijiji cha Bwagamoyo wilayani Kiteto wakati alipotembelewa na Afisa Ufuatiliaji wa TASAF  ndugu Kishari Shegella ambapo amesema kwamba kwa kutumia fedha za PSSN ameweza kuongeza chumba kimoja katika nyumba yake .

 Akizungumza na ndugu Shegella bibi Mariamu amesema  kwamba kabla ya kuingia katika PSSN alikuwa akiishi kwenye chumba kimoja, lakini baada ya kuanza kupokea fedha za PSSN  ameweza kujenga chumba kingine.Hapa Bibi Mariam anafafanua zaidi anasema ‘‘Kabla sijaanza kupokea ruzuku ya TASAF nilikuwa na chumba kimoja, ambacho ndicho nilikuwa naishi na watoto wangu wote watano, lakini naishukuru TASAF kwani kwa kutumia fedha za PSSN nimeweza kuboresha makazi yangu kwa  kujenga chumba kingine . Nimeongeza chumba kingine ambacho nimejenga kwa matofali  na nimepaua kwa mabati’’.


Kadhalika bibi Mariamu amesema kwamba baada ya kuanza kupokea fedha za  PSSN alianzisha biashara ya kuuza mboga za majani,ambapo alitumia shilingi 15,000  kama mtaji anzia  wa biashara hiyo, na inampatia faida  isiyopungua  shilingi  2000 kila siku , fedha ambayo inamsaidia  kununua chakula . Bibi Mariamu ambaye ndiye mkuu wa kaya kwa sasa baada ya kufiwa na mumewe , kaya  ambayo ina jumla ya wanakaya 6 anasema, ‘‘ hali ya chakula nyumbani kwangu ilikuwa ngumu sana, mimi na familia yangu tulikuwa tunakula milo miwili tu kwa siku. Asubuhi tunakunywa uji na usiku tunakula ugali, mchana tulikuwa hatuli kabisa, lakini sasa hivi tunakula milo mitatu kwa siku, chai asubuhi, chakula mchana na chakula cha usiku”.

Kwa upande wa mavazi bibi Mariamu amesema kwamba PSSN inamuwezesha kupata mavazi , hususani sare za shule kwani kabla ya kuingia kwenye PSSN hakuwa na  uwezo wa kununua sare za shule za watoto wake watatu ambao ni wanafunzi, wawili wakiwa shule ya msingi na mmoja sekondari jambo ambalo lilikuwa linasababisha watoto wake kwenda shule na sare zilizochakaa sana,lakini baada ya kuanza kupokea fedha za PSSN  mambo yamekuwa tofauti . Bibi Mariamu anasema ‘‘ Kuna tofauti kubwa kabla ya kupata fedha za TASAF na sasa, sasa hivi watoto wangu  nimeweza kuwanunulia sare mbilimbili za shule, na nguo nyingine za kuvaa ,na  mimi mwenyewe naweza hata kununua kanga  , tofauti na ilivyokuwa siku za nyuma ambapo hali yetu kwa upande wa mavazi ilikuwa mbaya sana’’.

Aidha bibi Mariamu amesema kwamba kwa kutumia  fedha za PSSN ameweza kulima shamba ekari mbili na amepanda mahindi na alizeti,ambapo kama mvua zitakuwa za kutosha anategemea kuvuna mahindi magunia kumi na alizeti magunia manne .

Sambamba na hayo bibi Mariamu ameeleza mipango yake ya baadae ya maendeleo ambapo amesema kwamba ni kuongeza biashara yake ya mbogamboga, kuanzisha mradi wa ufugaji mbuzi,kondoo na kuku pamoja na kuongeza shamba kwa kukodi ili aweze kulima shamba kubwa zaidi ya ambavyo amelima mwaka huu .Bibi Mariamu  amesema kwamba anapokea fedha za PSSN shilingi 36,000 , anapozipata fedha hizo anajitahidi kuzitumia kwa uangalifu na kuweka akiba kidogo kidogo  ili aweze kufikia malengo yake.

                                                                                                                                 


                                                                                                                               ........... MWISHO.............

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa