• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu kwa Kushirikiana na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilayani Kiteto Waongeza Fursa za Uwekezaji Mradi wa Kitalu Nyumba kwa Vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

Imetumwa : June 5th, 2020

Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Tamim H. Kambona na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya Kiteto Bw. Christopher Simwimba


Hatua za Awali za Ujenzi wa Kitalu Nyumba


Hatua za Awali za Utandazaji wa Bomba za Umwagiliaji Ndani ya Kitalu Nyumba Hicho

Kutoka Kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Tamim H. Kambona Akimsikiliza Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Rodrick Kidenya Katika Kutoa Maelezo Ya Vijana Wanaoshugulikia Kitalu Nyumba Hiki na Kushoto ni Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya Kiteto Bw. Christopher Simwimba



Kutoka Kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Tamim H. Kambona  Akikagua Utekelezaji wa Mradi Huo na Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya Kiteto Bw. Christopher Simwimba 


Bw. Emmanuel Magubika Akipogolea Nyanya Husika Ili Ziwe na Afya Zaidi 



 Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya Kiteto Bw. Christopher Simwimba Akiwa Katika Ukaguzi wa Kitalu Nyumba Hicho 

Afisa Kilimo  na Umwagiliaji Bw. Balabala Pundungu Ambaye ni Mratibu wa Kitalu Nyumba Hicho 


Bw. Ezra Mariki Akinyunyizia Mbolea Katika Miche Hiyo ya Nyanya Kwa Ustadi na Teknolojia ya Kisasa na Kimamboleo 


Muonekano wa Nje wa Kitalu Nyumba Hicho na Miundombinu Mahususi ya Umwagiliaji Maji 

------------------------------------ HABARI KAMILI -----------------------------------



Vijana wapatao zaidi ya 100 toka katika kata 4 za Partimbo, Bwagamoyo, Kibaya na Kaloleni wamenufaika na  mradi wa Kitalu nyumba Wilayani Kiteto Mkoani Manyara baada ya kupata mafunzo elekezi ya siku 6 ya uzalishaji wa mimea aina ya nyanya kwa kutumia teknolojia ya kitalu nyumba mwezi Agosti 2020. Mafunzo hayo yalifadhiliwa na ofisi ya Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu na kusimamiwa na Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya chini ya wataalamu wake wa Idara ya Kilimo umwagiliaji na Ushirika kwa kushirikiana na idara ya maendeleo ya jamii ambayo ndiyo yenye vikundi hivi vya vijana.

Kimsingi kampuni ya  “Royal Agricultural Company Limited” ya Mkoani Morogoro ndiyo iliyopewa kazi hii na Ofisi ya Waziri Mkuu  kwa kutekeleza hili ileta vifaa, ilitoa mafunzo ya ujenzi wa kitalu nyumba na mafunzo ya kilimo kupitia teknolojia ya kitalu nyumba kwa vijana 100; Wataalamu wa Kilimo na wataalamu wa Idara ya maendeleo ya jamii walikuwa ni miongoni mwa wataalamu waliowezeswa.

Kwa mujibu wa Mratibu wa Kitalu nyumba  Bw.Balabala Pundungu ambaye ni Afisa Kilimo Msaidizi aliyeteuliwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya. Aidha, Kitalu nyumba hiki kina ukubwa wa eneo lenye upana wa mita 8 na urefu wa mita 30 zenye ujanzo wa miche 780 aina ya “Kibo Star “ yenye uwezo wa kuzalisha kwa  kila  mche mmoja kilo 10 hadi 11 baada ya kuanza kuvuna mzao ya nyaya .

Wataalamu wengine wa Kilimo ni  Catherine Hagile ambaye yeye ni mbobezi wa kilimo katika masuala ya mbogamboga na matunda (Horticulture) , Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii Wilaya ya Kiteto Bw. Rodrick Kidenya ambaye husimamia kazi za Afisa Vijana Wilaya kwa kufuatilia mahudhurio ya vijana hawa na mhimili wa shuguli hii ni  Bw. Christopher M. Simwimba ambaye ni  Mkuu wa Idara ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kwa ujumla wao hawa ndiyo husimamia shughuli zote za mradi huu  wa Kitalu nyumba.

Hata hivyo hii ni fursa pekee kwa vijana wa Halmashauri ya Wilaya ya  kiteto kutumia ujuzi huu ili kujiongeza kivingine namna ya kupata mtaji ili kuzalisha kibiashara kwa mtu moja mmoja, familia au kivikundi. Pia ni ajira kwa kuwa na elimu ya uzalishaji mazao haya kupitia teknolojia ya kitalu nyumba hivyo wamepanua wigo wa kufanya kazi ndani ya  Halmashauri ya Wilaya ya  kiteto na nje  pia  kwa ajili ya kujiletea maendeleo binafsi na taifa kwa ujumla.

Mwisho, tunaishukuru Serikali ya Awamu ya Tano kupitia Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge,Kazi, Ajira, Vijana na Walemavu, kwa kuleta mradi huu mkubwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kwani umefungua fursa lukuki kwa vijana, na sisi kama Halmashauri ya Wilaya tutahakikisha tunausimamia ipasavyo kadri iwezekanavyo ili matunda ya teknolojia hii yaendelee kwa vijana wengine wa wilaya hii.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa