• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

RC Manyara atoa kongole Kiteto

Imetumwa : June 1st, 2021

Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mh. Makongoro Nyerere leo tarehe 1 June, 2021 amepongeza halmashauri ya wilaya ya Kiteto kwa kupata

hati safi katika taarifa ya Mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali ya mwaka 2019/2020.


Mhe. Makongoro ameyasema hayo wakati akizungumza na baraza maalumu la madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto kuhusu

taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali akisema, majukumu ya mkuu wa mkoa yapo kwa mujibu wa sheria

Na. 19 ya mwaka 1997 kifungu cha 5 na kifungu kidogo cha (1) (2)


"Mkuu wa mkoa atakuwa na shughuli zote za serikali katika mkoa wake na kusimamia shughuli zote za msingi, kama vile ulinzi,

usalama na kusimamia sera za serikali za kisekta, kusimamia shughuli za utekelezaji wa maendeleo, kusimamia rasilimali fedha

na watu katika mkoa husika".


Alisema ziara yake kwenye kikao cha  baraza hilo maalumu la madiwani ni kuzungumzia taarifa ya ukaguzi kama ilivyowasilishwa

na mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali, kwa mwaka 2019/2020  akisema ukaguzi haumanishi kutafuta makosa bali ni

njia ya kubaini mapungufu na kushauri namna ya kuondokana ama kutojirudia kwa mapungufu hayo na kuleta ufanisi katika usimamizi

wa rasilimali za umma.


"Mhe. Mwenyekiti nimesoma taarifa ya mdhibiti na mkaguzi mkuu wa hesabu za serikali pamoja na maoni yake kuhusu usimamizi wa

hesabu kwa halmashauri yako kwa mwkaa 2019/2020, nichukue nafasi hii kukupongeza wewe mwenyewe na baraza lako pamoja na

wataalamu kwa kupata hati safi kwa miaka mitau mfululizo kuanzia 2017/2018, 2018/2019 na 2019/2020 hongereni sana"


Alisema kupata hati safi ni matokeo ya usimamizi mzuri uliofanywa na baraza lako, kamati za kudumu za halmashauri na menejimenti

hongereni sana... kwa kupata hati safi, akisema pamoja na kupata hati safi ya ukaguzi baraza lako  la madiwani lisimamie kikamilifu

manejimenti ya halmashauri yako.


Mweka Hazina wa wilaya ya Kiteto, Bi. Hadija Bofu akiwasilisha taarifa ya ukaguzi kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri

ya wilaya ya Kiteto Bw. Tamim Kambona alisema hoja nane za miaka ya nyuma zimefungwa na kusalia hoja tano ambazo zipo katika hatua

mbalimbali za utekelezaji


Alisema kati ya hoja 52 za mwaka 2019/2020, kati ya hizo 47 zimefanyiwa kazi na kufungwa, na hii ni kutoka na jitihada  zilizofanywa

na menejimenti kwa kushirikiana na kamati za kisekta hali iliyofanya halmashauri ya wilaya ya Kiteto kupata hati safi kwa mwaka 2019/2020.


kwa upande wake Kaimu Katibu tawala wa  mkoa wa Manyara Bw. Kenedy Kaganda ameeleza kuwa mkoa wa Manyara ni miongoni mwa mikoa

inayofanya vizuri katika taarifa za ukaguzi wa hesabu za serikali kutokana na kuwepo kwa mpango na mikakati ya kujibu hoja hizo huku

akisisitiza kuwa Wilaya ya Kiteto ambayo imejitahidi kuwa na hoja chache iendelee kupunguza na zibaki hoja za kisera tu,


Nao baadhi ya madiwani  baadhi ya madiwani wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto akiwepo Mhe. Paul Tunyoni na Hassan Benzi wamemuomba

mdhibiti na mkaguzi mkuu  wa hesabu za serikali kufuta hoja za miaka ya nyuma na ambazo halmashauri hazina uwezo wa kuzifuta kwa kuwa

ni madeni ya vyama vya ushirika AMCOS ambayo hayalipiki, huku Mhe. Mbunge wa Jimbo la Kiteto Wakili Edward Ole Lekaita akishauri kuwa

kesi zilizopo mahakamani kati ya halmashauri na mzabuni sheria ichukue mkondo wake.


Akizungumzia hali ya usalama, Mkuu wa wilaya ya Kiteto Kanali Patrick Songea, alisema hali ni shwari ingawa kuna changamoto za

mipaka katika hifadhi ya Mkungunero iliyopo wilayani Kondoa na vijiji vya wilaya ya kiteto akidai jitihada zinaendelea kutatafuta

ufumbuzi wake ingawa aliomba mkuuwa mkoa kuingilia kati katika jitihada hizo.











Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa