• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

SHULE 13 KITETO ZAKABIDHIWA KOMPYUTA NA MBUNGE.

Imetumwa : September 13th, 2023

Mbunge wa Jimbo la Kiteto, Mh. Edward Olelekaita  amesema kwamba muda wowote yupo tayari kufuatilia fursa mbalimbali kwaajili ya maendeleo ya kiteto.

Haya ameyasema Septemba 12, 2023 katika Ukumbi wa Maktaba kwenye  hafla fupi ya kukabidhi kompyuta mpakato kwa  wakuu wa shule  13 ambapo 11 ni kutoka shule za sekondari na wawili kutoka shule za msingi.  

Mh. Olelekaita alitoa rai kwa wakuu wa shule hao 13 kuzitumia kompyuta hizo kwa kuweka kumbumbuku ili  waweze kuongeza ufanisi katika majukumu yao.

“Kompyuta hizi zitawanufaisha sana. Kwa sekondari zilizobaki nazo zitapatiwa kompyuta mwakani kupitia mfuko wa jimbo. Kila wakati ikitokea mkasikia kuna fursa yoyote na kokote naomba mnijulishe nami  nipo tayari muda wowote kuzifuatilia, lazima Kiteto isikike vizuri”, aliongeza Mh. Olelekaita.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mtendaji (W), Bwana  Erasmo Tellun Ndelwa ambaye ni Afisa Mipango (W), amemshukuru sana mbunge huyo kwa jitihada zake ambazo amekua akizifanya katika kuchochea maendeleo ya Kiteto. Aliongeza kwa kusema kwamba Mh. Olelekaita amekua mstari wa mbele katika kufuatilia na kuhakisha pesa zote ambazo zipo kwenye bajeti zinafika halmashauri kwa wakati.

Nae Afisa Elimu Sekondari (W), Bwana Ally Kichuri, alisema kwamba idara ya elimu msingi  na sekondari inamshukuru sana Mh. Olelekaita kwakua amekua akizisaidia idara hizo katika mambo mengi ikiwemo kufuatilia na kuhakikisha Kiteto inapata shule mpya.

Mmoja ya wakuu wa shule hizo, Bwana Asheri Lowasa ambaye ni Mkuu wa Shule ya Sekondari Edward  Olelekaita, alimshukuru mbunge kwa niaba ya wenzake na aliongeza kwa kusema kwamba kompyuta hizo ni chachu ya kuwafanya waendelee kufanya vizuri zaidi.

Kompyuta zilizokabidhiwa zina jumla ya thamani ya shilingi 13,000,000. Mh. Olelekaita aliahidi kutoa kompyuta hizo akiwa kwenye ziara zake katika mwaka 2022/2023 maeneo mbalimbali  kwenye jimbo hilo.

Shule zilizopokea kompyuta hizo ni shule za msingi Boma na Laalakiri ilhali upande wa sekondari shule zilizopokea ni Dosidosi, Kibaya, Kijungu, Edward Olelekaita, Partimbo, Dongo, Magungu, Njoro, Kiperesa na ECO.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa