• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

SIDO Waendesha Warsha Kuhamasisha Mkakati wa Uanzishwaji na Uendelezaji wa Viwanda kwa Njia ya Kongano Mkoani Manyara Wilayani Kiteto Tarehe 04.07.2017

Imetumwa : July 10th, 2017

Bw. Sempeho Manongi ( Meneja wa SIDO mkoa wa Manyara) akitoa ufafanuzi  kuhusu Mkakati wa  uanzishwaji na uendelezwaji Kongano  wilayani Kiteto.


Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mh. Tumaini Magessa  akifungua warsha ya Mkakati wa Uanzishwaji na uendelezwaji Kongano iliyoandaliwa na SIDO mkoa wa Manyara.


Kaimu mkurugenzi  mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Bw. Rafael Makoninde  akizungumza katika warsha ya Mkakati wa Uanzishwaji na uendelezwaji Kongano iliyoandaliwa na SIDO mkoa wa Manyara.





Wataalamu wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakisikiliza kwa makini maelekezo katika warsha ya Mkakati wa Uanzishwaji na uendelezwaji Kongano iliyoandaliwa na SIDO mkoa wa Manyara .

Habari kamili

SIDO Mkoa wa Manyara  Waendesha Warsha  Kuhamasisha Mkakati wa Uanzishwaji wa Viwanda kwa  Kutumia Dhana ya Kongano Wilayani Kiteto.
 SIDO mkoa wa Manyara  wameendesha warsha ya kuhamasisha mkakati wa uanzishwaji wa viwanda  vya Kongano. Warsha hiyo imefanyika katika  ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya kiteto ikiwahusisha Mkuu wa wilaya ya Kiteto, kaimu mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto na wataalamu wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto.

Mwezeshaji katika warsha hiyo meneja wa SIDO mkoa wa Manyara bwana Sempeho Manongi amesema kwamba  ili uanzishwaji viwanda kwa kutumia dhana ya uendelezaji Kongano uweze kufanikiwa katika wilaya ya Kiteto halmashauri ya wilaya inatakiwa kuainisha  rasilimali zilizopo, rasilimali hizo      zitumike  kuanzisha viwanda  vidogo. Hata hivyo bwana   Manongi amesema kwamba ili rasilimali hizo ziweze kuwa fursa na wajasiliamali waweze kuzitumia kuanzisha viwanda, ni lazima  halmashauri  iweke mazingira wezeshi ambapo  uanzishwaji na uendelezwaji wa kongano za viwanda  utawezekana. Halmashauri zinatakiwa kutenga  maeneo ya kutosha , pia kwa kutumia wataalamu wake, halmashauri ifanye  juhudi  katika kujenga uelewa kwa wananchi, hii ikiwa   ni pamoja na uwasilishwaji wa mkakati wa SIDO na uundwaji wa kamati  ya  wilaya ambayo  itakuwa  mahususi kwa ajili ya  kuwaunganisha walengwa wa Kongano  na wataalamu  wilayani Kiteto.

 Serikali ya awamu ya tano imeweka msisitizo katika  kuhamasisha uanzishwaji  na uendelezwaji wa viwanda.Wadau muhimu ; wazalishaji wa malighafi, wasambazaji, wafanyabiashara, wasafirishaji, wanunuzi na wauzaji  wajengewe  uelewa  wa dhana  ya Kongano  za viwanda zinazojikita katika rasilimali zilizochaguliwa wilayani ambazo zitaendelezwa kwa ushirikiano kati ya wataalamu kutoka katika  halmashauri ya wilaya na wadau hao  kwa kutumia dhana ya mnyororo wa thamani. Dhana ya uendelezaji Kongano haihitaji kuanza  mambo mapya, rasilimali zinazopatikana katika wilaya  zinatumika kama fursa za uanzishaji  viwanda. SIDO  kama msimamizi wa maendeleo ya viwanda vidogo vidogo  Tanzania wanatoa huduma ya kuhamasisha uwekezaji katika sekta ya  viwanda vidogo na biashara ndogo kulingana na fursa zilizopo, wanatoa huduma ya mafunzo, huduma ya teknolojia, msaada wa masoko , na ndio wenye jukumu la kuhamasisha  halmashauri kutenga maeneo kwa ajili ya uanzishwaji wa Kongano.

Aidha dhana ya Kongano ni muhimu sana katika uendelezaji  viwanda kwani  Kongano za viwanda zinasaidia katika kurahisisha mawasiliano na taarifa, kupata teknolojia, kuongeza ujuzi, kuongeza uwezo wa kuzalisha, ushirikiano, kupata masoko, kupata huduma wezeshi kirahisi kama vile huduma za kudhibiti ubora na viwango  kutoka katika taasisi kama vile TBS na TFDA na pia kurahisisha uwezeshaji kupitia serikali au wahisani. Hivyo kwa kuzingatia jografia ya  wilaya  ya Kiteto, hususani mji wa Kibaya ambao  unakua kwa kasi, pia ni njia panda ya kuelekea miji mingine  kama Dodoma, Dar es Dalaam, Babati na Tanga , ni soko la wakulima na bado una fursa ya kupangwa. Uanzishwaji wa viwanda  vidogo  vya kusindika mazao ya kilimo na mifugo,Kuzalisha bidhaa za ngozi, kuzalisha vyuma,  kuzalisha  samani, matengenezo ya magari na uwekezaji katika  vyuo vya ufundi, utakuwa na mafanikio makubwa sana.

“ KONGANO’’  ni mkusanyiko wa viwanda vilivyo karibu karibu  vinavyofanya shughuli zinazofanana  au kushabihiana vikisaidiwa na watoa huduma mbalimbali wanaolenga shughuli za kongano husika.



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • JAMII YAASWA KUZINGATIA HAKI ZA WATOTO.

    June 16, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa