• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

"Stawi Ulipopandwa na Ulete Mabadiliko”, DC Mwema.

Imetumwa : September 16th, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Remidius Mwema amewasisitiza watumishi wa ajira mpya wilayani hapa kufanya kazi kwa bidii maeneo waliyopo  badala ya kutamani kufanya kazi mijini pekee.


Akizungumza Septemba 16, 2025 wakati wa ufunguzi wa mafunzo elekezi kwa waajiriwa wapya wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mhe. Mwema alisema maendeleo ya kweli hayaletwi na mazingira bali na bidii ya mtu binafsi.


“Huhitaji kuwa mjini au kuwa na nafasi kubwa ili uweze kuleta maendeleo na mabadiliko ni vizuri kila moja astawi alipopandwa", alisema Mhe. Mwema.


Mhe. Mwema aliendelea kuwaasa kwamba kila mmoja atengeneze alama kwenye eneo lake la kazi kwa kufanya kazi kwa bidii na weledi.


Hata hivyo Mhe. Mwema aliwataka  watumishi wa wapya wajifunze vizuri mazingira yao ya kazi akieleza kua hawawezi kufanya kazi kwa ufanisi endapo hawana uelewa mzuri wa mazingira yao kazi.


Sambamba na hayo Mhe. Mwema aliwakumbusha watumishi wa ajira mpya  kutambua majukumu yao, kuheshimu mipaka ya kazi na kufuata sheria, taratibu na miongozo ya utumishi wa umma.


Aidha, Mhe. Mwema alisisitiza maadili na matumizi bora ya teknolojia kwa kuepuka matumizi mabaya ya mitandao ya kijamii.


"Kesho yako ipo mikononi mwako, utaijenga wewe au utaibomoa wewe", aliongeza Mhe. Mwema.


Mafunzo hayo ya siku moja yalihudhuriwa pia na Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, CPA Hawa Abdul Hassan ambaye alihitimisha mafunzo ya waajiriwa wapya.


Mafunzo hayo yalitolewa kwa Watumishi wa ajira mpya  kutoka Idara  ya Utawala, Kilimo na Mifugo, Ununuzi na Ugavi, Biashara pamoja na Michezo na Utamaduni.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • "KURA YAKO HAKI YAKO, JITOKEZE KUPIGA KURA"

    October 27, 2025
  • MHE. REMIDIUS MWEMA AONGOZA MATEMBEZI YA AMANI KUHAMASISHA WANANCHI KITETO KUPIGA KURA

    October 27, 2025
  • WASIMAMIZI WA VITUO WAHIMIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UWAZI WAKATI WA UCHAGUZI

    October 26, 2025
  • MSIMAMIZI WA UCHAGUZI KITETO AWAASA MAKARANI KUTOKUA CHANZO CHA MALALAMIKO.

    October 25, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa