• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

SUNYA, NDIRIGISHI NA NJORO WATINGA KILELENI KATIKA KUTEKELEZA MKATABA WA LISHE KWA MWAKA 2024/25.

Imetumwa : July 23rd, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Kiteto, Mhe. Remidius Mwema Emmanuel, Julai 23, 2025 ameongoza kikao cha Tathmini ya Utekelezaji wa Mkataba wa Lishe katika kipindi cha Robo ya Nne (April-June 2025).


Kikao hicho kimebeba uzito wa kijamii kwa kuangazia mafanikio, changamoto na msukumo mpya katika utekelezaji wa mkataba huo.


Katika tathmini hiyo, kata ya Sunya imeshika nafasi ya kwanza kwa kuonesha viwango vya juu vya utekelezaji wa afua za lishe, ikifuatiwa na Ndirigishi na Njoro. Kata hizi tatu zimepongezwa rasmi na kupewa vyeti vya kutambua juhudi zao katika kuhakikisha watoto wanapata  chakula shuleni katika mwaka 2024/25.


Aidha, kata ya Magungu ilitajwa na kupongezwa kwa kuonyesha ongezeko la ufanisi licha ya kuwa haikuingia katika tatu bora. Hii ni dalili kwamba juhudi za kimkakati zinaanza kuzaa matunda hata kwa kata ambazo awali zilikuwa nyuma.


Kwa upande mwingine, kata ya Lengatei ilitajwa kama iliyofanya vibaya  katika robo hiyo ya nne na hivyo kukabidhiwa bendera nyeusi.


Mhe. Mwema ametoa msisitizo mzito kwa watendaji wa kata kuhakikisha wanasimamia kikamilifu utekelezaji wa mkataba wa lishe, huku akiwataka kuhakikisha wanafunzi wote wanapata angalau mlo mmoja shuleni kila siku.


Vilevile  amehimiza wazazi na walezi kushiriki kikamilifu katika mchakato huo kwa kutoa mchango wa chakula cha wanafunzi. 


"Tafsiri ni fupi, kile chakula ambacho angekula mtoto nyumbani unakipeleka shuleni maana muda wa kula anakua hayupo nyumbani anakua yupo shuleni", alisema Mhe. Mwema.


Matarajio na dhamira ya wajumbe wa kikao hicho ni kuhakikisha mwaka huu wa fedha ni kuona kata zote zikifanya vizuri katika utekelezaji wa mkataba huo kwa kuhakikisha watoto wote wanapata angalau mlo mmoja wakiwa shuleni lengo ni kuboresha afya ya wanafunzi na kuongeza usikivu wa wanafunzi hao wawapo darasani.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa