• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TEA Wakabidhi Nyumba kwa Halmshauri ya wilaya ya Kiteto

Imetumwa : August 20th, 2018

Mkurugenzi wa miradi wa TEA Ndg. Waziri Rajab Salum akimkabidhi  Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto nyaraka zinazohusu ujenzi  kama ishara ya makabidhiano ya nyumba za walimu zilizojengwa na kampuni ya Watumishi Housing (WHC) kwa ufadhili wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA).

Maafisa kutoka TEA na WHC, Wataalamu kutoka Halmshauri ,uongozi wa shule ya sekondari Lesoit pamoja na uongozi wa kijiji cha Lesoit wakikagua nyumba za walimu kabla ya makabidhiano

Nyumba za walimu ( 6 kwa 1) zilizojengwa na Watumishi Housing Company  kwa ufadhili wa  Mamlaka ya elimu Tanzania( TEA)  katika muonekano wake wa mbele.

Nyumba za walimu ( 6 kwa 1) zilizojengwa na Watumishi Housing Company(WHC) kwa ufadhili wa Mamlaka ya elimu Tanzania( TEA)   katika muonekano wake wa  nyuma.

Mkurugenzi wa Miradi wa Mamlaka ya Elimu Tanzania (TEA) Ndg. Waziri Rajab Salum  akisaini nyaraka wakati wa makabidhiano ya nyumba za walimu katika shule ya sekondari Lesoit.

Mhandishi  wa kampuni ya Watumishi Housing ( WHC)  Mhandisi L.J Mwandobo akisaini nyaraka wakati wa makabidhiano ya nyumba za walimu.

Mkurugenzi Mtendaji halmashauri ya wilaya ya Kiteto Ndg. Tamim Kambona akisaini nyaraka wakati wa makabidhiano ya nyumba za walimu

Kaimu Mhandisi wa ujenzi ( W) Mhandisi Chogo Magera  akisaini nyaraka  katika makabidhiano hayo




...............HABARI KAMILI..................





Mamlaka ya elimu Tanzania (TEA) wamekabidhi jengo lenye  nyumba  6 kwa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto.Makabidhiano hayo yamefanyika  mwishoni mwa wiki katika shule ya msingi Lesoit ambapo ndipo  zilipojengwa nyumba hizo.

Nyumba hizo ambazo zimejengwa na ‘Watumishi Housing Company’(WHC) zimekabidhiwa kwa Mkurugenzi wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto mahususi kwa ajili ya kuishi walimu wa shule ya sekondari Lesoit.

Akizungumza baada ya makabidhiano hayo  Mkurugenzi wa  miradi wa TEA  ndugu Waziri Rajab Salum  ameipongeza ‘Watumishi Housing Company’ kwa kazi nzuri waliyoifanya, sambamba na kuwapa muda wa mwezi mmoja kurekebisha mapungufu madogo madogo ambayo yameonekana wakati wa kukagua  nyumba hizo.

Aidha ndugu Waziri ametoa maelekezo kwa mwalimu mkuu wa shule ya sekondari Lesoit  Mwalimu Peter Nada kuhakikisha kwamba walimu wanahamia na kuishi katika nyumba hizo mapema iwezekanavyo. Akisisitiza kuhusu nyumba hizo kuanza kutumika ndugu Waziri anasema  “kimsingi nyumba ziko vizuri na ziko tayari  kwa ajili ya kuwasaidia walimu wetu wanaokaa mbali waweze kukaa karibu na wanafunzi wao .Marekebisho ambayo tumekubaliana kwamba WHC watayafanya,naamini watayafanya, na  watayakamilisha ndani ya mwezi mmoja, wakati marekebisho hayo yakiwa yanendelea,walimu waingie waendelee kuishi katika nyumba hizi.”.

Kwa upande wake Mhandisi wa WHC ndugu  L.J. Mwandobo amezishukuru mamlaka zote ambazo wameshirikiana wakati wote wa utekelezaji hadi kukamilika kwa mradi huo.Vilevile amewashukuru walimu na serikali ya kijiji kwa ushirikiano waliouonyesha wakati wote.Mhandisi Mwandobo amesema kwamba mara nyingi kazi za ujenzi huwa zinaambatana na wizi wa vifaa ,hususani kusipookuwa na serikali ya kijiji makini katika kulinda mali ambazo ni za serikali ,vitu vingi huwa vinapotea,hali inayosababisha serikali isifikie malengo katika miradi husika,lakini kwa Lesoiti hali imekuwa tofauti,kwani hakukuwa na upotevu wa kifaa chochote cha ujenzi.

Kuhusu mapungufu yaliyoonekana wakati wa kukagua nyumba hizo kabla ya makabidhiano, mhandisi Mwandobo amesema ,” Ninaamini kwamba sisi ‘Watumishi housing’ pamoja na mamlaka ya elimu(TEA) tutaweza kuweka utaratibu,kuhakikisha kwamba kila kitu kinakwenda kama ambayo tulivyokuwa tunatarajia”.

Naye Mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona amewashukuru TEA kwa ujenzi wa nyumba hizo, ndugu Tamim amesema “ Kwanza niwashukuru sana TEA, kwa ufadhili huu waliotufanyia, Kwa kweli wametukomboa ,tulikuwa na nyumba moja tu ya mwalimu, hapa Lesoit, sasa tutakuwa na nyumba saba za walimu,kwa hiyo changamoto ya uhaba wa nyumba za walimu kwa kiasi kikubwa imepungua.Kwa hiyo ningeomba na maeneo mengine pia watusaidie, kama tulivyoona kwenye yale mabweni na madarasa kwamba yanahitaji ukarabati mkubwa”.

Kadhalika kaimu mhandisi wa ujenzi wilaya ya Kiteto Mhandisi Chogo Magera   amepongeza kazi iliyofanyika . Sambamba na pongezi hizo Mhandisi Magera ametoa rai kwa TEA kwamba wakati mwingine watakapokuwa na miradi katika wilaya ya Kiteto watumie wahandisi wa Halmashauri kwani wana uwezo wa kufanya kazi nzuri na kwa gharama nafuu.

Katika hatua nyingine mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Lesoiti ndugu  Wilson Ranjili, amewashukuru TEA pamoja na ‘Watumishi Housing Company’ kwa kazi kubwa waliyoifanya kuwajengea nyumba nzuri sana. Na kwamba anaamini kwamba itakuwa ni chachu ya kuinua kiwango cha taaluma katika shule hiyo,kwani walimu wataishi katika mazingira mazuri , karibu na shule, hivyo  ari ya ufundishaji itaongezeka.

Kabla ya makabidhiano hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto alitembelea maeneo mbalimbali ya shule ya Lesoit , maeneo hayo ni mabweni ( bweni moja la wasichana na bweni moja la wavulana, madarasa na maabara ya somo la kemia na baiolojia), ambapo katika mabweni hayo  amejionea hali ya uchakavu wa dari na sakafu za mabweni hayo , ndipo  akatoa maelekezo kwa mwalimu mkuu wa shule hiyo kuitisha kikao cha bodi ya shule, kutathmini gharama inayotakiwa kutumika , ili ukarabati wa kuweka gipsam na sakafu katika mabweni hayo uanze mara moja.



.........MWISHO.............


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa