• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Tani 4 za Mahindi Yenye Sumuku Yameteketezwa tarehe 11.10.2019 Ikiwa ni Jitihada za Serikali Kunusuru Afya za Wananchi Wilayani Kiteto

Imetumwa : October 12th, 2019

Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Bw.Fadhili Dedani Akizungumza Kwenye Eneo la Uteketezaji Kijiji cha Partimbo.  

Mahindi Yenye Sumukuvu Yakimwagwa na Gari Tayari kwa Uteketezaji

Kaimu Afisa Afya Wilaya Bw. Keveratusi Sibanganya Akitoa Maelezo kwa Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya na Wadau Wengine Walioshiriki Katika Uteketezaji Huu.


Wahudumu wa Afya Wakianza Kazi ya Umwagiliaji wa Mafuta Aina ya Petroli Tayari kwa Uteketezaji.


Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Bw.Fadhili Dedani Akirusha Mti wa Moto ili Kuteketeza Mahindi hayo. 


Mbunge wa Jimbo la Kiteto Mh. Emmanuel Papian akiongea Eneo la Uteketezaji Baada ya kuwakuta Wataalamu wa Afya Wakiwa Eneo Husika Akiwa Katika Safari Zake. 



------------------------------ HABARI KAMILI ------------------------------

Katika kuhakikisha wananchi wanakuwa salama kiafya siku zote Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia Idara ya Afya na Mazingira, Mwezi Julai 2019 sampuli za  mahindi haya yalichukuliwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara na majibu yamepatikana mwezi Septemba 2019 yakionyesha kwamba haya mahindi yanakiwango kikubwa sana cha Sumukuvu. Gunia 38 ni za mfanyabiashara wa Kibaya aitwae Musa Mwamba na zingine gunia 8 zilitokea Kijiji cha Nalang'tomoni ndipo taratibu za kuteketeza mzigo huu zilifuata ikiwa ni pamoja na wahusika kujaza "Surrender Form" inayoonyesha kuridhia kuteketezwa kwa mahindi haya.

Kaimu Afisa Afya wa Wilaya ya Kiteto Bw. Kevaratusi Sibanganya alisema tunafanya hivi kutokana na kanuni na taratibu za kisheria ili kuwaweka salama wananchi wote  kwani zaidi ya watotot 9 wamefariki mwezi Julai 2019 katika Wilaya yetu ya Kiteto kutokana na Sumukuvu. Hadi sasa Hospitali yetu ya Wilaya haina vipimo vya kupima sumukuvu ila kitaalamu dalili za mtu kuwa na sumukuvu tunazitambua kwa binadamu yeyote kisha tunawapa rufaa ya kwenda Hospitari ya Benjamini Mkapa Dodoma. Hata hivyo wataalamu wa Shirika la Viwango nchini (TBS) Kanda ya Kaskazini tuliendelea kushirikiana nao katika ufuatiliaji zaidi wa mahindi mbalimbali ambayo yapo stoo na kaya 4 jirani toka Kijiji cha Ndirigishi kwa uchunguzi unaendelea ili kupata majibu na kuweza kuchukua hatua zaidi.
Mwakilishi wa Mkuu wa Wilaya Bw.Fadhili Dedani alisema elimu ya Sumukuvu ni endelevu lakini hadi sasa wataalamu wa Hospitali ya Wilaya, Vituo vya Afya na Zahanati wameshapewa Elimu hii na namna ya kutambua mgonjwa wa Sumukuvu kwa dalili za awali za kiafya kwa binadamu. hata hivyo Serikali imefanya jitihada kubwa sana za kutoa Elimu hii kwa wananchi kupitia Mikutano mbalimbali ya hadhara katika Vijiji na Vitongoji mbapo vipeperushi vinavyohusiana na Sumukuvu vilisambazwa Wilaya nzima kupitia maeneo  yote ya kutolea huduma za afya Wilayani Kiteto ili kufikisha ujumbe wa matumizi bora ya kilimo kuanzia ukuzaji wa mimea, wakati wa mavuno, uhifadhi wa mazao husika na wajibu wa mwananchi na Serikali katika kuhakikisha tunajikinga na kutokomeza ugonjwa huu katika Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, maelekezo yako wazi kwa kila mtu na wanajua kuwa mazao yakiwa na hali fulani ni dalili za sumukuvu kwa hiyo achukue jukumu mwenyewe la kuyateketeza mazao husika haraka au toeni taarifa ofisi ya karibu ya Serikali, isipokuwa kuna wananchi wanaokaidi maagizo haya, lakini yeyote atakayeenda kinyume na maagizo haya ya Serikali atachukuliwa hatua kali za kisheria.


Mbunge wa Wilaya ya Kiteto
Tunashukuru Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia Idara ya Afya na Mazingira kutekeleza haya kwa vitendo, lakini Wizara ya Kilimo wanalifahamu hili na ndiyo maana wametilia mkazo sana katika ufuatiliaji wa jambo lolote linalohusiana na sumukuvu katika Wilaya yetu.


MAKALA YA SUMU KUVU KUTOKA MAKTABA YETU.pdf

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa