• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

TIMU YA UKUSANYAJI MAPATO KITETO YAPONGEZWA.

Imetumwa : September 23rd, 2025



Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, CPA Hawa Abdul Hassan ameipongeza timu ya wakusanya mapato ya Halmashauri  kwa kazi kubwa na kujituma kwao, hatua iliyofanikisha ukusanyaji wa mapato kwa Mwaka wa Fedha 2024/2025 kwa kiwango cha asilimia 127.


Akizungumza katika kikao maalum cha mapato kilichofanyika wilayani Kiteto Septemba 23, 2025, CPA. Hawa alisema ufanisi huo umeifanya Halmashauri ya Kiteto kushika nafasi ya kwanza kwa ukusanyaji mapato katika Mkoa wa Manyara. Alisema mafanikio hayo yanatokana na mshikamano, uadilifu na bidii ya timu ya ukusanyaji mapato.


“Leo tumekutana kwa lengo la kuwapongeza kwa kazi nzuri mnayoifanya. Nawapongeza sana kwa kujituma. Mafanikio haya ni ushahidi kuwa tukizingatia maadili ya kazi, tukiwa waaminifu na kushirikiana, tunaweza kufanikisha kila jambo,” alisema CPA Hawa.


Katika kikao hicho, watu nane waliotambuliwa kama.wakusanyaji bora wa mapato kwa mwaka 2024/2025,  walikabidhiwa vyeti vya pongezi pamoja na zawadi ya fedha taslimu ikiwa ni ishara ya kutambua mchango wao katika kuongeza mapato ya Halmashauri. Vilevile wakusanya mapato wengine wote walipatiwa vyeti vya pongezi kwa kazi nzuri waliyoifanya ya ukusanyaji wa mapato.


Hata hivyo, watendaji hao waliwasilisha changamoto mbalimbali zinazowakabili wakati wa utekelezaji wa kazi. CPA. Hawa aliahidi kuwa ofisi yake itazifanyia kazi changamoto hizo, akibainisha kuwa nyingine zinaweza kutatuliwa haraka na nyingine zinahitaji mipango ya muda mrefu. 


“Nawaomba muwe wavumilivu, kwa sababu si kila tatizo linaweza kutatuliwa kwa haraka,” alisisitiza CPA. Hawa.


Aidha, alitumia nafasi hiyo kuwakumbusha wakusanya mapato kuwa waadilifu na waaminifu, akisisitiza kuwa uaminifu wao ndio msingi wa mafanikio endelevu.


Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mapato Wilaya ya Kiteto,Ndg. Prisca Mjema aliwasihi watendaji hao kuendelea kufanya kazi kwa bidii na kwa kuzingatia sheria, kanuni na taratibu ili kuepuka makosa yanayoweza kuwapeleka kwenye vyombo vya sheria.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

    October 07, 2025
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

    September 29, 2025
  • WITO WA LEO SEPTEMBA 29,2025

    September 29, 2025
  • TANZANIA YA TATU AFRIKA MPANGO RASMI WA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa