• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

''Tubadili Tabia ,Tutathmini Mchango wa Wanawake’’ DC Magessa

Imetumwa : May 30th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akihutubia wananchi kwa niaba ya mgeni rasmi(Makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ) katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake .

Wanawake  wakiandamana kutoka katika ofisi ya Mkuu wa wilaya  kuelekea uwanjani( chini ya mti) kwa ajili ya uzinduzi wa jukwaa la wanawake wilaya ya Kiteto.

Mwakilishi wa mgeni rasmi katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akikagua bidhaa mbalimbali zinazotengenezwa na vikundi vya wanawake wajasiliamali.

Diwani wa viti maalumu Kibaya Mhe. Zamzam Msabi akisoma risala ya wanajikwaa kwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake wilaya ya kiteto uliofanyika katika mji mdogo wa Kibaya.Aliyesimama upande wake wa kulia ni diwani wa  viti maalum Loorela Mhe. Esta Lemahati.

Mkuu wa wilaya ya Kiteto  Mhe. Tumaini Magessa akizungumza kwa niaba ya mgeni rasmi katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake (Makamu wa Rais wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan). baada ya kukabidhiwa zawadi maalumu kwa ajili ya mgeni rasmi.

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akizawadiwa na wanajukwaa katika uzinduzi wa jukwaa uliofanyika katika mji mdogo wa Kibaya .


......... HABARI KAMILI............





Mgeni rasmi katika uzinduzi wa jukwaa la wanawake wilaya ya Kiteto ambaye amemuwakilisha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Samia Suluhu Hassan, mkuu wa wilaya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa amesema kwamba wakati umefika sasa jamii ibadili tabia na kutathmini mchango wa wanawake katika kuleta maendeleo katika familia na taifa kwa ujumla.Mhe Magessa ameyasema hayo wakati wa uzinduzi huo ambao umefanyika katika  mji mdogo wa  Kibaya  mapema wiki hii.


 Akizungumza wakati wa hotuba yake Mhe. Magessa amesema  kwamba, kwa muda mrefu mwanamke amekuwa akionekana kama chombo cha kuzalisha mali,mtu asiye na sauti mbele ya mwanaume,na mlezi wa watoto. Lakini mwanawake ana mchango mkubwa sana katika kuleta maendeleo ya familia na taifa, malezi ya watoto na familia ,uzalishaji mali na kuinua pato la familia na taifa. Na kwa kuzingatia hilo,wanawake na wasichana wanastahili kupata elimu kama wavulana au wanaume wanavyopata elimu, na kupata ajira kama wavulan wanaume wanavyopata ajira, na wana haki ya kupata mgawanyo wa mali kama wanaume .Pia Mhe Magessa amaesema kwamba wanawake wanastahili kushiriki katika maamuzi.Akisisitiza kuhusu hilo Mhe ,Magessa amesema ‘‘ Pamoja na imani zetu za dini, mila na desturi zetu, wanawake washiriki katika maamuzi”.


Kadhalika Mhe. Magessa amezungumzia suala la malezi ya watoto ,ambapo amesema kwamba malezi ya watoto ni jukumu la wazazi wote wawili( baba na mama). Hivyo ni vema wazazi wote wawili kuwa karibu na watoto ili kufahamu matatizo yao na kuwafundisha maadili mema. Sambamba na hayo, amelitaka jukwaa la wanawake kuhakikisha kwamba linashirikiana na wanaume ili kutokomeza tatizo la mimba za utotoni, tatizo ambalo linakwamisha maendeleo ya watoto wa kike.


Katika risala yao kwa mgeni rasmi, wanajukwaa hao wametaja mambo makubwa matatu ya kuzingatia ili kupata maendeleo,Mambo hayo ni;  kila mtu kuwa na  maono ya kufika mbali katika maendeleo yake kuanzia katika ngazi ya familia, Kuthubutu na kuwa na ujasiri wa kujaribu jambo analoliamini kwamba litamtoa kutoka mahali alipo na kwenda katika hatua nyingine ya maendeleo na kuwa na moyo wa kujituma katika kutafuta maendeleo, ikiwa ni pamoja na kujiunga katika vikundi mbalimbali vya wajasiriamali.


Aidha wamesema kwamba uzinduzi wa jukwaa hilo utachangia kuwepo kwa fursa za ajira kwa wanawake na vijana.Uzinduzi huo unaenda sambamba na kauli mbiu isemayo ‘kuelekea uchumi wa viwanda , tuimarishe usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake kiuchumi’.Kauli mbiu ambayo inasisitiza juu ya umuhimu wa kutowabagua wanawake na kuwawezesha kushiriki katika shughuli mabalimbali za kiuchumi ili kujiletea maendeleo.


Uzinduzi wa jukwaa hilo ulianza kwa maandamano ambayo yalianzia katika ofisi ya mkuu wa wilaya(Bomani) na kuishia uwanjani (maarufu kama chini ya mti).Jukwaa la wanawake wilayani Kiteto lilianzishwa mwezi Mei 2017 na mkuu wa wilaya hiyo Mhe. Tumaini Magessa,lengo likiwa ni kuwakutanisha wanawake pamoja ili waweze kujadili fursa,changamoto na kushiriki kikamilifu katika biashara na shughuli  mbalimbali za kiuchumi.


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa