• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

“Tutahakikisha Miradi Yote Inakamilika kwa Wakati" DED Kiteto.

Imetumwa : February 17th, 2018



Mwenyekiti wa  halmashauri ya wilaya ya Kiteto  Mhe. Lairumbe Mollel akifungua kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto cha kupitisha  bajeti ya halmashauri  kwa mwaka wa fedha 2018/2019  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.

Mwenyekiti wa  halmashauri ya wilaya ya Kiteto  Mhe. Lairumbe Mollel akiendesha kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto cha kupitisha  bajeti ya halmashauri  kwa mwaka wa fedha 2018/2019  kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.

Mkurugenzi Mtendaji  wa  halmashauri ya wilaya ya Kiteto  Ndg. Tamim Kambona  akiwasilisha  bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto kwa mwaka wa fedha 2018/2019 wakati wa  kikao cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.

Katibu Tawala wilaya ya Kiteto Ndg. Stephano Ndaki akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa wilaya katika kikao cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto  kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.

Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Kiteto Ndg. Mohamed Kiondo  akizungumza wakati wa kikao cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto  kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.





Wahe. madiwani wa  halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto kwa mwaka wa fedha 2018/2019 wakati wa  kikao cha baraza la madiwani  cha kupitisha bajeti hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.


Wahe. madiwani wa  halmashauri ya wilaya ya Kiteto  wakitoa hoja  wakati wa kikao cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto kwa mwaka wa fedha 2018/2019 kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.


Wataalamu kutoka idara mbalimbali za halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakifuatilia kwa makini uwasilishwaji wa bajeti ya halmashauri ya wilaya ya Kiteto kwa mwaka wa fedha 2018/2019 wakati wa kikao  cha baraza la madiwani cha kupitisha bajeti hiyo kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri.



  ..................... HABARI KAMILI..................



“Tutahakikisha Miradi Yote Inakamilika kwa Wakati” DED Kiteto.


Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto ndugu Tamim Kambona amesema kwamba watafanya kila liwezekanalo kuhakikisha kwamba miradi yote ya maendeleo ambayo haijakamilika katika mwaka wa fedha  2017/2018  inakamilika katika mwaka  2018/2019.Ndugu Kambona ameyasema hayo katika kikao cha baraza la madiwani la halmashauri ya wilaya ya Kiteto cha kupitisha  bajeti ya halmashauri   kwa mwaka wa fedha 2018 /2019 kilichofanyika katika ukumbi wa halmashauri  mwishoni mwa wiki .


Ndugu Kambona amesema kwamba ipo miradi mingi ambayo haijakamilika kutokana na ukosefu wa fedha, lakini kwa mwaka 2018/2019  halmashauri imejipanga kukamilisha miradi hiyo ili iweze kutoa huduma kwa wananchi kama ilivyokusudiwa. Akizungumza wakati akijibu hoja mbalimbali za waheshimiwa madiwani ndugu Kambona anasema ‘‘naomba niwatoe wasiwasi waheshimiwa madiwani wote kwamba sisi tunaendelea kuvifanyia kazi vitu vyote.Kwa vile ambavyo viko kwenye bajeti na tunaona fedha hazifiki,tunapopata fedha zetu nyingine zozote tunaelekeza huko  ili tumalize.Lengo letu ni kuhakikisha kuwa miradi yote inakamilika. Miradi ambayo haijakamilika mimi inaniumiza kichwa kuliko ninyi waheshimiwa.Nataka miradi hii yote  tuliyonayo ambayo haijakamilika,yote ikamilike.Na ni lazima ikamilike. Tunajua fedha za miradi za mwaka huu tulionao tunaoumaliza hatujapokea hata senti moja,kati ya zile bilioni 1.2,fedha hizo nazo zikianza kufika tutazielekeza huko na miradi yote tutahakikisha inakamilika kwa wakati”. Ndugu Kambona  amesema kwamba mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha wa 2018/2019 umezingatia sheria ya bajeti  namba 11 ya mwaka 2015 .Vile vile mpango huo  pia  umezingatia ushirikishwaji wa jamii kuanzia ngazi ya vijiji na kata.


Aidha ndugu Kambona ameainisha vipaumbele vya halmashauri kwa mwaka wa fedha 2018/2019,vipaumbele hivyo ni; Kuboresha mapato ya ndani kwa kutumia mfumo wa kielekroniki,kufanya mipango ya matumizi bora ya ardhi katika vijiji 41 vilivyosalia,utoaji wa elimu bila malipo,ukamilishaji wa miradi ambayo haikukamilika katika mwaka wa fedha 2017/2018,ajira za watumishi na upandishaji wa vyeo,utawala bora kwa maana ya mikutano ya kisheria ikiwemo ndani yake,stahili za watumishi,kutenga asilimia kumi ya mapato ya ndani kwa ajili ya maendeleo ya vijana,wanawake na walemavu,kuongeza kiwango cha upatikanaji wa maji kutoka 37% hadi 55% ,kuongeza kiwango cha ufaulu wa kumaliza elimu ya msingi kutoka 60% hadi 80%, kuwezesha uanzishwaji wa viwanda vipya vidogo vidogo na vya kati 15,kusimamia amani na utulivu ili kuweka mazingira mazuri kwa wadau kutekeleza shughuli za maendeleo,pia kufanya ufuatiliaji na tathmini ya utekelezaji wa shughuli za maendeleo.


Kadhalika ndugu  Kambona ameainisha mafanikio yaliyopatikana katika mwaka wa fedha 2017/2018 ambapo katika sekta ya maji, halmashauri imefanikiwa kuchimba visima saba katika vijiji vya Ndedo, Makame,Kijungu,Ndirgishi Lembapuri,Engongare na Sunya ,kazi ya uchimbaji wa visima hivyo imekamilika, kazi ya kufanya usanifu kwa ajili ya usambazaji wa maji katika vijiji hivyo inaendelea ili maji .Katika sekta ya afya halmashauri imefanikiwa kuongeza upatikanaji wa dawa,vifaa tiba na vitenganishi kutoka 60% hadi 80%. Kuvuka kwa lengo la taifa la asilimia 90%  na kufikia  95% katika utoaji wa matone ya vitamin A kwa watoto wenye umri wa miezi 6 hadi miaka 5. Kufikia lengo la taifa la 60% katika huduma za uzazi wa mpango .Kwa upande wa elimu msingi imefanikiwa  kuboresha miundo mbinu katika baadhi ya shule,utengenezaji wa samani  kwenye shule za msingi na sekondari, ujenzi na ukamilishwaji wa vyumba vya madarasa na uboreshaji wa miundombinu. Katika sekta ya ardhi ,vijiji 22 vimeandaliwa mipango ya matumizi bora ya ardhi kwa lengo la kuondoa migogoro. Mashamba 3014 yamepimwa,ambapo mashamba 1205 yanaandaliwa hati miliki za kimila. Mipaka ya vijiji vyote 63 imepimwa upya na kupangiwa  ramani za upimaji  kwa kila kijiji.


Katika hatua nyingine ndugu Kambona  ameainisha changamoto mbalimbali zinazoikabili halmashauri katika mwaka wa fedha 2017/2018 ikiwemo kuchelewa  kwa ruzuku ya miradi ya maendeleo,ambapo amesema kwamba hadi kufikia mwezi  Desemba kiasi cha shilingi bilioni 2.6 tu sawa na 34% ya bajeti yote ndizo zilizokuwa zimepokelewa kati ya shilingi bilioni 7.7. Kukosekana kwa mvua za kutosha kumesababisha mapato kushuka, kwa kuwa mapato mengi ya halmashauri hutegemea mazao ya kilimo na mifugo. Sambamba na changamoto ndugu  Kambona  amebainisha mikakati ya halmashauri yake katika kukabiliana na changamoto hizo katika mwaka wa fedha 2018/2019, mikakati hiyo ni; kuendelea kufuatilia kwa karibu  upatikanaji wa ruzuku ya maendeleo kwa kupitia ofisi ya katibu tawala mkoa wa Manyara.Pia kuongeza vyanzo vipya vya ukusanyaji mapato ya ndani, ambapo halmashauri itaanza kukusanya mapato katika vyanzo vyake vipya vya mapato.Itaboresha miundo mbinu ya minada ili kuzuia ukwepaji wa ushuru na kuanzisha minada mipya,vilevile kuendelea kuhamasisha wananchi kushiriki katika shughuli za uchangiaji miradi ya maendeleo.


Katika kikao hicho bajeti  ya  shilingi  33,432,375,089 imepitishwa.Mapato ya ndani yakiwa ni shilingi 2,179,069,168, mishahara shilingi 22,432,026,741, miradi ya maendeleo 7,865,880,180 na matumizi mengineyo (OC)  955,399,000.




                                                                                                                               .................MWISHO......................


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa