• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

UFAULU MITIHANI YA KIDATO CHA NNE WAONGEZEKA 2023.

Imetumwa : February 17th, 2024

Ufaulu wa mitihani ya Kidato cha Nne katika Halmshauri ya Wilaya ya Kiteto umeongeza na kufika 90.6% kutoka 90%.

Hayo yameelezwa February 16, 2024 na Mkuu wa Idara ya Sekondari, Ndugu Ally Kichuri katika Kikao Kazi cha Tathmini ya Matokeo ya Mitihani kilichofanyika katika Ukumbi wa Maktaba wilayani hapo.

Kikao hicho pia kiliambatana na Hafla ya utoaji wa Vyeti vya Pongezi kwa shule zilizofanya vizuri pamoja na kwa walimu waliofaulisha vizuri masomo yao katika matokeo ya mitihani hiyo iliyofanyika Novemba 2023.

Mgeni Rasmi katika Hafla hiyo alikua ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto, Mh Abdala Bundala ambaye aliongozana na Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Jamii  WIlayani hapo, Mh. Kassim Msonde.

Mh. Bundala, aliwapongeza watendaji wote katika sekta ya elimu kwa kuongeza ufaulu huo. Pia Mh. Bundala alitoa rai kua  waliofanya vizuri wapongezwe na waliofanya vibaya pia waambiwe ukweli.

Mbali na hilo Mh. Bundala alisema kwamba, sekta ya elimu ni eneo ambalo linashika nafasi kubwa kwenye kuitangaza Halmashauri ambapo inaweza kuitangaza vizuri ama vibaya kutokana na matokeo ya mitihani ya Taifa.

“Hata tufanye vizuri kwenye mapato kama kwenye elimu hatufanyi vizuri tutaonekana wa hovyo”, aliongeza Mh. Bundala.

Nae Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, CPA. Hawa Abdul Hassan, aliwapongeza watendaji hao katika sekta ya elimu kwa kuongeza ufaulu na kusema kwenye matokeo ya mitihani ongezeko la 0.6% ni kubwa na anathamini jitihada zao ambazo zimepelekea ongezeko hilo la ufaulu.

Mbali na hayo Mkurugenzi aliwasihi watendaji hao kuendelea kupanga mikakati mizuri ya kuendelea kuongeza zaidi  ufaulu katika shule zao.

“Mikakati iwe mizuri yenye tija na yenye kutekelezeka. Msiishie kupanga tu, bali na kutekeleza hiyo mikakati” aliongeza CPA. Hawa Abdul Hassan.

Vyeti vya pongezi vilivyotelewa kwenye hafla hiyo ilikua ni pamoja na pongezi za kufuta daraja sifuri ambapo vyeti hivyo vimetolewa kwa shule mbili ambazo ni Magungu na Engusero ilhali shule ya Orkine Partimbo na Magungu zilipokea vyeti vya pongezi kwa kuongeza Ufaulu kwa Miaka Mitatu Mfululizo. Shule ya sekondari Bwakalo ilipata cheti cha pongezi kwa kuongeza ufaulu kwa mika mitatu mfululizo kwa upande wa mitihani ya kidato cha pili.

Aidha Kiteto na Engusero zilipokea vyeti vya kuwapongeza kwa kuendelea kufanya vizuri katika kidato cha sita ambapo zimeendelea kufaulisha kwa 100%.Vilevile Kiteto ilipata tena cheti cha pongezi kwa kufaulisha 51% ya wanafunzi daraja la I-III.

Kikao hicho cha Tathmini kilihudhuriwa na Wakuu wa shule za sekondari wote, walimu wa taaluma kutoka katika  shule hizo, Maafisa Elimu Kata; wataalamu wa Idara ya Elimu kutoka Ofisi ya Mkurugenzi, wataalamu kutoka Ofisi ya Mdhibiti Ubora na Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC) Kiteto.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa