• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Uzinduzi wa Mnada wa Njoro Wilayani Kiteto umekuwa kivutio na fursa kubwa kwa Wafanyabiashara wa ndani na nje ya Kiteto.

Imetumwa : April 22nd, 2017

Leo tarehe 22.04.2017 Kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) Kiteto Bw.John Malle (aliyeshika Mic) amezindua Mnada wa Njoro ulioko Kata ya Njoro umbali wa Kilometa 17 toka Makao Makuu ya Wilaya ya Kiteto (Kibaya Mjini). Kushoto ni Mheshimiwa Diwani Jimbo N. Maitei wa Kata ya Njoro.

Kwa juhudi za Halmashauri (W) kusukuma gurudumu la maendeleo ya Wilaya na Wananchi wake imesimamia kwa dhati kwa kushirikiana na wananchi wa Kata husika hadi kupata eneo hili la ekari kumi (10)

 kwa ajili ya shuguli za Mnada, huku uwekezaji wa miundombinu ya Barabara, Maji, Choo kikubwa na kisafi, Jengo zuri la Machinjio linalojitoshereza, 

Ulinzi mahususi wa Askari Polisi kwa usalama wa raia na mali zao upo muda wote. 

Vitu mbalimbali vya kuuzwa na kununua vinapatikana hapa kuanzia Mifugo (Ng'ombe, Mbuzi, Kondoo, Kanga, Kuku wa kienyeji wapo kwa wingi), mazao (Mahindi, Alizeti, Mbaazi, Mtama na Ulezi), Matunda,  bidhaa mbalimbali za madukani zinapatikana  kwa uhalisia wa gharama utakayoimudu basi ukisoma taarifa hii karibu Kiteto, karibu Mnada Mpya wa Njoro kila Jumamosi ya kila wiki.

Kutoka kushoto mwenye nguo ya rangi nyeupe ni Mshereheshaji Bw. Kimolo, wa pili ni Mhasibu wa Mapato (W) Bw. C. Mwigani, 

wa tatu aliyeshika Mic ni Kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) Kiteto Bw.John Malle akihutubia wananchi waliofika Mnadani hapo.


Lengo la Kuwepo kwa Mnada huu
kuongeza wigo wa eneo la watu wengi kuweza kufanya biashara,
Kuweka msingi wa kuimarisha masoko ya uchumi wa viwanda utakaokuwa na bidhaa nyingi.


Faida Kuwepo kwa Mnada huu
Kuongeza ajira katika jamii yetu kupitia kushiriki katika biashara na utoaji huduma mbalimbali,
Kuongeza kipato cha mtu mmoja mmoja na familia kwa ujumla.
Kurahisisha upatikanaji wa vyakula na huduma zingine muhimu.

Kwa ujumla wake yote haya hupelekea kuwa na maisha bora kwa kila Mtanzania.


Wananchi wakimpongeza Kaimu Mkurugenzi Mtendaji (W) Bw.John Malle kwa kumpigia makofi na kunyanyua mikono juu 

 ikiwa ni ishara ya kupokelewa vyema na kukubalika 

 uanzishwaji wa Mnada huu ambao ni chachu ya maendeleo ya kiuchumi na kijamii Kata ya Njoro na Kiteto kwa ujumla.



Afisa Mtendaji Kata ya Njoro Bibi Mariam akiwasalimia wananchi.


Katika uzinduzi huu Kaimu Mkurugenzi huyo amesisitiza mambo ya msingi yafuatayo:-

          - Wananchi kujituma katika kufanya kazi kwa bidii siku zote ili kujiletea maendeleo ya mtu binafsi, kaya na Taifa kwa ujumla

          - Kila mfanyabiashara kutumia busara katika kufanya biashara hapa mnadani bila kuanzisha tabia mbaya za vurugu, uwizi na

            vinginevyo vinavyofanana na hivi ili kuinua hali ya kibiashara ambayo itatunufaisha sisi wote.

          - Kila mtu aliyefika hapa leo awe mwakilishi mzuri wa kuutangaza mnada huu ndani na nje ya Wilaya ya Kiteto ili uendelee kukua.


Mifugo aina ya Kondoo katika mauzo



Mifugo aina ya Mbuzi katika mauzo


Mifugo aina ya Ng'ombe katika mauzo

Kuku  ambao mteja ameshawanunua amewaning'inIza anaondoka nao kwa Pikipiki maarufu "boda boda" kwenda nyumbani kwa biashara na kitoweo pia.


Mazao mbalimbali

Nyama Choma za Minadani

Nguo mbalimbali


Vyombo mbalimbali kwa matumizi ya nyumbani


Bidhaa mbalimbali


Machinjio nzuri na kubwa ya Mnadani hapo.

Choo kikubwa na kizuri cha kulipia


Watoa huduma ya usafirishaji nao hawako nyuma katika kujipatia riziki kupitia usafirishaji wa abiria na uchukuzi wa mizigo, Taxi, Pikipiki maarufu Bodaboda zote zinapatikana hapa.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa