• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Viongozi wa Ngazi za Chini Simamieni Utekelezaji wa Maagizo - RC Mnyeti

Imetumwa : January 19th, 2018



                                 Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti  akijibu kero mbalimbali zilizowasilishwa na wakazi wa kata ya Engusero katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Engusero wilayani Kiteto.


                       Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akifafanua jambo mbele ya  Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Engusero.


                                    Diwani wa kata ya Engusero  Mhe. Solomoni Mbulunyuku  akifafanua jambo mbele ya  Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Engusero.


                       Waheshimiwa madiwani ,wakuu wa taasisi mbalimbali za serikali  , kamati ya ulinzi na usalama ,kamati ya siasa pamoja na wakuu wa idara na vitengo wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto  wakimsikiliza  Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata  ya Engusero wilayani Kiteto.


                                    Wakazi wa kata ya  Engusero wakimsikiliza Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Engusero wilayani Kiteto .

                 Wakazi wa kata ya Engusero wakiwasilisha kero zao kwa Mkuu wa Mkoa wa Manyara Mhe. Alexander Mnyeti katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Engusero wilayani Kiteto.



                                                                                                                                  ...... HABARI KAMILI.......


Viongozi wa Ngazi za Chini Simamieni Utekelezaji wa Maagizo  -  RC Mnyeti

Mkuu wa Mkoa wa Manyara  Mheshimiwa Alexander Mnyeti  amewataka viongozi wote walio chini yake kusimamia utekelezaji wa maagizo yote anayoyatoa na yanayotolewa na viongozi wengine wa juu wa serikali.Mheshimiwa Mnyeti ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Engusero wilayani Kiteto.

Akizungumza katika mkutano huo Mhe. Mnyeti amesema kwamba Kiongozi anapotoa maagizo ni vema viongozi walio chini yake wakayasimamia na kuyatekeleza ili kuondoa malalamiko ya wananchi.Akisisitiza kuhusu utekelezaji wa maagizo Mhe. Mnyeti anasema ‘‘ Yale ambayo tutakubaliana katika mkutano huu nitayafuatilia kuhakikisha  kwamba yanazingatiwa na kufanyiwa kazi kwa wakati ili wananchi wasiendelee kupata shida. Inawezekana kabisa kwamba viongozi walishakuja hapa na kutoa maagizo,lakini  utekelezaji wa maagizo hayo  haukuzingatiwa na viongozi wa ngazi za chini. Mimi leo niko hapa maelekezo nitakayoyatoa hapa, naamini viongozi wote mlio chini yangu mtayazingatia na kuyasimamia  kuhakikisha kwamba wananchi wetu wanapungukiwa kero walizonazo”.


Vilevile Mhe. Mnyeti amesema kwamba  viongozi wanatakiwa kushughulikia  kero za wananchi  na kuzipatia majibu katika muda  sahihi ili wananchi wasiendelee kuelemewa na kero . Akisisitiza kuhusu viongozi hao kushughulikia shida za wananchi ,Mhe. Mnyeti anasema    ‘‘Mheshimiwa Rais Dkt. John Pombe Magufuli ametuelekeza viongozi wote wa ngazi za chini tuhakikishe tunashughulika,tunahangaika na shida za watu’’ .

Katika hatua nyingine Mhe. Mnyeti amewahakikishia wananchi hao kuwa maagizo yote aliyoyatoa katika mkutano huo yatasimamiwa na yatatekelezwa.Akisisitiza kuhusu hilo Mhe. Mnyeti anasema ‘‘ Mimi niwatoe wasiwasi wananchi , na niwahakikishie kwamba Awamu hii viongozi wote lazima wafanye kazi zao.Na kila mtu lazima ahakikishe  amekaa kwenye mstari wa kazi yake.Akishindwa kutimiza wajibu wake, ni bora akapumzika ,akatafutwa mtu mwingine ambaye anaweza akafanya  kazi kwa ajili ya watu’’.Mhe. Mnyeti pia amesema kwamba wananchi ndio waajiri wa viongozi, na ndio waliowaweka madarakani  hivyo wana wajibu  na wanapaswa kusema kile ambacho wanadhani  viongozi wao wanaweza wakakifanya.Na  viongozi wasiofanya yale wananchi wanayoyataka, hao  sio viongozi wanaofaa . Aidha Mhe. Mnyeti amesema kwamba yeye kwa niaba ya Mhe. Rais atahakikisha anafuatilia shida za wananchi na zinatafutiwa majibu katika muda muafaka.

Katika mkutano huo kero zilizojitokeza ni kutotekelezwa kwa baadhi ya  ahadi za viongozi wanaofika katika kata hiyo, mwananchi kulalamika shamba  lake kugeuzwa njia ya n’gombe (Palio), wafugaji kulishia mifugo katika mashamba ya wakulima  na mkulima kupigwa na kuporwa pesa zake na  vijana wa kifugaji na baadae kufunguliwa  mashtaka. Ambapo Mheshimiwa Mnyeti ameahidi kuzipatia ufumbuzi kero hizo ndani ya muda mfupi, na ametoa maelekezo kwa viongozi wa chini kuhusu  namna ya kutatua kero hizo.


                                                                                                                        ......... MWISHO.........

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa