• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAAJIRIWA WAPYA KITETO WAPATIWA MAFUNZO ELEKEZI, WAASWA KUZINGATIA MAADILI NA KUEPUKA RUSHWA.

Imetumwa : September 17th, 2025

Septemba 16, 2025, Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ilifanya  semina elekezi kwa watumishi wa ajira mpya wa wilayani hapa, yenye lengo la kuwajengea uelewa kuhusu wajibu wao, maadili ya kazi na namna bora ya kutekeleza majukumu yao kwa manufaa ya taifa na jamii kwa ujumla.


Katika semina hiyo, mada mbalimbali ziliwasilishwa kutoka taasisi na idara tofauti za serikali. Afisa kutoka Idara ya Uhamiaji Konstebo Anthony Mapunda aliwapatia elimu ya namna ya kuwatambua wasio raia wa Tanzania na kuwatahadharisha kutokutoa barua za utambulisho  kwa watu wasiowajua kwa lengo la kuzuia udanganyifu na upatikanaji holela wa hati za kusafiria.


Aidha, Afisa kutoka Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Bi. Mwanaisha Juma alitoa somo kuhusu madhara ya rushwa, ambapo watumishi hao walipewa onyo dhidi ya kujihusisha na vitendo vya ubadhirifu.

Vilevile, Afisa kutoka Shirika la Hifadhi ya Jamii (PSSSF) Ndugu. Harrison Werema aliwasilisha elimu kuhusu mafao mbalimbali ambayo wanachama wake hunufaika nayo, ikiwemo mafao ya uzeeni, matibabu, pamoja na mafao mengine ya kijamii.

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Utawala na Rasilimali Watu wa Halmashauri, Ndg. Rose Massay aliwafundisha watumishi hao kuhusu stahiki zao kisheria pamoja na wajibu wao wa kila siku katika utumishi wa umma.


Mbali na elimu hizo, mada kuhusu maadili ya utumishi wa umma pia ilitolewa, ambapo watumishi wapya walihimizwa kuzingatia maadili na kuishi kama kioo cha jamii hata wanapokuwa nje ya maeneo ya kazi. Vilevile watumishi hao wapya walipewa elimu juu ya matumizi ya mfumo wa utendaji kazi (PEPMIS).


Akifungua rasmi semina hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mhe. Remidius Mwema, aliwasihi watumishi hao kuwa mfano wa kuigwa kwa wananchi na kuhakikisha wanastawi na kustahimili mazingira yoyote waliyopangiwa kwa uadilifu na moyo wa kujitolea.

Nae, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto CPA. Hawa Abdul Hassan, alifunga semina hiyo kwa kuwataka watumishi hao wapya kutumia mafunzo waliyoyapata kama dira ya kazi.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAAJIRIWA WAPYA KITETO WAPATIWA MAFUNZO ELEKEZI, WAASWA KUZINGATIA MAADILI NA KUEPUKA RUSHWA.

    September 17, 2025
  • WAAJIRIWA WAPYA WAASWA KULINDA AFYA ZAO.

    September 16, 2025
  • "Stawi Ulipopandwa na Ulete Mabadiliko”, DC Mwema.

    September 16, 2025
  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa