• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WACHIMBAJI WA MADINI ILNDOROKON WALIA NA GHARAMA ZA MAJI MGODINI HAPO

Imetumwa : May 8th, 2024


Wachimbaji wa machimbo ya madini ya dhahabu katika machimbo ya Ilndorokon yaliyopo kata ya Njoro wameomba kuchimbiwa kisima ili kuwawezesha kupata maji kwa bei nafuu.

Akiongea Mei 6, 2024 mbele ya Mkuu wa Wilaya ya Kiteto Mh. Remidius Mwema, mmoja wa wachimbaji hao Ndg Thomas Masuke alisema kwamba dhahabu inahitaji maji mengi na  kwa sasa wachimbaji hao wanaingia gharama kubwa kwani wananunua lita 20 za maji kwa gharama ya TZS 1,500.

Kutokana na kero hiyo Masuke aliomba wachimbiwe kisima katika eneo hilo ili waweze kupata maji kwa gharama nafuu.

Mbali na kero ya maji wachimbaji hao pia walilalamika kuhusu ubovu wa barabara inayoelekea eneo hilo la uchimbaji na hivyo kumuomba Mh. Mkuu wa Wilaya kuwasaidia pia kwenye eneo la barabara.

Aidha Mchimbaji Gullam Tambwe aliomba wachimbaji waruhusiwe kutumia vifaa vya kisasa “compressor” katika uchimbaji wa dhahabu katika machimbo hayo ili kuongeza tija tofauti na sasa ambapo wanalazimika kutumia vifaa duni.

“Mimi nimeleta compressor kutoka Dar es Salaam kwaajili ya uchimbaji ila baada ya kufika hapa imezuiwa tunaambiwa hatutakiwi kutumia hiyo mashine ila hatujui sababu. Ombi langu tunaomba turuhusiwe kutumia kompresa” aliongeza Gullam.

Mbali na hayo wachimbaji hao waliomba pia huduma za afya katika eneo hilo.

Kuhusiana na changamoto ambazo zinahusisha wachimbaji na muwekezaji wa eneo hilo, Mh. Mwema ameahidi kuitisha kikao kati yake na muwekezaji halisi wa eneno hilo na sio muwakilishi wake pamoja na wawakilishi wachache wa wachimbaji hao ili wakae pamoja na kutatua changamoto hizo.

“Najua nae angekuwepo hapa huenda ana yake kuhusu wachimbaji. Lazma kuwepo mazingira ambayo yatalinda haki za pande zote mbili yaani mwenye leseni ya uchimbaji na wachimbaji” ameongeza Mh. Mwema.

Kuhusiana na changamoto ya maji, Mh. Mwema amesema hiyo ni fursa kwa mtanzania yoyote ambaye anaweza kuchimba kisima katika eneo hilo anaweza fanya hivyo.

“Changamoto zenu nimezisikia nyingine siwezi kuzipatia ufumbuzi hapa, ninazichukua nikaongee na timu yangu nitarudi tena kwa mrejesho” aliongeza Mh. Mwema.

Machimbo ya Ilndorokon yalianza rasmi April 15,2024 na mpaka sasa eneo hilo lina watu wapatao 320.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa