• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wafanya Biashara wa Mafuta ya Alizeti Wilayani Kiteto Wahimizwa Kudumisha Ubora wa Mafuta ya Kula Wanayozalisha ili Kukidhi Soko la Ndani na Kimataifa.

Imetumwa : September 4th, 2019

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bw. Emanuel Mwagala (aliyesimama) Akifungua Kikao cha Kamati ya Lishe Katika Ukumbi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto.

Dkt. Mwanaidi Shaban Akitoa Salamu kwa Wajumbe wa Kamati Ikiwa ni Pamoja na Kumkaribisha Mwenyekiti wa Kikao Bw. E. Mwagala

Wajumbe mbalimabli katika kikao hicho

Bw. Pundugu Balabala akiwasilisha taarifa ya Idara ya Kilimo na Umwagiliaji  kwa niaba ya Afisa Kilimo na Umwagiliaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto.


Bw. Emanuel Masha akiwasilisha taarifa ya Idara ya Mifugo na Uvuvi  kwa niaba ya Afisa  Mifugo na Uvuvi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto.

Bi. Fatuma Kawia Mratibu wa Huduma za Afya ya Uzazi na Mtoto Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto akiwasilisha taarifa.


Bi. Amina Mwesa akiwasilisha tarifa ya Idara ya Maji (kwa sasa RUWASA wakala wa Maji Mjini na Vijijini)  kwa niaba ya Meneja wa RUWASA Wilayani Kiteto.

Bw. Rodrick Kidenya Kaimu Afisa Maendeleo ya Jamii wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto akiwasilisha taarifa.

Bw. Mohamed Ismail mwakilishi wa Wamiliki wa Mashine za Kukamua Alizeti Wilayani Kiteto akiwasilisha taarifa.

Bw. Fabian Simon akiwasilisha tarifa ya Idara ya Elimu Sekondari kwa niaba ya Afisa  Elimu Sekondari wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto


Bw. Seif Lipyoga akiwasilisha taarifa ya Idara ya Afya Kiteto cha Madawa niaba ya Mfamasia wa  Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

Bw. Godwin Nagolo  akiwasilisha taarifa ya Asasi Isiyoya Kiserikali (NGO) ya Mwanasatu Development Organization (MWADO) Wilayani Kiteto.

Bw. James Paul  akiwasilisha taarifa ya Idara ya Mipango kwa niaba ya Afisa Mipango wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto


Bw. Kerevatus Sibanganya  akiwasilisha taarifa ya Idara ya Usafi na Mazingira kwa niaba ya Afisa Usafi na Mazingira wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto.

Mwakilishi wa BAKWATA Wilayani Kiteto Bw. Ibrahim Bori akichangia mada.

Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bi. Beatrice Lutanjuka akichangia mada kwenye kikao hicho.



-------------------------------------- HABARI KAMILI -----------------------------------------

Haya yamejiri katika kikao cha Kamati ya Lishe Wilayani Kiteto Julai 2019 ambapo Idara, Vitengo na Wadau wengine wa afya ya lishe kama zilivyotajwa hapo juu kwenye mawasilisho walijadili.  Ili kuwa na lishe bora, kiwango cha ubora wa mafuta ni muhimu sana kwa afya ya binadamu lakini pia mfanyabiashara husika atakua kiuchumi kwani atakuwa amejipatia fursa ya kutosha kwa kupata soko la uhakika ndani na nje ya nchi.


Wakizungumza kwa nyakati tofauti ni kwamba,  ukamuaji wa alizeti unafanywa na wafanyabiashara wenye weledi wanaofuata sheria, taratibu na kanuni za Wakala wa Chakula na Dawa nchini (TFDA) pamoja na Shirika la Viwango nchini (TBS) kiasi kwamba wanahakikisha wanakamua alizeti inayoonekana ni nzuri na salama kwani wakamuaji alizeti wanajua kuzitofautisha kuwa zipi ni mbaya na zipi ni nzuri.  


Chanzo cha mafuta kuwa mabaya hasa yale machungu hakijajulikana kisayansi kwamba nini hasa kinasababisha haya, lakini kwa uzoefu wa wanaoshugulika na ukamuaji wa alizeti wamesema wamefuatilia kwa kina waligundua sababu kuu mbili; ya kwanza ni kwamba huwa tatizo linaanzia shambani kutokana na alizeti kuvunwa bila kukauka kwa kiwango kinachotakiwa hivyo zikihifadhiwa punje za alizeti husika huvunda na zikikamuliwa mafuta hayo huwa machungu ambapo hizi alizeti ukiziona unazitambua na ukitafuna punje zake ni chungu pia, na la pili  ni mafuta ya alizeti yanayopatikana baada ya kuchemsha mabaki ya alizeti yaliyokwisha kukamuliwa viwandani maarufu kama tope.


Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto kupitia Kamati ya Lishe na Kamati ya TFDA ngazi ya Wilaya imesisitiza wamiliki wa mashine hizi za kukamua alizeti bora na atakayeonekana kukiuka agizo hili atachukuliwa hatua kali za kisheria, lakini pia akionekana mtu anazo alizeti za aina hiyo basi itolewe taarifa haraka Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto ili hatua za kisheria ziweze kuchukua mkondo wake kwani kuna madhara yanayoweza kutokea kwa walaji aidha moja kwa moja au kuathiri afya za binadamu taratibu. Kamati za ukaguzi wa mashine hizi za kukamua alizeti zinafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha mwananchi anakuwa salama na wadau wote wanaohusika wanafuata miongozo ya TFDA na TBS ipasavyo.


Matokeo chanya ya jambo hili kufanywa hivyo kutakuwa kunaisaidia jamii kupata lishe bora kwa  kutumia mafuta bora, na wao kama wafanyabiashara watakuwa katika nafasi nzuri ya kibiashara kwa mafuta husika kuuzwa si tu ndani ya nchi lakini na kimataifa pia,  jambo ambalo litakuwa limeongeza wigo wa soko la mafuta yao matokeo yake ni kupata fedha nyingi za kigeni ambazo ni zitaongeza mtaji wa mfanyabiashara mwenyewe, serikali kuongeza makusanyo mbalimbali yanayotokana na uzalishaji huu kupitia kodi, manunuzi ya umeme, maji na vifungashio. Pia kutaongeza mnyororo wa ajira katika sekta ya kubwa ya kilimo bila kusahau usafirishaji na kuongezeka kwa ubunifu wa teknolojia tatuzi ya uzalishaji itakayotokana na mahitaji mvuto "demand driven" ya ushindani wa kimataifa.


Akizungumza wakati wa majadiliano, Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Bi. Beatrice Lutanjuka amesema  Sumukuvu bado ni changamoto, jamii bado haina uelewa wa kutosha  katika kuhifadhi mazao yao hususani nafaka kama mahindi, karanga na mtama ili mazao hayo yasiweze kupata sumukuvu, jambo ambalo ni hatari sana kwani madhara ya sumukuvu ni makubwa. Sumukuvu inapoingia mwilini kidogo kidogo, madhara yake  hayawezi kuonekana kwa mara moja, lakini  moja wapo ya madhara yanayoweza kuonekana baada ya muda mrefu ni  saratani ya ini.


Wataamu wa Mifumo na Uvuvi wamefafanua zaidi kuhusu sumukuvu, kwamba Sumukuvu haiko kwenye nafaka peke yake, bali inaweza kuwepo hata kwenye nyama, pamoja na mazao ya mifugo kama vile maziwa, kutokana na mifugo kula vyakula ambavyo vina sumukuvu, hivyo jamii inapaswa pia kutahadharishwa kwamba mifugo inapokula mabua au pumba ambazo zina sumukuvu, nyama  pamoja na mazao yake yote ambayo hutumika kama chakula kwa binadamu vyote vinaweza kuwa na viambata vya sumu hiyo.


Nawasilisha.







Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa