• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAFUGAJI WA MBWA NA PAKA WAHAMASISHWA KUSHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA KICHAA CHA MBWA DUNIANI

Imetumwa : September 24th, 2025

Wafugaji wa mbwa wilayani Kiteto wamehimizwa kujitokeza kwa wingi kuwaleta mbwa na paka wao ili kupata chanjo dhidi ya kichaa cha mbwa katika maadhimisho ya Siku ya Kichaa cha Mbwa Duniani ambayo Kitaifa yanayotarajiwa kufanyika wilayani Kiteto Septemba 26-29, 2025.


Daktari wa Mifugo wa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto Dkt. Lunonu Sigalla amesema maandalizi ya maadhimisho hayo yanaendelea vizuri, na Kiteto inatarajiwa kupokea  wataalamu wa mifugo zaidi ya 100 kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi, Wizara ya Afya,  Shirika la Kilimo na chakula (FAO) na Chuo Kikuu cha Kilimo cha Sokoine (SUA). Pia watakuwepo wataalumu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu, Halmashauri na Mikoa mbalimbali pamoja na wadau  kutoka sekta binafsi kwaajili ya maadhimisho hayo.


“Kwa siku tatu, kila asubuhi timu zetu za wataalamu zitatawanyika katika maeneo mbalimbali ya wilaya hii kutoa huduma za chanjo na elimu. Hii ni nafasi muhimu kwa wafugaji wote kuhakikisha mbwa na paka wao wanapata chanjo na huduma nyingine zitakazotolewa bila gharama yoyote”, amesema Dkt. Sigalla.


Mbali na chanjo, huduma nyingine zitakazotolewa bure ni pamoja na kuhasi mbwa na paka dume na kutoa kizazi kwa mbwa na paka jike. Aidha, kutatolewa elimu kwa wanafunzi wa shule za msingi na sekondari kuhusu utaratibu wa chanjo za kichaa cha mbwa, namna ya kujikinga na maambukizi ya kichaa cha mbwa na hatua za haraka za kuchukua iwapo mtu atang’atwa na mbwa.


Dkt. Sigalla ameongeza kuwa chanjo ni kinga madhubuti na nafuu zaidi ikilinganishwa na gharama kubwa za matibabu ya binadamu anaposhambuliwa na mbwa mwenye kichaa.


“Kiteto kuwa wenyeji wa maadhimisho haya Kitaifa ni fursa ya kipekee sana, hivyo tunatoa wito kwa wafugaji wote wajitokeze na kuwaleta mbwa pamoja na paka wao katika maeneo yatakayotangazwa. Hii ni nafasi ya kulinda wanyama na familia zetu dhidi ya madhara makubwa ya ugonjwa wa kichaa cha mbwa”, amesisitiza Dkt. Sigalla.


Maadhimisho haya yanatarajiwa kuwa fursa ya pekee kwa jamii ya Kiteto sio tu kupata huduma hizo bure bali pia kuongeza uelewa juu ya afya ya wanyama ili kujenga jamii salama.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA MAPOKEZI YA FEDHA SEPTEMBA 2025 September 16, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • WAZEE WAHIMIZWA KUJITOKEZA KWA WINGI KUPIGA KURA OKTOBA 29

    October 07, 2025
  • KATIBU MKUU WIZARA YA MIFUGO NA UVUVI AKABIDHI VIFAA NA CHANJO YA KICHAA CHA MBWA KITETO

    September 29, 2025
  • WITO WA LEO SEPTEMBA 29,2025

    September 29, 2025
  • TANZANIA YA TATU AFRIKA MPANGO RASMI WA KUDHIBITI KICHAA CHA MBWA

    September 29, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa