• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Wakazi wa Kiteto Waaswa Kutojihusisha na Vitendo vya Uvunjaji wa Sheria

Imetumwa : October 8th, 2018

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akizungumza na wakazi wa kata za Kibaya, Kaloleni na Bwagamoyo ,katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Kibaya mwishoni mwa wiki.

Diwani wa kata ya Kibaya Mhe. Kasim Msonde akifungua mkutano .

Kaimu  Mkurugenzi mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto akizungumza katika mkutano huo.

Wakuu wa idara mbalimbali za halmashauri ya wilaya ya Kiteto wakipunga mkono kama ishara ya kuwasalimia wananchi katika  mkutano huo.

Afisa Ardhi (W) ya Kiteto  Ndg. Damas Gulisha akitoa maelekezo kuhusiana na taratibu zinazotakiwa kufuatwa ili mwananchi aweze kumiliki ardhi.

Mkuu wa Kituo kituo kikuu cha polisi  Kibaya Patric Kimaro akitoa ufafanuzi kuhusiana na kero iliyowasilishwa na mmoja wa wakazi wa kibaya waliohudhuria mkutano huo.

Wananchi wakiwa wamekusanyika katika mkutano huo kumsikiliza Mkuu wao wa wilaya.

Wananchi wakiwasilisha kero zao wakati wa mkutano huo.



.....HABARI KAMILI......



Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mheshimiwa Tumaini  Magesa amewataka wakazi wa Kiteto kutojihusisha na vitendo vya uvunjifu wa sheria  kwani kwa kufanya hivyo serikali itawachukulia hatua kali.Mhe. Magesa ametoa angalizo hilo katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika mji mdogo wa Kibaya, wilayani Kiteto mwishoni mwa wiki.

Akizungumza wakati akihutubia mkutano huo Mhe. Magessa amesema kwamba Kuna ujangili unaendeshwa Kibaya, ambapo watu wanakwenda  maeneo ya Makame ,wanawinda digidigi ,wanawaleta Kibaya wanatumika kama kitoweo, na watu wengine wameonekana wakiuza mishikaki ambayo inasadikika kwamba ni ya digidigi. Mhe Magessa amewaonya watu wanaojihusisha na uuzaji wa nyama ya digidigi ,ikiwemo mishikaki , kwamba waache mara moja tabia hiyo,kwani serikali itaendesha operesheni maalumu kwa ajili ya kukabiliana na vitendo hivyo vya ujangili. Akisisitiza kuhusu angalizo hilo Mhe Magessa amesema “kazi inaanza leo,ukikamatwa utaingia kwenye mikono ya sheria kwa sababu unafanya ujangili.Ninajua kabisa kwamba kuna watu siku nyingi hawaendi kwenye mabucha ,wanakula nyama pori ambazo zinawindwa kinyume cha sheria, tutawakamata, na tutawapelekeka kwenye vyombo vya sheria, watashughulikiwa ipasavyo”.

Sambamba na suala  la ujangili Mhe. Magessa  ameonya kuhusu uchimbaji madini usiofuata sheria. Hapa Mhe. Magessa anasema “Kuna ndugu zetu hapa hapa Kibaya, wamekuwa wakiondoka wanatafuta madini kila mahali, kwa hiyo kila mahali sasa, watu wanavizia wanalipua  baruti wanatafuta madini.Hili nalo  liwe na utaratibu, ziko leseni kama unataka kuchimba madini,ambazo unatakiwa uwe nazo ili uweze kufanya hizo shughuli za uchimbaji madini.Sio kila mahali watu wanapiga baruti tu .Kuna watu wanabaruti humu,na kazi yake ni hiyo,wanakwenda wakilipua katika maeneo  mbalimbali kwa lengo la kutafuta madini , na wanapopiga baruti wanyama  waliopo katika maeneo hayo wanakimbia. Sasa hili tuelezane tu kama wananchi, tusije tukaingia katika mtego ambao mtu unavuja sheria ya nchi,na baadae ukikamatwa inaonekana kama unaonewa’’.


Kadhalika Mhe .Magessa amezungumzia suala la elimu ambapo amesema  kwamba  kila mzazi ama mlezi mwenye  mtoto ambaye amefikia umri wa kwenda shule ,kuhakikisha kwamba mtoto huyo anaandikishwa kwa ajili ya kuanza  shule, na kwamba ni lazima kufanya hivyo, na mzazi au mlezi ambaye hatampeleka mtoto wake shule atakamatwa na kushtakiwa kwa kutompekeka mtoto shule. Mhe Magessa amewasisitiza wakazi wa Kiteto kulipa kipaumbele suala la elimu kwa ajili ya manufaa ya baadae ya watoto wao, wao wenyewe wazazi, jamii na Taifa kwa ujumla.
 Mhe. Magessa pia amezungumzia suala la chaneli za televisheni ambazo zilikuwa zikionekana katika visimbuzi vya DSTV, ZUKU na AZAM ambazo kwa sasa hazionekani katika visimbuzi hivyo.Mhe. Magessa ametoa ufafanuzi kuhusiana na suala hilo ambapo amesema kwamba  urushaji wa chaneli za televisheni unafanyika kulingana na leseni ambazo kampuni zinazohusika na urushaji wa chaneli za televisheni kwa mfumo wa kidigitali zinakuwa zimepewa na tume ya mawasiliano. Na kwamba ziko  leseni za kurusha chanel bure, na zipo leseni za kurusha chaneli kwa kulipia tu. Hata hivyo kampuni hizo zimekuwa zikirusha  kwa kulipia ,chaneli  hizo ambazo kwa mujibu wa sheria za tume ya mawasiliano zinatakiwa zirushwe bila kulipia, kwamba kisimbuzi kinapokuwa  hakijalipiwa,au muda uliolipiwa umeisha, chaneli zinazotakiwa kuonyeshwa bure, zimekuwa  hazionekani.

Mhe. Magessa ameendelea kusema kwamba tume ya mawasiliano ilikuwa na kesi ambayo ilikuwa imefunguliwa baina yake na wamiliki wa kampuni hizo ambazo zimekuwa zikikiuka utaratibu kwa kuonyesha chaneli za bure kwa kulipia, na baada ya kesi hiyo kumalizika,wakatakiwa kunyang’anywa leseni zao,na ili wasinyanganywe leseni hizo,wakaamua kuziondoa chaneli zote za bure. Mhe. Magessa amesema kwamba ni vema wananchi wakafahamu kwamba chaneli hizo hazitarudi hadi kampuni hizo zitakapokuwa na leseni zinazowaruhusu kuonyesha chaneli  za bure.

Aidha Mhe Magessa  pia ametoa ushauri kwa wakazi  wa Kiteto ambao wana visimbuzi hivyo ambavyo  chaneli za bure hazionekani , kwamba  waendelee kuvitumia kwa sababu vina maudhui ambayo wanayapenda, lakini pia wafanye utaratibu wa kupata visimbuzi vya Star Times, TING, Digtec na Continental ili waweze kuona chaneli za bure ambazo ndizo zinazoonyesha mambo mengi yenye maudhui ya ndani ya nchi, hususani habari, matukio  na kazi mbalimbali zinazofanywa na serikali yao.

Katika hatua nyingine Mhe. Magessa amezungumzia suala la migogoro ya ardhi ambapo amesema kwamba kumekuwa na mlundikano wa migogoro ya ardhi, migogoro hiyo imetokana na migongano katika umiliki wa ardhi. Mhe Magessa  amesema kwamba utaratibu wa namna gani mtua anatakiwa kupata ardhi ameusema zaidi ya mara moja,lakini inaonekana bado watu hawajaelewa ndio sababu migogoro inaendelea.Hapa akamtaka afisa ardhi wa wilaya ya Kiteto ndugu Damas Gulisha  kuwaeleza wananchi taratibu ambazo zinatakiwa kufuatwa iki kuweza kupata umiliki wa ardhi,ambapo ndugu Gulisha ametoa maelezo ya kina kuhusiana na taratibu hizo.

Ili kuhakikisha kwamba migogoro yote ya ardhi wilayani inafika idara ya ardhi, Mhe. Magessa amewaagiza wenyeviti wa vijiji wote kuorodhesha watu wenye matatizo ya ardhi wote na kuyapeleke idara ya ardhi,ambapo wataalamu wa ardhi  watafika kila mahali panaposemwa pana mgogoro ili kutatua migogoro hiyo.

Mhe. Magessa amesema kwamba migogoro mingi imekuwa haipatiwi ufumbuzi kutokana na kwamba watu wamekuwa wanakwenda mahali  ambako sio sahihi.Kwamba iko idara ya ardhi ambayo ina wataalamu wa kutosha kushughulika na masuala ya ardhi,kama mtu ana mgogoro wowote unaohusu ardhi, majibu yote atayapata idara ya ardhi.Na kama atakuwa hajaridhika afike ofisini kwake au ofisini kwa DAS ili migogoro hiyo iweze kutatuliwa na hatimaye wilaya iweze kuwa na amani na utulivu.Mhe. Magessa pia amesema kwamba ziko fomu ambazo wenyeviti wa vijiji/mitaa wanatakiwa wawe nazo, zinaitwa sema usikike,kwamba kama mtu ameshindwa kueleza maelezo yake kwa mkuu wa wilaya, anataka kuyaeleza kwa waziri, atajaza hiyo fomu, itatumwa kwenda kwa waziri,waziri akishaisoma atamjibu.Na kwamba wakifanya hivyo migogoro itakuwa inakwisha kwa usalama,badala ya vile ambavyo imekuwa ikiisha kwa magomvi.

Mhe. Magessa amefanya mkutano wa hadhara katika mji mdogo wa Kibaya,mkutano huo umehusisha kata tatu ambazo ni Kibaya,Kaloleni  na Bwagamoyo.Mkutano huo ni wa kawaida, ambao lengo lake ni Mkuu wa wilaya kutoa maelekezo ya serikali, kusikiliza kero za wananchi na kuzipatia ufumbuzi.




.......MWISHO.......

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa