• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WA MBAAZI WILAYANI KITETO WAPATA KICHEKO

Imetumwa : September 6th, 2023

WAKULIMA WA MBAAZI WILAYANI KITETO WAPATA KICHEKO

 

Wakulima wa zao la mbaazi wilayani Kiteto wamefurahishwa na mfumo mpya wa uuzaji  wa zao hilo kupitia mfumo wa stakabadhi ghalani baada ya zao hilo kununuliwa kwa bei ya shillingi 2261 kwa kilo moja  kupitia mnada wa kwanza.

Katika mnada huo ambao umeendeshwa  Septemba 5,2023 na Chama Kikuu cha Ushirika Arusha (ACU) katika kata ya Matui, jumla ya tani 250 za mbaazi zimenunuliwa.  Jumla ya makampuni sita yalijitokeza kuomba kununua mbaazi hizo hata hivyo kampuni ya SM Holding LTD ndio iliyoshinda katika mnada huo.

Mmoja ya wakulima ambao walipeleka mbaazi   ghalani kwaajili ya kuuzwa kwa mnada, Bwana Mohamedi Said Kidevu aliishukuru serikali  kwa kuleta mfumo huo maana hauna usumbufu na pia wameuza kwa bei nzuri ambayo hata wangeamua kusafirisha zao hilo wakauzie Dar es Salaam wasingeweza kuuza kwa bei hiyo.

Akiongea katika mnada huo, Meneja wa ACU Bwana Innocent Kisole alitoa rai kwa wakulima wote kujiunga katika vyama vya msingi.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Kiteto SSI Mbaraka Alhaj Batenga ambaye ndiye aliyekua mgeni rasmi katika mnada huo  alisema kwamba serikali haiwezi kuweka pesa kwenye mfuko wa kila mwananchi ila badala yake serikali inachokifanya ni kuweka mazingira mazuri ya watu kuinuka kiuchumi.

“Katika mazao changamoto ilikua ni kukosa soko ila Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan amekuja na mfumo huu kilimo sasa kimekuja kumkomboa mwananchi. Kila mtu asimame kwenye nafasi yake vizuri” aliongeza Mh  Batenga.

Pia Mh Batenga alitoa onyo  dhidi ya watu ambao watajaribu kuchezea ushirika  na ameagiza kwamba mbaazi zote zinazolimwa Kiteto ziuzwe kwenye mfumo wa stakabadhi ghalani.

Naye Mwenyekiti wa Halmashauri ya Kiteto Mh. Abdala Bundala alisema kwamba mfumo wa stakabadhi ghalani umekuja mkombozi wa wakulima  na pia umekuja kama mkombozi kwa Halmashauri kwa kukusanya mapato pasipo kukimbizana.

Katika mnada huo Kampuni ya SEDACO iliomba kununua kwa bei ya shilingi 2105 kwa kilo, HS LTD iliomba kununua kwa bei ya shilingi 1900 kwa kilo na Kampuni ya YURI iliomba kununua kwa bei ya shilingi 2050. Kampuni ya   Export Trading iliomba kununua kwa bei ya shilingi  2168 na kampuni ya Afrishan iliomba kununua kwa shilingi 2250.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa