• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WAKULIMA WAELIMISHWE UMUHIMU WA KUPIMA AFYA YA UDONGO

Imetumwa : February 18th, 2024

Mwenyekiti wa Kamati ya Huduma za Uchumi , Diwani Mussa Braiton,  ametoa rai kwa watumishi wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi,  kuwajulisha wananchi kuhusu uwepo wa huduma ya upimaji wa afya ya udongo.

Hayo ameyasema katika Kikao  Cha Robo ya Pili cha Kamati ya Huduma za Uchumi  kilichofanyika Februari 16, 2024 katika Ukumbi wa Halmashauri.

Diwani Braiton amesema kwamba serikali imeleta kifaa cha kupimia afya ya udongo na pia imewawezesha Maafisa Ugani   pikipiki ili kurahisha zoezi hilo,  hivyo wananchi wanapaswa wajue upatikanaji wa huduma hiyo.

“Wananchi wajulishwe na wapewe elimu kuhusu upimaji wa afya ya udongo” aliongeza Diwani Braiton.

Nae Mwenyekiti wa Halmashauri, Mh. Abdala Bundala, amesisitiza kwamba jambo la kupima afya ya udongo lichukuliwe kwa umuhimu mkubwa  ili kuweza kuongeza  uzalishaji haswa katika kipindi hiki ambacho  uzalishaji unashuka.

Huduma ya upimaji wa afya ya udongo hutolewa bure na ili mwananchi aweze kupimiwa afya ya udongo katika shamba lake, anapaswa kupeleka ombi lake kwa Afisa Ugani kisha Afisa huyo ataenda kwenye shamba la mkulima na kuchukua sampuli ya udongo na kwenda kuipima  katika maabara iliyopo katika Ofisi za Idara ya Kilimo Kiteto.

Baada ya majibu ya afya ya udongo kutoka, mkulima anashauriwa  aina sahihi ya mbolea ya kutumia ili kurutubisha ardhi ya shamba lake.

Toka Halmashauri ipokee kifaa cha kupimia udongo  Agosti 2023, jumla ya sampuli 312 za udongo kutoka katika vijiji  15 vilivyopo katika kata za Bwawani, Matui, Chapakazi, Ndirigishi, Olboroti, Njoro na Partimbo zimepimwa afya yake na ushauri stahiki wa matumizi ya ardhi hizo umetolewa kulingana na majibu ya afya ya udongo katika vijiji husika.

                                                                                   

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa