• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Walengwa wa TASAF Wilayani Kiteto Wakiri Kuboreshewa Maisha na Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini ( PSSN)

Imetumwa : December 11th, 2017


Walengwa wa TASAF katika vijiji vya Dongo na Olgila  wilayani Kiteto wakiwa katika zoezi la uhawilishaji fedha na uhakiki wa watoto wanaopaswa kuwepo kwenye huduma za afya na elimu zinazotolewa na TASAF  kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN) 

Walengwa wa TASAF katika vijiji vya Dongo na Olgila wilayani Kiteto wakipokea  fedha ya ruzuku inayotolewa na TASAF  kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN) 

Mlengwa wa TASAF  katika kijiji cha Dongo wilayani Kiteto  Rahel Wiliam Christopher aliyefanikiwa kuboresha  maisha yake kutokana na  ruzuku inayotolewa na TASAF  kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN).

   Nguruwe wa mlengwa wa TASAF  katika kijiji  cha Dongo Wilayani Kiteto Rahel Wiliam Christopher. Nguruwe hawa  wamenunulia kwa fedha ya  ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN)   


Nyumba ya Mlengwa wa TASAF  katika kijiji cha Dongo wilayani Kiteto  Rahel Wiliam Christopher.Nyumba hii imejengwa kwa fedha ya ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN)



Mlengwa wa TASAF katika kijiji cha Olgila wilayani Kiteto Katarina Elias aliyefanikiwa kuboresha maisha yake kutokana na fedha ya  ruzuku inayotolewa na TASAF  kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN).


                                                Mbuzi wa mlengwa wa TASAF katika kijiji cha Olgila Wilayani Kiteto  Katarina Elias. Mbuzi hawa wamenunuliwa kwa fedha ya  ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa  Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN)                                                            

Nyumba aliyokuwa akiishi mlengwa wa TASAF katika kijiji cha Olgila wilayani Kiteto  Katarina Elias kabla  ya kuanza kupata ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN)

Nyumba ya Mlengwa wa TASAF katika kijiji cha Olgila wilayani Kiteto Katarina Elias.Nyumba hii imejengwa kwa fedha ya ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN)

Mlengwa wa TASAF  katika kijiji cha Olgila wilayani Kiteto Penina Kilongola Magoha aliyefanikiwa kuboresha makazi yake kutokana na fedha ya ruzuku inayotolewa na TASAF  kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN) 

Nyumba ya Mlengwa wa TASAF katika kijiji cha Olgila wilayani Kiteto Penina  Kilongola  Magoha.Nyumba hii imejengwa kwa fedha ya ruzuku inayotolewa na TASAF kupitia Mpango wa kunusuru Kaya Maskini  (PSSN)


Mlengwa wa TASAF  katika kijiji cha Olgila wilayani Kiteto Esta Bilishani Mkali aliyefanikiwa kuboresha maisha yake kutokana na  ruzuku inayotolewa na TASAF  kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN).

                                                               

                                                                          HABARI KAMILI....


WALENGWA WA TASAF WILAYANI KITETO WAKIRI KUBORESHEWA MAISHA NA MPANGO WA KUNUSURU KAYA MASKINI (PSSN)

Walengwa wa TASAF wilayani Kiteto wamesema kwamba Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini (PSSN) umewaboreshea maisha .Walengwa hao wameyasema hayo wakati wa zoezi la uhawilishaji fedha awamu ya tatu, dirisha la malipo la mwezi Novemba - Decemba  na uhakiki wa watoto wanaopaswa kuwepo kwenye huduma za afya na elimu .

Akizungumza baada ya kupokea fedha za ruzuku, mlengwa wa TASAF katika kijiji cha Dongo Rahel Wiliam Christopher amesema kwamba PSSN imeboresha maisha yake, kwani kwa kutumia fedha za TASAF ameweza kununua Nguruwe na kuku ambao anawafuga, anapowauza anapata fedha ,ambazo anazitumia kukidhi mahitaji ya lazima ya familia yake. Pia ameweza kujenga nyumba ya vyumba viwili ambayo iko kwenye lenta. Rahel anasema‘‘tangu nimeanza kupokea hela za TASAF sihangaiki sana.kama nimeishiwa sabuni naweza nikachukua kuku wangu mmoja nikauza , pia kupitia hela hiyo hiyo ya TASAF  napata mahitaji ya watoto kama sare za shule na madaftari .

Mlengwa wa TASAF Esta Bilishani Mkali amesema kwamba PSSN imeboresha maisha yake,kwani kabla hajaingia kwenye PSSN hakuwa na chochote , Esta anasema ‘‘TASAF imeboresha familia yangu , kwa kutumia fedha za TASAF nimeweza kununua mbuzi watatu,kuku nane ,pia imenisaidia kupata matibabu ya mtoto. Mtoto wangu alikuwa anasumbuliwa sana na macho, lakini sikuwa na fedha ya kumpeleka hospitali, baada ya kuanza kupokea fedha za TASAF, niliweza kukusanya kidogo kidogo hadi nikafanikiwa kumpeleka mtoto wangu hospitali Morogoro kupata matibabu’’. Aidha  Esta amesema kwamba lengo lake ni   kununua ng’ombe wa maziwa, hivyo mbuzi alionao watakapo ongezeka atawauza , pia fedha  anayopewa na TASAF  atakuwa akiweka kidogo kidogo  ili aweze kutimiza lengo hilo.

Vilevile mlengwa wa TASAF Katarina Elias amesema kwamba PSSN imeboresha maisha yake .Katarina anasema ‘‘ Nilikuwa nateseka sana, kwenye miraba kila siku kulima vibarua ili niweze kuishi, lakini TASAF imenisaidia, kabla sijaingia kwenye mpango wa TASAF nilikuwa naishi kwenye nyumba ya nyasi, nimeweza kujenga nyumba nyingine ambapo kwa kutumia hela ya TASAF nilinunua bati saba nikapaua nyumba yangu , nimenunua mbuzi nane, na ninapata fedha ya kujikimu kwa mahitaji yangu madogo madogo ya nyumbani’’.

Kadhalika mlengwa mwingine wa TASAF Penina Kilongola Magoha amesema kwamba PSSN imeboresha maisha yake kwani kwa kutumia fedha za TASAF ameweza kupaua nyumba yake kwa bati, na pia inamsaidia kupata mahitaji yake madogo madogo ya kila siku,tofauti na wakati kabla hajaingia kwenye PSSN ambapo hali yake ya maisha ilikuwa ngumu na alikuwa na makazi duni.

Katika hatua nyingine Afisa ufuatiliaji  wa TASAF wilaya ya Kiteto ndugu Kishari Shegela amewataka walengwa wa TASAF katika kijiji cha Olgila  kuhakikisha kwamba wanakamilisha michango yao ya Bima ya afya (ICHF) mara tu wanapopokea ruzuku zao ili kupata kadi za bima ya afya ambazo zitawawezesha kupata matibabu pindi watakapougua.Shegela anasema ‘‘bima ya afya itakusaidia, ukilazwa hospitali hata  siku saba tu,unaweza kutumia pesa zaidi ya shilingi 50,000, lakini bima ya afya unailipia shilingi 30,000 tu na unatibiwa wewe, mwenzi wako na watoto wako kwa mwaka mzima.

 Aidha ndugu Shegela amewataka walengwa wa TASAF kuzitumia vizuri  fedha wanazopewa na TASAF. Akisisitiza  kuhusu matumizi bora ya fedha hizo  Shegela anasema ‘‘Jamani hizi fedha sio za kula tu, tafuta kitu uwekeze,tafuta kabiashara,sio kila fedha unayopata  unakula tu , jiunge kwenye kikundi, peleka kidogo kwenye VICOBA, cheza hata kamchezo katakusaidia kupata sare za shule na mahitaji mengine ya familia’’Shegela anaendelea kusema kwamba walengwa wa TASAF  waandikishe kwenye mpango watoto  wote walio katika kaya zao ambao wanasoma shule na wale ambao wanahudhuria kliniki, na wahakikishe kwamba watoto wanaotakiwa kuhudhuria kliniki wanapelekwa kliniki kwani kutowaandikisha, na kutowapeleka kliniki  kunasababisha kutokupata ruzuku zao.Pia amewataka walengwa hao kununua mahitaji muhimu ya watoto wao,kama, sare za shule, masweta na viatu vya shule, kwani ,katika ruzuku wanazopewa , kuna ruzuku ya elimu ambayo walengwa ni hao watoto, hivyo  wazazi ama walezi wanapopokea fedha hizo wafahamu kwamba  wanapaswa kuwanunulia watoto wao mahitaji yao ya shule na si kwamba wazitumie zote.

Katika wilaya ya Kiteto,  TASAF kupitia Mpango wa Kunusuru Kaya Maskini  (PSSN) ina walengwa 5739, ambapo idadi hiyo inajumuisha walengwa wanaopatiwa ruzuku ya msingi  na ruzuku ya masharti ambayo hutolewa kwa walengwa wenye  watoto wanaohudhuria kliniki na watoto wanaosoma elimu ya msingi na sekondari kidato cha kwanza hadi kidato cha sita.

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • JAMII YAASWA KUZINGATIA HAKI ZA WATOTO.

    June 16, 2025
  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa