Kiswahili
  • English
  • Kiswahili
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WALEZI KITETO WAHIMIZWA KUPAMBANA NA UKATILI WA KIJINSIA

Imetumwa : August 31st, 2023

Walezi na wamiliki wa vituo vya kulea watoto wadogo mchana (Daycare Centres) wilayani Kiteto wamehimizwa kua mstari wa mbele katika kupambana na ukatili wa kijinsia wilayani hapo.

Rai hiyo imetolewa Agosti 30, 2023 na Mgeni Rasmi , Dr. Vicent Gyunda alipokua akifunga mafunzo ya siku kumi kwa walezi na wamiliki wa vituo hivyo wilayani hapo.


Dr. Gyunda ambaye pia ni Mganga Mkuu wa Wilaya, alisema kwamba katika mafunzo hayo washiriki walifundishwa namna ya kupambana na ukatili wa kijinsia na jinsi ya kuwatambua waathirika wa matukio hayo, hivyo baada ya mafunzo hayo Halmashauri inaamini sasa inaenda kujenga jamii nzuri maana wahitimu hao wanaenda kua mabalozi katika kutoa elimu na kupambana na ukatili.


Mbali na hayo Dr Gyunda alisema kwamba baada ya mafunzo hayo wanategemea kuona malezi katika vituo vyao yanafuata misingi yote kama ambavyo wameelekezwa katika mafunzo hayo . Pia alisema kwamba anaamini kuwa wahitimu hao watakua mabalozi wa kuelimisha kuhusu umuhimu wa lishe shuleni.


“Tunaamini kwamba sasa mtahakikisha malezi kwenye vituo vyenu hayaingii doa ila pia tunategemea mtakua walinzi kwa kukemea pale ambapo mtaona mambo hayaendi sawa kwenye vituo ” aliongeza Dr. Gyunda.

Licha ya hayo, DR. Gyunda alisema kwamba wahitimu hao sasa wamebaki na kazi kubwa ya kusajiri vituo vyao kutokana na misingi na vigezo walivyofundishwa.

Katika risala ya wahitimu wa mafunzo hayo ambayo ilisomwa na Bw Enerick Mwambene, wahitimu hao waliushukuru uongozi wa Halmashauri kupitia Ustawi wa Jamii Wilaya kwa kua viungo muhimu katika kufanikisha mafunzo hayo.


Mbali na hilo wahitimu hao walieleza moja ya changamoto katika vituo vyao ni ukosefu wa miongozo ya kutumia katika vituo vya kulelea watoto wadogo mchana na hivyo kulazimika kutumia muongozo wa elimu ya awali. Katika kujibu hoja hiyo Mgeni rasmi alisema kwamba suala hilo wamelipokea na watalifanyia kazi.


Mafunzo hayo ambayo yameratibiwa na Ofisi ya ya Rais TAMISEMI pamoja na Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wanawake na Makundi Maalumu; wilayani Kiteto yalihudhuliwa na washiriki 85 na yaliongozwa na Mkufunzi wa Kitaifa Bi Restituta Bujiku.


Nae Afisa Ustawi wa Wilaya Bi Jackline Barongo alisema kwamba lengo la mafunzo hayo ni kupunguza changamoto ya walezi wasio na sifa ya kulea na kufundisha watoto chini ya miaka mitano waliopo katika vituo vya kulea watoto wadogo mchana.


Nchini Tanzania, huduma ya vituo vya kulea watoto wadogo mchana inatolewa kwa mujibu wa Sheria ya Watoto namba 21 ya mwaka 2009 ikiwa na lengo la kuwapatia watotot wadogo wenye umri chini ya miaka mitano malezi changamshi.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO KWAAJILI YA MAANDALIZI YA ZOEZI LA UBORESHWAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KURA AWAMU YA PILI

    May 14, 2025
  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa