• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kiteto Watakiwa Kudumisha Amani

Imetumwa : July 8th, 2018

Mbunge  wa Kiteto  Mhe. Emmanuel Papian akizungumza na wakazi wa kijiji cha Kimana katika mkutano wa hadhara uliofanyika  kijijini Kimana mwishoni mwa wiki.


Mwenyekiti wa Kijiji cha Kimana akifungua Mkutano wa Mbunge wa Kiteto Mhe. Emanuel Papian kuzungumza na wananchi katika  kijiji cha Kimana.

Wakazi wa kijiji cha Kimana  ,kata ya Partimbo, wilaya ya Kiteto wakiwa wamekusanyika kumsikiliza Mbunge  wao Mhe. Emmanuel Papian katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.

Wakazi wa kijiji cha Kimana wakiwasilisha kero zao kwa Mbunge wa Kiteto Mhe. Emmanuel Papian katika mkutano wa hadhara uliofanyika kijijini hapo.



.....HABARI KAMILI........




Mbunge wa Kiteto Mheshimiwa Emmanuel Papian amewataka wakazi wa Kiteto kudumisha amani  kwa kuheshimu  mipango ya matumizi  bora ya ardhi waliyojipangia katika vijiji vyao . Mhe. Papian ameyasema hayo katika mkutano wa hadhara kijijini Kimana mwishoni mwa wiki.

Akizungumza katika mkutano wa hadhara kijijini Kimana, Mheshimwa Papian amesema  “  Kwa sasa hatutarajii kusikia migogoro ya wakulima na wafugaji, maana wakulima wako sehemu yao, na wafugaji wako sehemu yao.Ninachotarajia kusikia ni mkulima amevuna, mabua amempa mfugaji .Ikitokea kwa bahati mbaya ng’ombe zimeingia kwenye shamba la mkulima,mkulima na mfugaji wakae ,wazungumze  walipane ,familia ziishi kwa  usalama na amani”.

Mheshimiwa Papian amesema kwamba japokuwa utaratibu ulishawekwa kuhusu suala ya  kuchunga mifugo  kwenye mashamba,kwamba  mtu atakayechunga kwenye shamba  tathmini  ya uharibifu ifanyike,mfugaji alipe fidia ya uharibifu , wenyeviti wa vijiji waorodheshe majina ya wafugaji wanaochungia kwenye mashamba ili kuweza kupata majina hayo na kufahamu ni wakina nani wanaochochea uvunjifu wa amani  ili waweze kushughulikiwa. Akisisitiza kuhusu hilo Mhe. Papian amesema  ‘’ Mwenyekiti wa kijiji  anatakiwa atafute daftari,mkulima  ukilishiwa shamba lete jina la aliyechungia shamba kwa mwenyekiti,ukiwa na shahidi wako,mwenyekiti ataandika jina hilo kwenye daftari, na wewe uliyelishiwa pamoja na shahidi wako mtasaini. Mkuu wa mkoa anataka  kupata orodha ya watu wanaochunga mifugo katika mashamba ya watu”.

Katika hatua nyingine wakazi wa kijiji cha Kimana wameeleza kuhusu suala la  nyumba za walimu zilizopo katika shule ya msingi Kimana  kugeuka mahame baada ya walimu wa shule hiyo waliokuwa wakiishi katika nyumba hizo kuhama na kuziacha nyumba hizo zikiwa hazina mtu wa kukaa. Akijibu kuhusu kero hiyo Mhe Papian amemtaka mwenyekiti wa kamati ya shule hiyo kufuatilia suala hilo kuhakikisha kwamba walimu wanaishi katika nyumba za shule ili kuinua hali ya taaluma shuleni hapo.


Katika mkutano huo wanakijiji wamewasilisha kero mbalimbali ikiwemo ukosefu wa maji, uchache wa vyumba vya madarasa, ukosefu wa zahanati , na suala la barabara, ambapo kwa upande wa suala la zahanati, Mhe. Papian amewataka wananchi wa kijiji hicho kutofikiria kujenga zahanati,badala yake wafikirie na kuweka malengo ya kujenga kituo cha afya kwa sababu uwezo wa kujenga kituo cha afya wanao.Na kwamba wafanye  utaratibu wa kuandaa harambee ambapo wakulima na wafugaji wote katika eneo hilo watashiriki katika harambee hiyo kuchangia ujenzi wa kituo hicho cha afya, na yeye mwenyewe ataalika wabunge wenzake kushiriki katika harambee hiyo ili fedha zipatikane, ujenzi uanze mara moja.

 Katika kuhakikisha kwamba jambo hilo linatekelezeka ameutaka uongozi wa kijiji hicho kutenga eneo kubwa kwa ajili ya ujenzi wa kituo hicho. Kwa upande wa barabara wanakijiji hao wamesema kwamba barabara iliyokuwa ikitumika zamani ambayo kwa sasa haitumiki tena , ndiyo iliyokuwa fupi na rahisi kwao kutoka na kuingia kijijini hapo, tofauti na barabara inayotumika sasa ambayo ni ndefu sana,jambo linalowasababishia usumbufu mkubwa  hususani wanapokuwa na wagonjwa, kwani hulazimika  kulipa gharama kubwa sana za usafiri, tofauti na wakati walipokuwa wakitumia   barabara ya zamani.Mhe. Papiani ametoa majibu ya maswali yote,ambapo ameahidi kushughulikia kero zote zilizowasilishwa na wanakijiji hao ili waweze kuishi vizuri.



Mhe. Papian yuko katika ziara ya kukagua miradi ya maendeleo na kuzungumza na wananchi katika vijiji mbalimbali jimboni mwake. Ziara hiyo inafanyika kwa muda wa siku saba,ambapo katika siku ya kwanza ya ziara yake hiyo, miongoni mwa vijiji alivyovitembelea ni kijiji cha Kimana.




................ MWISHO.................



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa