Mkuu wa Wilaya ya Kiteto SSI Mbaraka Alhaj Batenga amewahimiza wananchi wa wilayani hapo kujenga tabia ya kufanya mazoezi kwaajili ya kuimairsha afya zao.
Agosti 26, 2023 Mh. Batenga aliwaongoza wananchi wa mjini Kibaya katika mbio za mazoezi za umbali wa kilometa mbili kuanzia katika ofisi zake na kuhitimishwa katika uwanja wa mpira mjini hapo ambapo mbio hizo zilihitimishwa na mazoezi ya viungo.
Mh. Batenga amesema kwamba mazoezi ya aina hayo yatakua sasa yanafanyika kila Jumamosi ya mwisho wa mwezi na mara baada ya kukamilisha mazoezi hayo kutafuatiwa na zoezi la usafi mjini hapo.
“Nawashauri watu kujiunga katika vikundi vya mazoezi ya kukimbia ili wawe wanafanya mazoezi mara kwa mara na sio kusubiria tu mazoezi ya mwisho wa mwezi” alisema Mh. Batenga.
Kibaya-Kiteto
Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto
Simu ya Mezani: +255 027-2552099
Simu ya kiganjani:
Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz
Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa