• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WAASWA KUUTUNZA UHURU WA NCHI.

Imetumwa : December 9th, 2023

Mkuu wa Wilaya ys Kiteto, SSI. Mbaraka Batenga, amewaasa wananchi wa Kiteto kuuenzi na kuuthamini Uhuru wa nchi ili kuliendeleza Taifa.

Hayo ameyasema Desemba 9,2023  katika Ukumbi wa Maktaba ya Wilaya kwenye maadhimisho ya Miaka 62 ya Uhuru wa Tanganyika ambayo katika Wilaya ya Kiteto yaliadhimishwa kupitia mdahalo maalumu wa kujadili mafanikio ya nchi katika miaka 62 ya Uhuru.

Mh. Batenga alisema kwamba kwavile uhuru upo, watu wanaweza wasione umuhimu wake ila pale ambapo uhuru umetoweka  ndipo utajulikana umuhimu wa uhuru.

“Lazima tuulinde uhuru wetu  maana hakuna mtu atakupa uhuru halafu asikunyemelee, tuulinde uhuru ili hata yule  aliyetupatia aone kua tulikua na dhamira  nzuri ya  kuudai uhuru ili kuliendeleza Taifa letu”, aliongeza Mh. Batenga.

Mdahalo huo ambao uliudhuriwa na watumishi, viongozi wa taasisi mbalimbali,wanafunzi na wananchi mbalimbali wakiwemo wazee maarufu wilayani hapo; ulitanguliwa na majaribio mbalimbali ya kikemia, fizikia na bailojia ambayo yalioneshwa na wanafunzi kutoka Shule ya Sekondari Kiteto.

Akiongea katika mdahalo huo, Mkurugenzi Mtendaji (W) Kiteto CPA. Hawa Abdul Hassan, amesema kwamba moja ya mafanikio katika miaka 62 ya  Uhuru ni pamoja na kuboreshwa kwa sekta ya elimu kupitia vifaa vya kujifunzia na kufundishia.

“Kabla ya kuanza mjadala huu  wanafunzi wametuonesha majaribio ya kisayansi kwa vitendo. Ila miaka ya nyuma majaribio hayo yalifanywa kwa nadharia tu” aliongeza Mkurugenzi Mtendaji huyo.

Nae mmoja ya wazee wa wilaya hiyo Mzee Lembulung Ole Kosiando alisema kwamba uhuru unatakiwa kuambatana na umoja na amani ila bila vitu hivyo viwili uhuru unakua hauna maana.

Vilevile Mzee maarufu wilayani hapo Mzee Mbaruku Said Muya alieleza jinsi ambavyo nchi imepiga hatua katika eneo la utawala na kueleza jinsi utawala wa serikali enzi za mkoloni ambao ulikua unaongozwa na mkuu wa wilaya ambapo mkuu wa wilaya alibeba majukumu yote na alitawala pia kimabavu.

“Enzi hizo mkuu wa wilaya ndio alikua kila kitu, yeye ndo hakimu, yeye daktari  na ulikua unaweza kwenda  ofisini kwake unashida ya kuonana nae ila ukaambiwa ana kazi nyingi na hapo huenda katulia tu anasoma gazeti hivyo itakupasa umsubiri mpaka amalize kusoma gazeni lake ndipo umuone kueleza shida yako” alisema Mzee Muya.

Kauli Mbiu ya Miaka 62 ya Uhuru ni “UMOJA NA MSHIKAMANO NI CHACHU YA MAENDELEO YA TAIFA LETU”.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa