• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WANANCHI WAASWA KUWAPA USHIRIKIANO MADAKTARI

Imetumwa : July 14th, 2025

Wananchi wa kijiji cha Ngabolo wilayani Kiteto, wameaswa kuwapa ushirikiano madaktari na wahudumu wa afya wote wanawapa huduma katika zahanati ya Ngabolo. 


Rai hiyo imetolewa na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Ndg. Ismail Ali Ussi,  Julai 13, 2025 wakati wa uzinduzi jengo jipya la zahanati hiyo. 


Akiongea baada ya kukagua zahanati hiyo, kiongozi huyo amesema kwamba amefurahishwa kujionea huduma ambazo zinatotelewa katika zahanati hiyo ikiwemo huduma ya kujifungua na huduma ya mama na mtoto. 


Aidha kiongozi huyo aliipongeza halmashauri kwa usimamizi mzuri wa ujenzi wa jengo hilo jipya kwani hiyo ni dhamiria ya Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma bora za afya. 


"Tunaposema Mwenge wa Uhuru unaleta upendo mahali ambapo hakuna upendo, matumaini ambapo hakuna matumaini basi tunamaanisha maana zahanati hii inaleta hayo", aliongeza Ndg. Ussi. 


Mbali na hayo kiongozi huyo alisema kwamba serikali imetumia fedha nyingi ili wananchi wasiweze kusumbuka hivyo alitoa rai kwa wananchi hao kulinda na kutunza miundombinu yote katika jengo hilo jipya na kuwapa ushirikiano madaktari na wahudumu wote wa afya kwenye zahanati hiyo kwani wanafanya kazi kubwa. 


Jengo hilo jipya la zahanati ya Ngabolo ambalo linalenga kutoa huduma kwa wananchi 5225, limezinduliwa na Mwenge wa Uhuru na ujenzi wa jengo hilo umegharimu kiasi cha fedha milioni 126. 


Kukamilika na kuzinduliwa kwa mradi huo kutasaidia kupatikana kwa huduma bora katika miundombinu iliyo bora na yenye kukidhi mahitaji ya sasa na hivyo kupunguza au kumaliza kabisa vifo vitokanavyo na uzazi, watoto wachanga na watoto chini ya miaka mitano. 


Aidha mradi huu pia utasaidia kutoa huduma za lishe, mapambano dhidi ya UKIMWI, malaria na afua zingine za afya kwa wanachi katika mazingira mazuri pamoja na watoa huduma wa zanahati hiyo.

Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa