• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

''Wanawake Tusinyamazie Ukatili wa Kijinsia'' WILAC Kiteto

Imetumwa : March 9th, 2019

Makamu mwenyekiti wa Jukwaa la wanawake Kiuchumi na Mtoa msaada wa sheria kutoka  Taasisi ya Msaada wa Sheria ( WILAC)  Bibi Mwadawa Ally akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.Maadhimisho hayo kiwilaya yamefanyika katika kijiji cha Ngipa - kata ya Engusero.

Wananchi kutoka katika  maeneo  na taasisi mbalimbali wakiwa katika maadhimisho ya siku ya wanawake duniani.



.................HABARI KAMILI........




Makamu mwenyekiti wa Jukwaa la Wanawake Kiuchumi wilaya ya Kiteto na mtoa msaada wa sheria kutoka katika Taasisi ya Msaada wa Sheria (WILAC) bibi Mwadawa Ally amewataka wanawake kutonyamazia vitendo vya ukatili wa kijinsia wanavyofanyiwa na waume zao majumbani.Mwadawa ameyasema hayo wakati wa maadhimisho ya siku ya Wanawake duniani ambayo kiwilaya yamefanyika katika kijiji cha Ngipa kata ya Engusero.


Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo Mwadawa amesema “ Kuna vitendo vingi vya ukatili wa kijinsia ambavyo wanawake mnafanyiwa huko majumbani,lakini mnakaa kimnya, inawezekana wengine mnakaa kimnya kwa sababu hamfahamu kwamba kufanyiwa hivyo ni ukatili,au mnafahamu  lakini mnaamua kunyamaza tu.Sio sahihi kunyamazia vitendo vya ukatili. Unapofanyiwa ukatili  toa taarifa kwenye vyombo vya usalama ili wahusika wa vitendo hivyo wachukuliwe hatua  stashiki.Kwa sababu kukaa kimnya kunatufanya wanawake tuendelee kuwa wanyonge kila siku.Tunajishughulisha sana kuinua uchumi wetu na wa familia zetu lakini bado tunaendelea kuwa wanyonge”.


Bibi Mwadawa  ameelezea aina mbili za ukatili wa kijinsia  ambapo aina ya kwanza ni ; wanawake wengi wamekuwa wakijishughulisha na shughuli mbalimbali za kujitafutia kipato, lakini wanapopata pesa, waume zao huwanyang’anya pesa hizo na kuzitumia wao kwa matumizi yao binafsi.Na ya pili ni wanawake  wanachukua mikopo kwa ajili ya biashara,lakini waume zao huchukua fedha hizo na kuzitumia kuolea,kupeleka kwa vimada ,kunywea pombe na kadhalika, hali ya kuwa wanawake hao ndio warejeshaji wa mikopo hiyo.Na pindi wanapojaribu kuhoji kuhusiana na  vitendo hivyo huishia kupata vipigo.


Aidha Mwadawa  amewataka wanawake kujitokeza, kujiunga kwenye vikundi na kufanya shughuli mbalimbali za ujasiliamali ili waweze kuondoa umaskini katika familia zao, kwa sababu uwezo wa kufanya hivyo wanao,kinachotakiwa ni kujiamini na kupambana kwa nguvu zote.Amesema kwamba jukwaa limeshazinduliwa tangu mwaka jana,lengo la jukwaa hilo ni kuwaunganisha wanawake kiuchumi kupitia shughuli mbalimbali za kijasiliamali.sambamba na kuwatafutia fursa  zitakazowawezesha kupanua shughuli zao ikiwemo mikopo kutoka katika taasisi kama mabenki,SACCOS na serikalini,hivyo ni vema wanawake wakahamasika kujiunga ili wainuke kiuchumi, watunze familia zao.


Wanawake  wengi wamekuwa mstari wa mbele katika kufanya shughuli mbalimbali ili kujipatia kipato na kukuza uchumi wao. Pamoja na mwamko na bidii hiyo, wamekuwa wakikutana na changamoto mbalimbali,ambapo changamoto hizo ndio chanzo cha wao kutokusonga mbele.Baadhi ya changamoto hizo hutokana na wanaume ambao  bado wana mitazamo hasi kuhusu mwanamke.Humtazama mwanamke kama chombo cha kuzalisha mali,na mali zinapopatikana,  mwenye mamlaka, sauti na haki ya umiliki wa mali hizo ni mwanaume.Mtazamo huo unawapa wanaume  ujasiri wa kujimilikisha na kutumia kwa nguvu kila kitu kilichopo nyumbani, bila kujali kimepatikana vipi na kipo kwa malengo gani.





..........MWISHO..............




Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa