• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WATOTO 57,435 KUPATA CHANJO YA SURUA RUBELLA KITETO

Imetumwa : February 16th, 2024

Mbunge wa Jimbo la Kiteto, Mh. Edward Ole Lekaita, amefanya uzinduzi wa Kampeni ya Kitaifa ya Chanjo ya Surua Rubella katika kata ya Sunya Februari 15, 2024.

Katika Kampeni hii ya Kitaifa ya siku nne kuanzia Februari 15-18, 2024, Halmashauri ya Wilaya Kiteto inalenga kuchanja watoto 57,435.

Chanjo ya Surua Rubella inatolewa bure kwa watoto walio na umri kuanzia miezi 9 hadi miezi 59 katika Hospitali ya Wilaya, Vituo vya Afya vyote, Zahanati zote na katika vituo maalumu  vilivyoteluliwa kwa muda kutoa huduma hiyo. Kampeni hii ina lengo la kuongeza kinga kwa walengwa.

                                                                                                   

Surua ni ugonjwa unaosababishwa na  virusi  vinavyoenezwa kwa njia ya hewa. Dalili za ugonjwa wa Surua ni pamoja na: Homa, mafua, Kikohozi, macho kuwa mekundu na kutoa majimaji; na vipele vidogo vidogo ambavyo huanza kwenye paji la uso, nyuma ya masikio na kusambaa usoni na mwili mzima

Rubella ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vya Rubella na kuenezwa kwa njia ya hewa. Mara nyingi huwapata watoto wadogo ingawa unaweza kumpata mtu wa umri wowote. Dalili zake hufanana na dalili za ugonjwa wa Surua.

Katika siku ya kwanza  ya Kampeni hii ya uchanjaji Februari 15,2024, Wilaya ya Kiteto imeweza kuchanja watoto 14,584 na hivyo kuweza kufikia lengo la uchanjaji kwa siku ambapo lengo  la siku lilikua kuchanja watoto 14,358.

                                                                                                  

Uzinduzi wa Kampeni hiyo uliambatana na zoezi la kukabidhi gari moja la wagonjwa (Ambulance) katika Kituo cha Afya cha Sunya. Uzinduzi huo  wa chanjo pamoja na hafla ya kukabidhi  gari hilo, mbali na kushuhudiwa na madiwani, wananchi na wataalamu kutoka katika Ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji, ulishuhudiwa pia na wabunge wawili ambao ni Mbunge wa Moshi Mjini Mh. Priscus Tarimo na Mbunge wa Msalala Mh. Kassim Idd.

                                                                                                                              

Gari hilo lililokabidhiwa katika Kituo cha Afya Sunya ni kati ya magari mawili (2) ambayo sekta ya Afya katika Halmashauri ya Wilaya  Kiteto ilipokea kutoka serikali kuu. Mwezi Desemba, 2023, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais TAMISEMI, Mh. Mohamed Mchengerwa  alikabidhi magari 13 kwa mkoa wa Arusha na Manyara kwa ajili ya usimamizi wa shughuli za Afya.

                                                                                                                                          

Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa