• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Watumishi Waaswa Kutofanya Kazi kwa Mazoea.

Imetumwa : March 2nd, 2019


.........HABARI KAMILI ............



Kaimu katibu tawala wa wilaya ya Kiteto ndugu  Fadhil Alexander amewaasa watumishi wilayani hapa kutofanya kazi kwa mazoea,.Alexander ameyasema hayo katika sherehe ya kuwaaga watumishi wa halmashauri waliostaafu  mwaka 2018 pamoja na kuaga mwaka 2018 na kuukaribisha mwaka 2019 iliyofanyika katika ukumbi wa CCM uliopo katika mji mdogo wa Kibaya mwishoni mwa wiki.


Akizungumza wakati  wa hotuba yake,Alexander ambaye amemuwakilisha Mkuuu wa wilaya ya Kiteto kama mgeni rasmi katika sherehe hiyo amesema “ Nawapongeza sana wazee wangu ninyi  ambao utumishi wenu umefika ukomo.Ni ukweli usiopingika kwamba kwa muda wote mliokuwa katika utumishi mmekutana na majaribu ,vikwazo na changamoto mbalimbali lakini kwa sababu ya uadilifu,bidii na moyo wa kujituma mliweza kuyashinda yote na hatimaye kufikia kustaafu, na leo hii mnaagwa kwa heshima .Watumishi wote walioko hapa wanatakiwa kujifunza kitu kutoka kwenu,wasifanye kazi kwa mazoea,bali wawe waadilifu na wenye bidii na moyo wa kujituma”.


Katika sherehe hiyo pia timu ya mpira wa miguu ya watumish wilaya(Watumishi FC) ilipongezwa kwa kupata ushindi na kutawazwa kuwa bingwa wa mkoa wa Manyara katika mashindano ya ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa.Kufuatia ushindi huo Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri alikuwa na haya ya kusema“hongereni sana kwa ushindi mlioupata.Ushindi tu ndicho kitu ambacho nilikuwa nakitamani kukisikia kutoka kwenu.Nimefurahi sana mmefanya kama nilivyokuwa natamani mfanye.Hii ndio timu sasa, na haya ndio mambo tunayoyataka.Ushindi huu unanipa moyo na nguvu ya kupambana kwa hali zote kuhakikisha kwamba mnaendelea mbele.Na ninyi sasa ni wajibu wenu kuongeza bidii kuhakikisha kwamba mnafanya vizuri zaidi mtakapokwenda  ngazi ya taifa’’.


Baada ya pongezi hizo harambee fupi ilifanyika kwa lengo la  kuiunga mkono timu hiyo ambapo fedha taslim kiasi cha sh. 776,500,na ahadi sh 1,540,000 zilipatikana.Aidha wastaafu wote  walipewa zawadi.Na katika kuonyesha shukrani na furaha yao, wastaafu hao hawakuwa nyuma, walimshukuru Mkurugenzi Mtendaji kwa kuwajali kiasi cha kuwaandalia sherehe ya kuwaaga, shukrani yao hiyo iliambatana na zawadi kwa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri.Baada ya matukio yote hayo kilichofuata ni kula na kunywa na kucheza muziki,ambapo watumishi wa taasisi mbalimba walijumuika pamoja katika kucheza muziki.


Halmashauri ya wilaya ya Kiteto imekuwa muandaaji wa  sherehe hizo kwa miaka 3 mfululizo sasa, ambapo lengo lake kuu

 ni kuwapongeza wastaafu kwa utumishi wao sambamba na kuwakutanisha watumishi wa taasisi mbalimbali za umma na za binafsi kukaa pamoja kufurahi na kushirikishana mawazo na uzoefu ili kuongeza ufanisi katika utendaji kazi.




..........MWISHO..............


Matangazo

  • KUITWA KWENYE USAILI September 01, 2025
  • TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MIKOPO INAYOTOLEWA KWA VIKUNDI VYA WANAWAKE, VIJANA NA WATU WENYE ULEMAVU September 01, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • DAS KITETO AWAHIMIZA WANANCHI KUJENGA UTAMADUNI WA UWEKEZAJI.

    September 11, 2025
  • UGONJWA WA HOMA YA INI (HEPATITIS B) NI TISHIO LA MAISHA LAKINI TUMAINI LIPO KUPITIA CHANJO

    September 04, 2025
  • DC MWEMA AFUNGUA RASMI ZAHANATI YA ENGUSERO SIDAN

    August 31, 2025
  • SAFARI YA KM 42 KUFUATA HUDUMA ZA AFYA SASA NI HISTORIA NDIRIGISHI

    August 30, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa