• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Waziri Jaffo kuwashughulikia wakandarasi wababaishaji

Imetumwa : November 18th, 2017


            Waziri  wa OR- TAMISEMI  Mh. Suleimani Jaffo akitoa maelekezo kuhusu mkandarasi aliyekuwa akifanya kazi ya ujenzi wa barabara   KM 44  Kutoka namelock.                                 

                                                                                                                 

                        Waziri  wa OR- TAMISEMI  Mh. Suleiman Jaffo akikagua barabara ya Namelock - Sunya  kama inavyoonekana katika picha                                                                                                                                  

 Waziri  wa OR - TAMISEMI Mh.Suleimani Jaffo akielekea kukagua  wodi ya wazazi katika kituo cha afya Sunya alipotembelea kituo hicho katika ziara yake wilayani Kiteto.

                                                                                                                                   

                      Waziri  wa OR - TAMISEMI Mh.Suleimani Jaffo akikagua chumba cha kujifungulia katika kituo cha afya Sunya alipotembelea kituo hicho katika ziara yake wilayani Kiteto.Upande wake wa kulia ni mkuu wa wilaya ya Kiteto Mh. Tumaini Magessa.

                                                                                                                       

            Waziri  wa OR - TAMISEMI Mh.Suleimani Jaffo akizungumza na wananchi wa Sunya katika mkutano wa hadhara katika ziara yake wilayani Kiteto

                                                                                                                                                               

                                                                                                                                                              


           Wananchi wa kata ya Sunya wakimsikiliza  Waziri  wa OR - TAMISEMI Mh.Suleimani Jaffo  


                                                                                                                                  HABARI KAMILI....                                      


Waziri Jaffo  kuwashughulikia wakandarasi wababaishaji

Waziri wa Ofisi ya Rais TAMISEMI mheshimiwa Suleimani Jaffo ameahidi kuwashughulikia wakandarasi wababaishaji. Mheshimiwa Jaffo ameyasema hayo wakati akikagua ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 88.1 ya Namelock - Sunya, ambapo alipokea taarifa ya kusitishwa kwa mkataba wa mkandarasi aliyekuwa amepewa kazi ya ujenzi wa barabara hiyo kilometa 44 kutoka namelock.Mheshimiwa Jaffo amesema kwamba pamoja na kusitisha mkataba wa mkandarasi huyo , ili kumsaidia  kwa sababu  ni mkandarasi Mtanzania, anatoa siku tano  hadi tarehe 22 Novemba 2017, katika  siku  hizo, meneja wa TARURA Wilaya ya Kiteto amuite wakae nae waangalie kazi aliyoifanya, alipwe anachostahili waachane nae. Baada ya Jumatano kama atakuwa hajafika ,serikali itafanya utaratibu wa kumpeleka mahakamani kwani alikuwa na lengo la kuitapeli serikali kwa sababu alishakiuka mkataba kwa kushindwa kutimiza vigezo vinavyotakiwa kama vilivyoainishwa kwenye  mkataba ikiwemo kuleta dhamana ya utendaji kazi. Mheshimiwa Jaffo amesisitiza kuwa katika ofisi yake wakandarasi kama hao hawataki kabisa, hivyo kama mkandarasi huyo atakuwa hajatekeleza alichoagiza, jina la mkandarasi huyo  lipelekwe ofisini kwake , na atahakikisha kwamba hapati kazi yoyote ya TARURA katika jamhuri ya muungano wa  Tanzania. 


Aidha Mheshimiwa Jaffo amesema kwamba  ameridhishwa na hatua ilyochukuliwa na meneja wa TARURA wilaya ya Kiteto mhandisi Gerald Matindi ya kusitisha mkataba wa mkandarasi huyo kwa sababu  ameshindwa kufanya kazi hiyo kwa kasi na kiwango kinachotakiwa, kwani  amefanya kazi kwa asilimia saba ambapo ni kilometa kumi na saba tu kati ya kilometa 44, tangu  ameanza kazi hiyo  tarehe 17/06/2017.Vilevile mheshimiwa Jaffo amemsifu   mkandarasi anayejenga barabara hiyo kilometa 44.1 baada ya Namelock, ambapo amesema kwamba mkandarasi huyo yuko vizuri sana, Kazi yake ni nzuri na kasi ya utendaji kazi wake ni ya kuridhisha.
 
Nae  mtendaji mkuu wa TARURA  Tanzania mhandisi Victor Seif amesema kwamba  wakandarasi wa aina hiyo kama watakuja kuomba kazi hawana uwezo hawatawavumilia kabisa, hata katika tathmini.Na ikitokea kwamba wameleta vigezo ambavyo sio vya kweli wakapewa kazi ,wakati wa kutekeleza kazi hizo kama hawatafanya vizuri  TARURA itasitisha  mikataba yao. Mhandisi Seif anasema   ‘‘Mkandarasi huyu hatapewa tena kazi ya kiwango hiki, hadi atakapotuhakikishia kuwa anavifaa vya kutosha na wataalamu wa kutosha kusimamia kazi ya ukubwa huu .Pia Maagizo ya mheshimiwa waziri tumeyapokea,mkandarasi huyu tutamuita tutaangalia kazi aliyofanya , kama kuna kitu anadai tutamlipa ili tuachane nae, akikaidi tutaanza taratibu za kumuweka kwenye orodha ya wakandarasi ambao hatutawapa kazi tena ,tutaanza taratibu hizo kwa sababu anayetakiwa kufanya hivyo ni PPRA”.

Katika hatua nyingine mheshimiwa Jaffo ametembelea Kituo cha afya cha Sunya ambapo amekagua wodi ya wazazi na chumba cha  kujifungulia,  baada ya kuona hali halisi ya  ya kituo hicho, amemuagiza kaimu mkurugenzi wa halmashauri  ya wilaya ya Kiteto ndugu  Emmanuel Mwagala kuwa  kufikia ijumaa ya tarehe 24/11/2017 ujenzi wa wodi ya wazazi,chumba cha upasuaji,maabara na chumba cha kuhifadhia maiti katika kituo hicho uwe umeanza .Vilevile amezungumza na wananchi wa kata ya Sunya katika mkutano wa hadhara  , ambapo amesisitiza juu ya usimamizi mzuri wa fedha za miradi ya maendeleo hususani barabara na ushirikishwaji wa wananchi katika miradi hiyo ili iweze kutekelezwa kwa ufanisi . Katika mkutano huo mkuu wa wilaya ya Kiteto  mheshimiwa Tumaini Magessa amemueleza mheshimiwa waziri kuhusu migogoro ya mipaka kati ya wilaya ya Kiteto na Kilindi. Pia mbunge wa jimbo la Kiteto mheshimiwa Emmanuel Papian alieleza kero za wananchi wa Sunya, kero kubwa ikiwa ni msitu wa SULEDO na uongozi wa SULEDO ,ambapo  wananchi walionyesha dhahili kuguswa sana na kero hiyo , hapa mheshimiwa Jaffo anatoa tamko anasema ‘‘Nitaunda timu maalumu kuja kushughulikia jambo hili, timu hiyo nitakayoiunda nitawapa hadidu rejea kubaini hizo fedha zinazokusanywa zinaenda wapi?Tusivumilie hii tabia ya wananchi wanakuwa na malalamiko siku zote. Leo mimi nimepokelewa na mabango, kesho Rais wangu atakuja atapokelewa na mabango, lazima tuchunguze kuna nini hapo? Nini chanzo cha tatizo? Kama mmeuhifadhi msitu , na nimesikia kuwa mna katiba yenu, na bila shaka mna taratibu zenu,nadhani mna malengo mahususi na msitu huo, sasa kama kuna watu wamejimilikisha msitu huo ,tutaangalia taratibu baada ya timu hiyo kumaliza kazi yake. Kama kuna wezi ,utaratibu wa wezi unajulikana ni kufikishwa katika vyombo vya sheria”. Kuhusu migogoro ya mipaka  kati ya Kilindi na Kiteto, mheshimiwa Jaffo amesema kwamba watalifanyia kazi suala  hilo  ili  lifike mwisho .




Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa