• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Waziri wa TAMISEMI afanya ziara wilayani Kiteto

Imetumwa : November 5th, 2017

                 Waziri wa TAMISEMI  Mhe. Suleiman Jaffo akisaini kitabu cha wageni katika ikulu ndogo ya  Kibaya  mara baada ya kuwasili  wilayani Kiteto

Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mhe. Tumaini Magessa akiwasilisha taarifa fupi ya ujenzi wa jengo jipya la halmashauri ya wilaya ya Kiteto  kwa waziri wa TAMISEMI Mhe.Suleiman Jaffo


Waziri wa TAMISEMI  Mhe. Suleiman Jaffo  akikagua  mradi  wa  ujenzi wa jengo jipya  la halmashauri ya wilaya ya Kiteto

                Waziri wa TAMISEMI Mhe.Suleiman Jaffo akitoa maelekezo kuhusu mradi wa ujenzi wa  Barabara ya Nameloku - Sunya 

Mkuu wa shule ya sekondari  Engusero akimkaribisha waziri wa TAMISEMI  Mhe. Suleiman Jaffo alipotembelea shuleni hapo katika ziara yake wilayani Kiteto


Wanafunzi wa shule ya sekondari Engusero wakiwa wamekusanyika  kumsikiliza waziri wa TAMISEMI mhe. Suleiman Jaffo alipotembelea shuleni hapo katika ziara yake wilayani Kiteto

          Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo akiwa katika picha ya pamoja na wasichana wanaosoma kidato cha tano katika shule ya sekondari Engusero

          Waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo akiwa katika picha ya pamoja na  wavulana wanaosoma kidato cha tano katika shule ya sekondari Engusero

Watumishi wa Kituo cha afya cha Engusero wakimkaribisha  waziri wa TAMISEMI  Mhe. Suleiman Jaffo alipotembelea kituo hicho katika ziara yake wilayani Kiteto

 Waziri wa TAMISEMI  Mhe. Suleiman Jaffo  akiingia katika kituo cha afya  cha Engusero  kuona hali ya kituo hicho  katika ziara yake wilayani Kiteto

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Jaffo akizungumza na wakazi wa kata ya Engusero baada ya kukagua miradi  katika ziara yake wilayani kiteto

Wakazi wa  kata ya Engusero wakiwa wamekusanyika kumsikiliza waziri wa TAMISEMI Mhe. Suleiman Jaffo 


HABARI KAMILI...


Waziri wa TAMISEMI  afanya ziara wilayani Kiteto


Waziri wa  Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa mheshimiwa Suleiman Jaffo amefanya ziara wilayani Kiteto mkoa wa Manyara.Katika ziara hiyo Mhe. Jaffo amekagua mradi wa ujenzi wa jengo jipya la halmashauri ya wilaya ya Kiteto, ujenzi wa barabara ya Nameloku – Sunya,  ametembelea  shule ya sekondari ya Engusero pamoja na kituo cha afya cha Engusero, na kuzungumza na wakazi wa kata ya Engusero .

Akiwasilisha taarifa fupi ya mradi wa ujenzi wa jengo jipya la halmashauri ya wilaya ya Kiteto kwa waziri wa TAMISEMI mheshimiwa Suleiman Jaffo, mkuu wa wilaya ya Kiteto mheshimiwa Tumaini Magessa amesema kwamba  jengo hilo lilianza kujengwa tarehe 26/10/2016 na kwamba hatua ya ujenzi huo ni ya kuridhisha , aidha mheshimiwa Magessa  amemueleza  mheshimiwa  Jaffo kuwa mkandarasi yuko nyuma ya muda kutokana na kucheleweshewa fedha za mradi huo, na kwamba  kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 3.4 kimebaki ili kukamilisha mradi huo. Jengo hilo la gorofa mbili hadi kukamilika kwake litagharimu kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 4.5.

Akikagua mradi huo wa ujenzi wa jengo  jipya la halmashauri , mheshimiwa Jaffo amesema kwamba ameridhika na kazi iliyofanyika  na kumpongeza  mkandarasi  kwa kazi nzuri, mheshimiwa Jaffo ameisifu kampuni inayojenga jengo hilo, ambapo amesema  kwamba kampuni hiyo  ni ya kizalendo lakini inafanya vizuri sana, aidha  amemuahidi   mkandarasi kuwa   fedha zitapatikana,wala wasihofu anachotaka ni kazi ikamilike. Mheshimiwa Jaffo pia  amemuagiza  afisa ardhi kuhakikisha kuwa eneo hilo  linapimwa na linapata  hati ili kuzuia migogoro baina ya serikali na wananchi wa eneo hilo .

Katika ukaguzi wa mradi wa barabara,  mheshimiwa Jaffo amesema kwamba hajaridhika na kasi ya mkandarasi  anayetengeneza barabara hiyo kutoka  Nameloku. Akijibu hoja hiyo ya mheshimiwa waziri meneja wa TARURA  wilaya ya Kiteto mhandisi Gerald  Matindi  amesema kwamba wameshakaa kikao cha juu cha menejimenti kumjadili na wanalengo la kukatisha mkataba wake, isipokuwa  ameomba wiki moja menejimenti iangalie  utendaji wake  kama  wataridhika au la.Wakishaangalia kama hatakuwa amefanya kazi kiasi cha kuridhisha , mshauri wao  ataanza taratibu za kusitisha mkataba wa mkandarasi huyo. Pamoja na majibu ya meneja huyo wa TARURA  mheshimiwa Jaffo  anatoa angalizo kwa meneja wa huyo anasema “Tumeanzisha wakala wa TARURA , lengo kubwa ni kwamba barabara zitengenezwe kwa uhakika zaidi, na tumekuteua wewe meneja ukae hapa lengo ni kwamba usifikirie jengo, usifikirie choo kimebomoka ,usifikirie darasa halipo, lengo lako ukiamka asubuhi unafikiria jinsi gani barabara ziimarike . Ndio maana kubwa ya kuweka wakala wa TARURA. Jambo la pili  tunataka wakandarasi ambao walikuwa wakifanya kazi kimazoea , katika utaratibu wa sasa hivi wasiwepo. Tunataka barabara zenye ubora.Kwa namna ambavyo mmeshasukumana nae ,hadi kufikia hatua ya kutakaka kusitisha mkataba wake, mimi napata mashaka kama mkandarasi huyu ataweza kujenga barabara hii kwa kiwango kinachotakiwa. Angalieni uwezo wa huyu mkandarasi je unatosha? tusiwe na mtu ambae ataharibu barabara zetu. Muangalieni  kama hana uwezo fukuza”. Kutokana na kutoridhishwa na kasi  mradi huo wa ujenzi wa barabara , mheshimiwa  Jaffo ameahidi kurudi Kiteto tarehe 17 /11 kwa ajili ya kukagua barabara hiyo ili kuona kazi imefika wapi,na kama haijafanyika atataka kujua ni hatua gani zimechukuliwa dhidi ya mkandarasi huyo. Mradi huo wa Barabara ya Nameloku – Sunya una kilomita 88.1 , hadi kukamilika kwake utagharimu  kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 6.4.

Vilevile mheshimiwa Jaffo alitembelea shule ya sekondari Engusero. Katika shule ya Sekondari Engusero mheshimiwa Jaffo amekagua madarasa mapya mawili yaliyojengwa na halmashauri pamoja na bweni la wasichana, ambapo ameupongeza  uongozi wa  wilaya ya Kiteto kwa juhudi kubwa waliyoifanya kuhakikisha kuwa wanakuwa na shule mbili za kidato cha tano , pia amewapongeza walimu wa shule hiyo kwa kazi kubwa wanayofanya. Aidha  mkuu wa wilaya  ya Kiteto mheshimiwa Tumaini Magessa alimweleza waziri kuwa  wamefanikiwa kujenga madarasa  mawili na mabweni mawili kwa ajili ya kidato cha tano, mwakani  wanafunzi hao waliopo kidato cha tano wataingia kidato cha sita, wanafunzi wengine wa kidato cha tano watakuja,hawatakuwa na mahali pa kuwalaza. Nae Mwenyekiti wa halmashauri ya Wilaya ya Kiteto mheshimiwa Lairumbe Mollel alimuomba mheshimiwa waziri  kwamba serikali iwaunge mkono katika kusaidia kukamilisha miradi ambayo wao kama halmashauri wamekuwa wakiianzisha kwa kutumia fedha za ndani, ambapo mheshimiwa Jaffo aliahidi  kuwaunga mkono kwa kuongeza madarasa mawili ,mabweni  mawili pamoja na vyoo  . Mheshimiwa Jaffo pia alizungumza na wanafunzi  wanaokaa bweni katika shule hiyo na kuwaasa kuzingatia masomo na kutokujiingiza katika mambo yasiyowahusu, mambo ambayo yataharibu mustakabali wa elimu yao na maisha yao kwa ujumla. Pia mheshimiwa Jaffo aliwapongeza wanafunzi hao kwa kuweka mazingira yao ya shule vizuri na kuwaahidi kuwa serikali itafanya kila liwezekanalo kuboresha mazingira ya shule hiyo ili vijana wanaochaguliwa kujiunga na shule hiyo  waweze kusoma vizuri. Mheshimiwa Jaffo  aliwaeleza wanafuzi hao kwamba ameshaahidi kuongeza madarasa mawili, mabweni mawili, matundu ya vyoo ,na kama uwezekano upo bwalo la chakula ambalo liko katika hatua ya lenta limaliziwe na pia wajengewe  jiko zuri,kwani ameona jiko linalotumika shuleni hapo lina hali mbaya,halistahili kutumika kupika chakula cha watoto hao.

Aidha mheshimiwa Jaffo alitembelea kituo cha afya cha Engusero ambapo alikagua stoo ya kuhifadhia madawa, wodi  na jengo la upasuaji. Akiwa kituoni hapo ,mheshimiwa Jaffo  alielezwa kuhusu changamoto wanazokabiliana nazo watumishi katika kituo hicho, changamoto hizo ni  uhaba wa baadhi ya dawa, kutokuwepo kwa chumba cha upasuaji kutokana  na chumba kilichopo kuthibitishwa na wataalamu baada ya ukaguzi kutokufikia kiwango cha kutumika kwa upasuaji, kutokuwepo kwa wodi ya kina mama ambao wanangojea kujifungua na ambao wameshajifungua, hali inayosababisha  wakina mama hao kuchanganyika na wagonjwa wengine .Baada ya kusikia changamoto hizo mheshimiwa Jaffo ameahidi   kutafuta fedha kwa ajili ya kujenga chumba cha upasuaji cha kisasa , kuongeza wodi  ya kina mama wanaongojea kujifungua na wodi ya wakina mama waliojifungua,na kuleta vifaa vyote vinavyohitajika ili kituo hicho kiweze kuwahudumia  wakazi wa Engusero kwa ubora zaidi.

 Mheshimiwa  Jaffo  alihitimisha ziara yake wilayani Kiteto  kwa mkutano wa hazara ambapo  alizungumza na wakazi wa kata ya Engusero. Mheshimiwa Jaffo  aliwaeleza wananchi kuwa ndani ya miaka miwili ya uongozi wa Mheshimiwa Rais Magufuli amesimamia kidete kuhakikisha kwamba rasilimali za nchi zinalindwa kwa nguvu zote.Raisi anapambana kuboresha maisha ya watanzania, hali ya afya ilikuwa mbaya,bajeti ya afya ilikuwa duni sana,Rais  ameongeza  bajeti ya madawa  kutoka bilioni thelasini na moja kwa mwaka  hadi bilioni mia mbili sitini na tisa kwa mwaka.Hali ya vituo vya afya ilikuwa duni , Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli inajenga vituo vya  afya 172, na wilaya ya kiteto ni miongoni mwa wilaya zilizopo katika mpango wa kujengewa vituo vya afya ambapo  imeshaingiziwa shilingi milioni mia nne kwa ajili ya kujenga kituo cha afya cha Sunya. Mheshimiwa Jafo anasema “Licha ya kwamba tumeleta fedha katika kituo cha Sunya,na zitakuja fedha nyingine shilingi milioni mia tatu na ishirini, huko Sunya, kituo kikikamilika tutaleta vifaa vyote. Lakini nimefika katika kituo chenu cha afya hapa  nimegundua na hapa kuna changamoto kubwa sana.Kwa uwezo wa Mungu ,sio kwa uwezo wangu,Mungu akijalia nitaleta fedha tutajenga  jengo la upasuaji la  kisasa hapa ,tutajenga wodi ya  wazazi, tutajenga jengo la kuhifadhia maiti ili mtu akifariki ahifadhiwe hapahapa ”.

Naye mbunge wa Kiteto mheshimiwa Emmanuel Papian  mbele ya wananchi wa Engusero waliokusanyika  ili kumsikiliza  mheshimiwa waziri akatumia fursa hiyo kuwasilisha kero za wananchi wa Kiteto kwa mheshimiwa waziri, mheshimiwa Papian anasema  “Wilaya ya kiteto ina tatizo la uhaba wa watumishi wa kada mbalimbali , mheshimiwa waziri naomba katika ajira  zitakazotoka uitazame wilaya ya Kiteto kwa jicho la huruma, wilaya ya Kiteto ikumbukwe kwa kuletewa watumishi ambao watakuja kuchapa kazi .Pia tuna  tatizo la maji  nakuomba mheshimiwa waziri kupitia wizara yako ya  TAMISEMI kitengo cha maji utusaidie kupata maji.







Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa