• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Kiteto Yadhamiria Kuinua Kiwango cha Elimu na Ufaulu

Imetumwa : November 1st, 2018

Mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Mhe. Lairumbe Mollel  akizungumza wakati  akifungua  kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika oktoba 30 -31 katika ukumbi wa halmashauri.

Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Ndg. Tamim Kambona akizungumza wakati wa kikao cha baraza la madiwani.

Baadhi ya madiwani wakiwasilisha taarifa za kata zao katika kikao cha baraza la madiwani.

Waheshimiwa madiwani , wataalamu mbalimbali wa Halmashauri ,wageni wakiwa katika kikao cha baraza la madiwani .


............HABARI KAMILI...........



Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto  mheshimiwa Lairumbe amewapongeza  na kuwashukuru walimu pamoja idara ya elimu chini ya Mkurugenzi ,kwa kufanya vizuri katika matokeo ya darasa la saba,hali iliyosababisha ongezeko la ufaulu  la 10.54 % .Amesema kwamba kiwango hicho cha ufaulu kinaonyesha kuwa wilaya inasonga mbele.Mheshimiwa Mollel ametoa pongezi na shukrani hizo katika  kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri, Oktoba 30, mwaka  huu.


Akizungumza kuhusu kiwango cha ufaulu Mheshimiwa Mollel amesema kwamba  katika mwaka huu 2018 ,ufaulu wa wilaya ya Kiteto umekuwa ni  69.55% , wakati mwaka jana 2017  ilikuwa ni 59.01 % .Akionyesha kufurahishwa na kiwango hicho cha ufaulu , Mhe. Mollel amesema “Katika shule ambazo zimefanya vizuri,shule ya msingi Boma imeshika nafasi ya kwanza kimkoa, na imeshika nafasi ya 54 kitaifa, shule hiyo moja imetutoa kimasomaso. Shule kushika nafasi ya 54 katika shule zaidi ya 10,000 sio jambo dogo,ni jambo kubwa sana. Walimu wamefanya kazi nzuri sana”.


 Mhe. Mollel  amezitaja kata ambazo ziko katika kumi bora kwa ufaulu,ambapo amesema, kata ya kwanza ni Kaloleni,kata ya pili ni Partimbo,kata ya tatu ni Ndedo,kata ya nne Magungu,ya tano ni Bwagamoyo ,ya sita ni Matui, ya saba ni Kibaya . Ya nane ni Chapakazi, ya tisa ni Kijungu na ya kumi ni Ndirigishi .


Kadhalika Mhe Mollel amesema kwamba kwa sababu ufaulu unaonekana uko vizuri,wao kama madiwani wahakikishe kwamba wanafunzi  waliofaulu wanapata madarasa na viti vya kukaa.Isije ikatokea kwamba watoto wameshindwa kwenda shule kwa sababu ya ukosefu wa vyumba vya madarasa.Ameongeza kwamba Mkurugenzi ana sehemu yake, lakini wao kama wazazi ,na wenyeviti wa ODC lazima wahakikishe kwamba wanafunzi waliofaulu wanakwenda shule.


Aidha Mhe. Mollel amewataka Wahe. madiwani kwenda kujipanga kuhakikisha kwamba wanafunzi watakaopangiwa kwenye kata zao, wote wanakwenda shule.Sambamba na hayo amewahimiza kwenda kujipanga vema kutoa zawadi kwa walimu wa shule zilizofanya vizuri ili kuwatia moyo kufanya vizuri zaidi.


Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Kiteto  ndugu Tamim Kambona amesema kwamba wamepanga mikakati ili kuhakikikisha kwamba wanaendelea kuboresha elimu katika wilaya hii; mikakati hiyo ni kuimarisha ushirikiano kati ya walimu,wazazi na wanafunzi, kuwatembelea walimu na wanafunzi kila wakati,kuhakikisha ufundishaji unafanyika vizuri,vile vile wameendelea kutoa motisha,kwa shule ambazo zimekuwa zikifanya vizuri.Na kwamba  shule ya msingi Boma ambayo imekuwa ya kwanza kimkoa mwaka huu wanawatafutia zawadi kubwa zaidi ya ile waliyowapa shule ya msingi Laalakir ambayo ilishika nafasi ya kwanza mwaka 2017, ambapo wanaamini kwamba kwa kufanya hivyo wanazipa  changamoto shule hizo kuongeza jitihada ili ziweze kufanya vizuri zaidi. Pia wameendelea kuhamasisha utoaji wa vyakula shuleni,na kwamba huo ndio msimamo wao, kuhakikisha wazazi wanachangia vyakula mashuleni, watoto wapate chakula shuleni wasome vizuri,kiwango cha ufaulu kiongezeke zaidi.


Katika hatua nyingine diwani wa kata ya Partimbo Mhe. Paulo Tunyoni amesema kwamba ili kuinua kiwango cha elimu wazee watano wa jamii ya kifugaji kutoka katika kitongoji cha Nabirikunya wameamua kujenga shule kwa kutumia mifugo yao,na kwamba hadi sasa wazee hao wameshachanga kiasi cha shilingi 13,500,000/= ,ambapo kazi ya ujenzi wa madarasa pamoja na ofisi za walimu  itaanza mnamo tarehe 02/11/2018 .


 Idara ya elimu msingi na idara ya elimu sekondari wilaya ya Kiteto, chini ya uongozi na usimamizi makini wa Mkurugenzi Mtendaji Tamim Kambona imekuwa ikifanya jitihada za makusidi kuhakikisha kwamba ,inaboresha elimu, inainua taaluma na kuongeza kiwango cha ufaulu mwaka hadi mwaka.




.......MWISHO..........


Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • HAYAWI HAYAWI SASA YAMEKUA: HATIMAYE KALOLENI YAPATA SHULE MPYA YA MSINGI

    July 30, 2025
  • SHULE YA MSINGI KINANGALI NAYO YANUFAIKA NA MRADI WA BOOST

    July 30, 2025
  • SERIKALI YA AWAMU YA SITA YAENDELEA KUWEKEZA KWA VITENDO: KURASH YAPATA MRADI MWINGINE WA MILIONI 153 KUPITIA BOOST

    July 30, 2025
  • KATA YA BWAWANI YAPATA MRADI WA SHULE MPYA YA ELIMU MSINGI.

    July 28, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa