• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

WMA MAKAME YAINGIA MKATABA WENYE THAMANI YA BIL.10

Imetumwa : November 19th, 2023

Jumuiya ya Hifadhi ya Wanyamapori Makame (WMA Makame), imeingia mkataba mpya   wenye  thamani  ya shilingi bilioni 10 na kampuni iitwayo UNTAMED Horizons Camps & Safaris LTD.

Mkataba huo umesainiwa Novemba 18, 2023 katika Ofisi za Jumuiya zilizopo katika kijiji cha Makame huku ukishuhudiwa na wananchi pamoja na viongozi mbalimbali wa serikali wilayani hapo.  

Akiongea katika tukio hilo, Mwenyekiti ya Halmashauri ya Wilaya Kiteto, Mh. Abdala Bundala amewakaribisha wawekezaji hao na kuahidi kuwapa ushirikiano kwani wanatambua na wanaona matokeo ya uhifadhi kwenye Halmashauri yake.

Nae Mkurugenzi Mtendaji (W), CPA. Hawa Abdul Hassan,amesema kwamba anatambua umuhimu wa utalii katika Halmashauri  hususani katika kuchangia mapato ya Halmashauri  na kusema kwamba kutokana na shughuli za utalii katika hifadhi hiyo, taarafa ya Makame imekua na uhakika wa upatikanaji wa fedha za utekelezaji wa miradi ya maendeleo.

Katika hafla hiyo ya kusaini mkataba, kampuni ya UNTAMED pia  imekabidhi gari aina ya Land Cruiser Hard Top lenye thamani ya shilingii milioni 150 kwa ofisi za WMA Makame pamoja na pikipiki mbili kwaajili ya kusaidia shughuli za doria katika hifadhi hiyo. Pamoja na hayo kampuni hiyo imekadhi kompyuta  mpakato moja pamoja na printa  mashine moja kwaajili ya ofisi ya WMA Makame

Mkataba huo umekua na neema kwa wananchi katika vijiji vya jumuiya hiyo kwani  Kampuni ya UNTAMED pia imeahidi kutoa Bima ya Afya kwa wazee 100 kutoka katika vijiji hivyo pamoja na kuchimba visima vitano (kila kijiji kisima kimoja)  vya maji ambavyo vitaendeshwa kwa nishati ya jua.

Aidha, kampuni hiyo imeahidi kuchimba mabwawa mawili na imeahidi kufungua  barabara kwa urefu kwa takribani km 100 ili kuunganisha vijiji hivyo

Nae Mbunge wa Jimbo hilo Mh Edward Olelekaita, aliisihi Kampuni hiyo kutekeleza ahadi kama walivyoahidi na pia kuwasihi kufanya kazi na jumuiya na sio mtu mmoja mmoja.

Pia Mkuu wa Wilaya Kiteto,SSI. Mbaraka Batenga  ambaye ndiye alikua Mgeni rasmi katika hafla hiyo,  mbali na kuwakaribisha wawekezaji hao alisema kwamba anafahamu Kampuni hiyo inafanya biashara nyingine ikiwemo biashara ya vituo vya mafuta na vifaa vya ujenzi. Vilevile aliialika Kampuni hiyo kufika na kuwekeza katika biashara ya Vituo vya Mafuta kwakua Kiteto bado inauhitaji wa kupata msambazaji mkubwa wa mafuta.

WMA Makame ambayo inaundwa na vijiji vitano, imeingia mkataba na kampuni hiyo kwaajili ya shughuli za uwindaji katika kitalu cha Masai East. Vijiji vinavyounda WMA Makame ni  Makame, Ndedo, Ngaboro, Katikati na Irkiushiobor.

Matangazo

  • TANGAZO NAFASI ZA KAZI July 23, 2021
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI NAFASI YA UTENDAJI WA KIJlJI III August 26, 2021
  • TANGAZO LA KUKODISHA VIBANDA March 01, 2022
  • TANGAZO LA KUITWA KWENYE USAILI SEPTEMBA 2023 September 03, 2023
  • Angalia zote

Habari mpya

  • TABIA MBAYA ZA WATUMUSHI ZINAHARIBU SIFA ZA TAASISI

    May 01, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI KITETO LIMEMPONGEZA RAIS SAMIA.

    May 30, 2025
  • PONGEZI KWA WANANCHI KWA KUTUNZA MAZINGIRA

    April 28, 2025
  • TUUENZI MUUNGANO WETU

    April 27, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa