• Wasiliana nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe watumishi |
    • Malalamiko |
Kiteto District Council
Kiteto District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Kiteto

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dhima na Dira
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Idara
      • Rasilimali watu na Utawala
      • Kilimo,Umwagiliaji na Ushirika
      • Mipango,Takwimu na Ufuatiliaji
      • Elimu ya Msingi
      • Elimu ya Sekondari
      • Usafi na Mazingira
      • Afya
      • Mifugo na Uvuvi
      • Ujenzi
      • Ardhi na Maliasili
      • Fedha na Biashara
      • Maji
      • Maendeleo ya Jamii
    • Vitengo
      • Manunuzi na Ugavi
      • Ukaguzi wa Ndani
      • Uchaguzi
      • Sheria
      • Teknolojia,Habari ,Mawasiliano na Mahusiano
      • Nyuki
    • Muundo wa Halmashauri
  • Fursa za Uwekezaji
    • Utalii
    • Uchimbaji Madini
    • Kilimo
    • Mifugo
  • Huduma Zetu
    • Huduma za afya
    • Huduma za elimu
    • Huduma za Maji
    • Huduma za kilimo
    • Huduma za Mifugo
    • Huduma za Ardhi na Maliasili
    • Huduma za Watumishi
  • Madiwani
    • This page is under construction
    • Kamati za kudumu za Halmashauri
      • Fedha na uongozi
      • Mipango miji na Mazingira
      • Uchumi,Afya na Elimu
      • Ukimwi
      • Maadili
    • Ratiba
  • Miradi
    • Miradi mipya
    • Miradi inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
  • Machapisho
    • Sheria ndogo
    • Mkataba wa huduma kwa wateja
    • Mpango mkakati
    • Taarifa mbalimbali
    • Fomu mbalimbali
    • Miongozo mbalimbali
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa kwa Umma
    • Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha

Zoezi la upigaji chapa ng’ombe wilayani Kiteto lapokelewa vizuri baada ya wafugaji kuelimishwa

Imetumwa : November 25th, 2017

                                                                                                                                                                                                Ng'ombe anavyoonekana baada ya kupigwa chapa katika zoezi la upigaji chapa  ng'ombe lililozinduliwa katika kata ya Namelock wilayani Kiteto  tarehe 24/11/2017         

               Ng'ombe wakisubiri kupigwa chapa  katika uzinduzi wa zoezi la upigaji chapa wilayani Kiteto

                                                                                 Viongozi wa wilaya ya Kiteto wakisubiri  uzinduzi wa  zoezi la upigaji chapa ngombe wilayani Kiteto                                                                              

                                                              Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mh. Tumaini Magessa akizungumza kuhusu zoezi la upigaji chapa ngombe                                                                                              

   Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Mh. Hassani Benzi akizungumza kuhusu zoezi la upigaji chapa ng'ombe

Diwani  wa kata ya Partimbo Mh. Paulo Tunyoni  akizungumza kuhusu zoezi la upigaji chapa ngombe  wilayani Kiteto

              Afisa mifugo wilaya ya Kiteto ndugu William Msuya  akizungumza kuhusu zoezi la upigaji chapa ngombe  

              Kiongozi wa mila kutoka jamii ya Wafugaji  wanaoishi wilayani Kiteto ndugu Ngayoni  Lebakari akizungumza kuhusu zoezi la upigaji chapa ngombe 

        Mkuu wa wilaya ya Kiteto Mh.  Tumaini Magessa  akipiga  chapa ng'ombe  katika uzinduzi wa zoezi la upigaji chapa ng'ombe wilayani Kiteto


                                       Makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto Mh. Hassan Benzi  akipiga  chapa ng'ombe  katika uzinduzi wa zoezi la upigaji chapa ng'ombe wilayani Kiteto


       Afisa mifugo wilaya ya Kiteto ndugu William Msuya akipiga  chapa ng'ombe katika  uzinduzi wa zoezi la upigaji chapa ng'ombe wilayani Kiteto


HABARI KAMILI.......

Zoezi la upigaji chapa ng’ombe wilayani Kiteto  lapokelewa vizuri  baada ya Wafugaji  kuelimishwa


Zoezi la upigaji chapa ng’ombe wilayani Kiteto limepokelewa vizuri na wafugaji baada ya wafugaji hao kuelimishwa juu ya umuhimu wa zoezi hilo.Akizungumza katika uzinduzi wa zoezi hilo lililofanyika  tarehe 24/11/2017 katika kata ya Namelock Mkuu wa wilaya ya Kiteto mheshimiwa Tumaini Magessa amesema kwamba zoezi hilo limepokelewa vizuri baada ya wafugaji  kupewa elimu ya kutosha  .

Kuhusu kusuasua kuanza kwa zoezi hilo mheshimiwa Magessa amesema kwamba, zoezi hilo limesuasua kwa sababu wahusika walitaka kulifanya bila kutoa elimu .Mheshimiwa Magessa  anasema ‘‘kazi tuliyoifanya kwanza ni kuwapa wafugaji elimu ya kutosha.Tumewaita viongozi wa wafugaji,Maleigwanan na wafugaji ,tumekaa nao,tumezungumza nao, ,wakalifahamu zoezi hili lina faida gani na hasara gani , tukakubaliana. Kwa hiyo niseme tu kwamba faida za zoezi hili hazikuwa zimefahamika kwa wananchi vizuri, na hivyo ikaonekana kama wanalipinga.Kuna watu ambao walipita wakieleza kwamba ng’ombe akipigwa chapa atakaa miaka minne bila kuzaa , na wafugaji wakajua hii ni hasara. Kama ng’ombe atakaa miaka minne bila kuzaa ni hasara kubwa,lakini tulivyowapa elimu kwamba huu ni utambuzi wa mifugo kwa maana kwamba sasa tukishajua idadi ya mifugo ,tutawapa sehemu ya malisho, tutaandaa malisho, tutafika mahali kwenye masoko kwa hiyo wizi wa ng’ombe utapungua, na vitu vingine kama hivyo, wafugaji wakaona kwamba kumbe hili suala lilikuwa halikuelezwa vizuri, .Ndio sababu unaona sasa tunaanza kulifanyia ’’

Naye  makamu mwenyekiti wa halmashauri ya wilaya ya Kiteto mheshimiwa Hassan Benzi amesema kwamba wamekubaliana kuwa zoezi hilo la upigaji chapa liende sambamba  na  chanjo kwa ajili ya homa ya mapafu ambayo imekuwa tatizo kubwa sana kwa wafugaji wao. Kila mfugaji atachangia shilingi mia tano kwa ng’ombe mmoja  kwa ajili ya kupata chanjo hiyo.

Katika hatua nyingine  diwani wa kata ya Partimbo mheshimiwa Paulo Tunyoni  ambaye pia ni  mwenyekiti wa kamati ya uchumi na mazingira amezungumza kuhusu watu waliokuwa wakieneza taarifa zisizofaa juu ya zoezi la upigaji chapa.Mheshimiwa tunyoni amesema ‘‘Wanasiasa waliokuwa wanasema kwamba chapa sio nzuri walikuwa hawajapata uelewa, lakini baada ya kuagiza kwenye baraza watu waelimishwe, tumeelewa kwamba chapa  ina umuhimu  mkubwa sana, umuhimu wa chapa ni nini, umuhimu wa chapa  ni kujua idadi ya ng’ombe tulizonazo ambapo unatupeleka sisi kwenda sasa kuhangaika kuhakikisha kwamba mifugo yetu kutokana na wingi uliopo kwenye kijiji fulani inakuwa na maeneo ya kutosha kwa ajili ya malisho ’’ Mheshimiwa Tunyoni anaendelea kusema kwamba  serikali imeliona hilo, na ndio maana imeagiza utekelezaji wa upigaji chapa ili kuhakikisha kwamba mifugo iliyo katika kijiji A inalingana na malisho yaliyopo  katika kijiji A.

Kwa upande wake Afisa mifugo wa wilaya ya Kiteto  ndugu William Msuya amesema kwamba anamshukuru Mungu zoezi hilo limeanza, lakini kulikuwa na changamoto kidogo kwa sababu ya uelewa wa vijana  wa Kimasai wanaoitwa Nyangulo, ambao walitaka kuingilia zoezi bila ridhaa ya wazazi wao,lakini baada ya wazazi wao kuwapa elimu kama walivyopewa wao, zoezi  limeenda vizuri. Kuhusu taarifa za upotoshaji wa zoezi hilo Msuya anasema ‘‘taarifa walizokuwa wanapata wafugaji  kwamba mifugo  ikipigwa chapa haizai ni upotoshaji na uzushi, ambao ulitengenezwa kwa lengo la kukwamisha zoezi hili .Lakini baada  ya kupatiwa elimu  na wataalamu na kupitia viongozi  wetu wa kisiasa, mkuu wa wilaya, mwenyekiti wa halmashauri na viongozi wote kupitia baraza la madiwani, wamepata uelewa wa kutosha na zoezi limeenda vizuri’’.

Naye kiongozi wa mila ndugu Ngayoni  Lebakari  amesema kwamba  zoezi hilo  wamelipokea vizuri,baada ya viongozi wa  mila kuitwa  tarehe 18/11 /2017 kwenye ukumbi wa halmashauri ,ambapo walielezwa na kupewa elimu kuhusu zoezi hilo. Lakini  kabla  hawajapata elimu, wafugaji walikuwa wanasuasua kukubali ng’ombe wao kupigwa chapa. Walikuwa wakihoji kwamba chapa ikoje, kwanini hawajaelezwa,lakini  baada ya kupata  elimu kutoka kwa viongozi ambao walipewa elimu , walielewa kwamba  upigaji chapa hauna madhara bali una faida,   wamelipokea zoezi hilo vizuri.

 Kuhusu ngombe walio nje ya wilaya, mkuu wa wilaya ya Kiteto  mheshimiwa Tumaini Magessa amesema kwamba kuna ng’ombe ambao wako nje ya wilaya kwa ajili ya kutafuta malisho,lakini huu ni mwezi ambao wanaanza kurudi,kwa hiyo wameanza kupiga chapa wakijua kwamba ndani ya miezi miwili  watakuwa wamemaliza zoezi kwa ng’ombe wote. Aidha  mheshimiwa magessa amesema kwamba wako ng’ombe wanaozaliwa, na wako wanaoendelea kuja kutoka wilaya nyingine kwa sababu ya kununuliwa , na kwa  hao pia watakuja kufanya zoezi hilohilo ,kama watakuja na chapa, maana yake makaratasi na hati ambazo watakuwa wamekuja nazo ndio zitawatambulisha kwamba wametoka wapi. Wilaya ya Kiteto ina  ngombe  zaidi ya 487,000, ambapo katika zoezi hilo ng’ombe 350,000 wanatarajiwa kupigwa chapa.



Matangazo

  • TAARIFA KWA UMMA 11.06.2025 June 11, 2025
  • TANGAZO NAFASI YA KAZI- MWENYEKITI BODI YA MFUKO WA ELIMU June 08, 2025
  • KUITWA KWENYE USAILI JUNI 2025 June 07, 2025
  • TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI June 06, 2025
  • Angalia zote

Habari mpya

  • MAFUNZO YA MFUMO WA E-UTENDAJI KWA WATUMISHI.

    June 12, 2025
  • KIKAO CHA MAANDALIZI YA MWENGE WA UHURU 2025

    June 11, 2025
  • WATOTO WA UMISSETA KITETO, WAWATOA JASHO WATU WAZIMA!

    June 10, 2025
  • WALIMU KITETO WAPEWA MAFUNZO YA AFUA JUMUISHI ZA ELIMU YA AFYA SHULENI

    June 05, 2025
  • Angalia zote

Video za matukio ya kiofisi na kitaifa.

MWENGE MAKABIDHIANO MKOA WA MANYARA 2018
Video Zaidi

Kiunganishi cha Haraka

  • Kupata Hati ya Mshahara

Viunganishi vya Tovuti Nyingine

  • TAMISEMI
  • UTUMISHI
  • IKULU
  • MANYARA
  • NECTA
  • eGA

World visitors tracker

world map hits counter

Hesabu ya watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya mahali

Wasiliana nasi

    Kibaya-Kiteto

    Anwani ya Posta: P.o.Box 98, Kibaya-Kiteto

    Simu ya Mezani: +255 027-2552099

    Simu ya kiganjani:

    Barua Pepe: ded@kitetodc.go.tz

Mawasiliano mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Eneo

Hakimiliki@2017 Halimashauri ya Kiteto.Haki zote zimehifadhiwa